NANI ALIYE TOLEWA KAFARA, ISHMAEL AU ISAKA?

0
5KB
Kwenye Mwanzo 22:1-18, je inawezekana kuwa mvulana ambaye Abraham alikaribia kumtoa kafara awe ni Ishmael, siyo Isaka, kama ambavyo Waislam wanadai? Vinginevyo, inawezekanaje Isaka awe "mtoto pekee wa kiume" wa Abram?
Jibu: Ni Isaka aliyetolewa kafara na si Ishmael kwa sababu angalau nne:
 
Hata Kurani haisemi kuwa alikuwa ni Ishmael: Mwanzo 22:2 inasema alikuwa ni Isaka. Kwa Waislam, ingawa Kurani ya kiislam inazungumzia jambo hili kwenye Sura 37:99-111, hakuna sehemu yoyote kwenye Kurani nzima inayosema kuwa huenda alikuwa Ishmael au Isaka. Kwa hakika, wanazuoni wengi wa awali wa kiislam walifundisha kuwa alikuwa ni Isaka, wakati wengine walifundisha kuwa alikuwa ni Ishmael. Tazama al-Tabari juzuu ya 2 uk.68. al-Tabari juzuu ya 2 uk.82-97 inasema mabingwa 16 wa kiislam walisema kuwa ni Isaka wakati mabingwa 23 wa kiislam walisema kuwa ni Ishmael.
 
Abram alikuwa na mtoto mmoja tu wa kiume wakati ule: Ishmael alikuwa na miaka 14 wakati Isaka alipozaliwa. Hajiri na Ishamael walifukuzwa na kwenda sehemu nyingine Isaka alipoachishwa kunyonya kwenye Mwanzo 21:8-10. Abraham alijaribiwa "kwa muda mrefu" baada ya hapo kwenye Mwanzo 21:34, na "mtoto wa kiume" alikuwa kwenye meza ya kutolea kafara kwenye Mwanzo 22:12.
 
Mrithi pekee: Isaka alikuwa mirthi pekee, na mtoto pekee wa kiume, pia inamaanisha "mtoto wa kiume mpendwa". Ingawa utamaduni wa wakati ule uliruhusu watu kuwa na masuria kwa ajili ya kupata watoto, urithi na haki ya mzaliwa wa kwanza vilienda kwa watoto wa kiume wa mke halisi, siyo watoto wa kiume wa masuria. Tazama Mambo Magumu kwenye Biblia na Mambo Yanayoonekana Kupingana uk.141 kwa maelezo kamili.
 
Mwana pekee wa ahadi: Mwanzo 21:12 inasema, "katika Isaka uzao wako utatajwa." Abraham alikuwa na watoto wengine pia wa kiume, lakini walizaliwa baada ya ahadi hii.
Ni mimi Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo
Suche
Kategorien
Mehr lesen
OTHERS
Bible Verses about Honoring Parents
The New Testament binds a great responsibility on children when it says in Ephesians 6, verses...
Von MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-23 10:58:36 0 7KB
OTHERS
Why did Jesus teach in parables?
It has been said that a parable is an earthly story with a heavenly meaning. The Lord Jesus...
Von MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-23 10:39:04 0 5KB
DEUTERONOMY
Verse by verse explanation of Deuteronomy 8
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 21 questions at the...
Von THE HOLY BIBLE 2022-01-25 05:56:32 0 6KB
1 CHRONICLES
Verse by verse explanation of 1 Chronicles 25
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 21 questions at the...
Von THE HOLY BIBLE 2022-03-20 05:18:30 0 6KB
2 CHRONICLES
Verse by verse explanation of 2 Chronicles 19
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 25 questions at the...
Von THE HOLY BIBLE 2022-04-02 01:41:14 0 5KB