NANI ALIYE TOLEWA KAFARA, ISHMAEL AU ISAKA?

0
5Кб
Kwenye Mwanzo 22:1-18, je inawezekana kuwa mvulana ambaye Abraham alikaribia kumtoa kafara awe ni Ishmael, siyo Isaka, kama ambavyo Waislam wanadai? Vinginevyo, inawezekanaje Isaka awe "mtoto pekee wa kiume" wa Abram?
Jibu: Ni Isaka aliyetolewa kafara na si Ishmael kwa sababu angalau nne:
 
Hata Kurani haisemi kuwa alikuwa ni Ishmael: Mwanzo 22:2 inasema alikuwa ni Isaka. Kwa Waislam, ingawa Kurani ya kiislam inazungumzia jambo hili kwenye Sura 37:99-111, hakuna sehemu yoyote kwenye Kurani nzima inayosema kuwa huenda alikuwa Ishmael au Isaka. Kwa hakika, wanazuoni wengi wa awali wa kiislam walifundisha kuwa alikuwa ni Isaka, wakati wengine walifundisha kuwa alikuwa ni Ishmael. Tazama al-Tabari juzuu ya 2 uk.68. al-Tabari juzuu ya 2 uk.82-97 inasema mabingwa 16 wa kiislam walisema kuwa ni Isaka wakati mabingwa 23 wa kiislam walisema kuwa ni Ishmael.
 
Abram alikuwa na mtoto mmoja tu wa kiume wakati ule: Ishmael alikuwa na miaka 14 wakati Isaka alipozaliwa. Hajiri na Ishamael walifukuzwa na kwenda sehemu nyingine Isaka alipoachishwa kunyonya kwenye Mwanzo 21:8-10. Abraham alijaribiwa "kwa muda mrefu" baada ya hapo kwenye Mwanzo 21:34, na "mtoto wa kiume" alikuwa kwenye meza ya kutolea kafara kwenye Mwanzo 22:12.
 
Mrithi pekee: Isaka alikuwa mirthi pekee, na mtoto pekee wa kiume, pia inamaanisha "mtoto wa kiume mpendwa". Ingawa utamaduni wa wakati ule uliruhusu watu kuwa na masuria kwa ajili ya kupata watoto, urithi na haki ya mzaliwa wa kwanza vilienda kwa watoto wa kiume wa mke halisi, siyo watoto wa kiume wa masuria. Tazama Mambo Magumu kwenye Biblia na Mambo Yanayoonekana Kupingana uk.141 kwa maelezo kamili.
 
Mwana pekee wa ahadi: Mwanzo 21:12 inasema, "katika Isaka uzao wako utatajwa." Abraham alikuwa na watoto wengine pia wa kiume, lakini walizaliwa baada ya ahadi hii.
Ni mimi Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo
Поиск
Категории
Больше
REVELATION
UFUNUO 19
Karibu tujifunze biblia na huu ni mwendelezo wa kitabu cha Ufunuo leo tukiwa katika ule mlango wa...
От GOSPEL PREACHER 2021-10-30 12:21:07 6 6Кб
OTHERS
ALLAH KWA KIEBRANIA MAANA YAKE NI LAANA “CURSE”
Ndugu msomaji, Je, hili limetokea kwa bahati mbaya? Isaya 24: 6 Ndiyo sababu laana...
От MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-24 21:05:20 0 7Кб
NUMBERS
Verse by verse explanation of Numbers 17
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 24 questions at the...
От THE HOLY BIBLE 2022-01-24 14:58:31 0 5Кб
OTHERS
KWANINI SULEIMAN ALIKUWA NA WAKE MIA SABA (700) NA MASURIA MIA TATU (300)?
Kwenye 1 WaFalme 11:1-3, kwa nini Suleiman alikuwa na wake 700 na Masuria 300, kinyume cha amri...
От MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-24 21:03:13 0 5Кб
DEUTERONOMY
Verse by verse explanation of Deuteronomy 22
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 29 questions at the...
От THE HOLY BIBLE 2022-01-25 06:35:24 0 5Кб