NANI ALIYE TOLEWA KAFARA, ISHMAEL AU ISAKA?

0
5χλμ.
Kwenye Mwanzo 22:1-18, je inawezekana kuwa mvulana ambaye Abraham alikaribia kumtoa kafara awe ni Ishmael, siyo Isaka, kama ambavyo Waislam wanadai? Vinginevyo, inawezekanaje Isaka awe "mtoto pekee wa kiume" wa Abram?
Jibu: Ni Isaka aliyetolewa kafara na si Ishmael kwa sababu angalau nne:
 
Hata Kurani haisemi kuwa alikuwa ni Ishmael: Mwanzo 22:2 inasema alikuwa ni Isaka. Kwa Waislam, ingawa Kurani ya kiislam inazungumzia jambo hili kwenye Sura 37:99-111, hakuna sehemu yoyote kwenye Kurani nzima inayosema kuwa huenda alikuwa Ishmael au Isaka. Kwa hakika, wanazuoni wengi wa awali wa kiislam walifundisha kuwa alikuwa ni Isaka, wakati wengine walifundisha kuwa alikuwa ni Ishmael. Tazama al-Tabari juzuu ya 2 uk.68. al-Tabari juzuu ya 2 uk.82-97 inasema mabingwa 16 wa kiislam walisema kuwa ni Isaka wakati mabingwa 23 wa kiislam walisema kuwa ni Ishmael.
 
Abram alikuwa na mtoto mmoja tu wa kiume wakati ule: Ishmael alikuwa na miaka 14 wakati Isaka alipozaliwa. Hajiri na Ishamael walifukuzwa na kwenda sehemu nyingine Isaka alipoachishwa kunyonya kwenye Mwanzo 21:8-10. Abraham alijaribiwa "kwa muda mrefu" baada ya hapo kwenye Mwanzo 21:34, na "mtoto wa kiume" alikuwa kwenye meza ya kutolea kafara kwenye Mwanzo 22:12.
 
Mrithi pekee: Isaka alikuwa mirthi pekee, na mtoto pekee wa kiume, pia inamaanisha "mtoto wa kiume mpendwa". Ingawa utamaduni wa wakati ule uliruhusu watu kuwa na masuria kwa ajili ya kupata watoto, urithi na haki ya mzaliwa wa kwanza vilienda kwa watoto wa kiume wa mke halisi, siyo watoto wa kiume wa masuria. Tazama Mambo Magumu kwenye Biblia na Mambo Yanayoonekana Kupingana uk.141 kwa maelezo kamili.
 
Mwana pekee wa ahadi: Mwanzo 21:12 inasema, "katika Isaka uzao wako utatajwa." Abraham alikuwa na watoto wengine pia wa kiume, lakini walizaliwa baada ya ahadi hii.
Ni mimi Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo
Αναζήτηση
Κατηγορίες
Διαβάζω περισσότερα
1 CHRONICLES
Verse by verse explanation of 1 Chronicles 28
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 25 questions at the...
από THE HOLY BIBLE 2022-03-20 05:23:17 0 6χλμ.
Injili Ya Yesu Kristo
MBINGUNI, PEPONI, KUZIMU NA JEHANNAM NI WAPI?
Mpendwa mmoja aliniuliza maswali yafuatayo ambayo nimeona ni muhimu niyajibu kama Makala fupi kwa...
από MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-25 11:56:58 0 7χλμ.
OTHERS
Jesus and Islam
Here are six questions that followers of Islam, and others, often ask about Jesus... This will...
από MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-23 09:45:24 0 6χλμ.
MASWALI & MAJIBU
Kubatizwa kwa ajili ya wafu ndio kupi, kuonakozungumziwa katika 1 Wakoritho 15:29?
Wenye kubatizwa kwa ajili ya wafu ni wakina nani? Swali linaendelea… kulingana na huu...
από GOSPEL PREACHER 2022-06-12 23:32:15 0 5χλμ.
JOB
Verse by verse explanation of Job 38
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 31 questions at the...
από THE HOLY BIBLE 2022-04-03 04:20:58 0 6χλμ.