Je! ni sahihi kuning’iniza picha nyumbani mwako kama ya Yesu?

0
6K

Swali linaendelea…maana imeandikwa kutoka 20:4 “Usijifanyie sanamu ya kuchonga, wala mfano wa kitu cho chote kilicho juu mbinguni, wala kilicho chini duniani, wala kilicho majini chini ya dunia. “

Sasa naomba kufahamu kufanya hivyo ni makosa?


JIBU: kwa kulijibu hili swali tumalizie kusoma mstari huo..

Kutoka 20:4-5″ Usijifanyie sanamu ya kuchonga, wala mfano wa kitu cho chote kilicho juu mbinguni, wala kilicho chini duniani, wala kilicho majini chini ya dunia.
5 Usivisujudie wala kuvitumikia; kwa kuwa mimi, Bwana, Mungu wako, ni Mungu mwenye wivu; nawapatiliza wana maovu ya baba zao, hata kizazi cha tatu na cha nne cha wanichukiao,”…

Sasa tunaona katika huo mstari wa tano msisitizo umewekwa pale katika neno “USIVISUJUDIE WALA KUVITUMIKIA”, lakini sio kwamba ukiweka picha yoyote kama ya Yesu nyumbani mwako ni vibaya hapana! unaweza kuweka picha yoyote upendayo ilimradi iwe ni njema,

Maana tukisema tusiweke picha yoyote basi hata tunaponing’iniza picha zetu wenyewe ukutani majumbani mwetu tunafanya vibaya kwasababu maandiko yanasema usijifanyie mfano wa kitu chochote sio tu kilicho juu mbinguni bali hata kilichopo chini duniani.

Unaona hapo msisitizo ni kwamba unapoweka picha yoyote au sanamu yoyote hupaswi kuiabudu wala kuisujudia kwa kufanya hivyo ni machukizo makubwa mbele za Mungu. Lakini leo hii kuna baadhi ya watu,na dini na madhehebu yanaabudu sanamu za Yesu na bikira Mariamu au watakatifu waliokufa zamani za kale hao ni dhahiri kuwa wanamwabudu shetani aidha kwa kujua au kwa kutokujua.

Ikiwa wewe ni mkatoliki na unayo sanamu ya Yesu au sanamu ya bikira Maria nyumbani mwako, nashauri iondoe haraka sana, kwasababu dini hiyo inaahusisha ibada zao na sanamu, vinginevyo utamtia Mungu wivu na kujikuta umeenda Jehanamu.

Lakini kama picha ipo kwa ajili ya urembo au kwa ajili ya kufikisha tu ujumbe fulani katika mazingira yanayokuzunguka au nyumbani kwako, wala husujudii wala kuabudu basi hakuna shida yoyote. Zingatia tu hilo neno ”USIVISUJUDIE WALA KUVITUMIKIA’ kwasababu yeye ni Mungu mwenye wivu.

Biblia inasema;

1 Wakorintho 10:14

[14]Kwa ajili ya hayo, wapenzi wangu, ikimbieni ibada ya sanamu.
[15]Nasema kama na watu wenye akili; lifikirini ninyi ninenalo.

Ubarikiwe sana.

Pesquisar
Categorias
Leia Mais
MAHUSIANO KIBIBLIA
MWANAMKE NA MWANAUME NA MAHUSIANO: TOFAUTI YA KIMAUMBILE
Sote tunajua kabisa ya kwamba kuna tofauti ya kimaumbile kati ya mwanaume na mwanamke, na tofauti...
Por GOSPEL PREACHER 2021-11-07 23:11:12 0 5K
DEUTERONOMY
Verse by verse explanation of Deuteronomy 8
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 21 questions at the...
Por THE HOLY BIBLE 2022-01-25 05:56:32 0 6K
OTHERS
UTATA KATIKA UUMBAJI WA MAJINI
ALLAH: UTATA KATIKA UUMBAJI WA MAJINIJe, Majini yaliumbwaje?Leo hii tutajifunza UTATA wa Allah...
Por MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-23 08:20:08 0 5K
NDOA KIBIBLIA
HATUA TATU MUHIMU KABLA YA KUFUNGA PINGU ZA MAISHA
Mojawapo ya swali gumu kuhusiana na mahusiano ni pale vijana wanapouliza wakae kwenye uchumba kwa...
Por GOSPEL PREACHER 2021-11-06 14:30:07 0 6K
OTHERS
JE NGUVU ZA GIZA ZIPO?
  Wapo watu wachache ambao huwa hawaamini habari za utendaji wa nguvu za giza,. na wengine...
Por MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-22 03:23:23 0 6K