FAHAMU UWEZO WA DAMU YA YESU KRISTO

0
6KB

Ukweli ni kwamba katika damu ya Yesu Kristo kunapatikana zaidi ya mambo manne nitakayokushirikisha humu; lakini kwa sasa naona nianze na haya manne:-

  1. Uwezo wa Damu ya Yesu Kristo katika kuondoa dhambi. Imeandikwa katika kitabu cha 1Yohana 1:9 kuwa; “Tukiziungama dhambi zetu, Yeye ni mwaminifu na wa haki hata ATUONDOLEE dhambi zetu, na kutusafisha na udhalimu wote”.

 

  1. Uwezo wa Damu ya Yesu Kristo katika kupatanisha. Imeandikwa katika kitabu cha Waefeso 2:13-16 kuwa; “Lakini sasa, katika Kristo Yesu, ninyi mliokuwa mbali hapo kwanza mmekuwa karibu kwa damu yake Kristo. Kwa maana yeye ndiye amani yetu, aliyetufanya sisi sote tuliokuwa wawili kuwa mmoja; akakibomoa kiambaza cha kati kilichotutenga. Naye akiisha kuuondoa ule uadui kwa mwili wake; ndiyo sheria ya amri zilizo katika maagizo; ili afanye hao wawili kuwa mtu mpya mmoja ndani ya nafsi yake; akafanya amani. AKAWAPATANISHA wote wawili na Mungu katika mwili mmoja, kwa njia ya msalaba, akiisha kuufisha ule uadui kwa huo msalaba”

 

  1. Uzima wa Milele katika Damu ya Yesu Kristo. Imeandikwa katika kitabu cha Yohana 6:53-54 kuwa; “Basi Yesu akawaambia Amini, amini, nawaambieni, msipoula mwili wake mwana wa Adamu nakuinywa damu yake, hamna uzima ndani yenu. Aulaye mwili wangu na kuinywa damu yangu anao UZIMA WA MILELE…..”

 

  1. Uwezo wa Damu ya Yesu Kristo katika kutulinda. Imeandikwa katika kitabu cha ufunuo wa Yohana 12:11a kuwa; “Nao wakamshinda (shetani) kwa damu ya mwana-Kondoo….” Mtihani mkubwa sana kwetu sisi wakristo ni kuyaweka katika matendo yale tunayofahamu katika Biblia. Nakushauri kwa Jina la Yesu Kristo kuwa uwe mtendaji wa neno, na usiwe msomaji tu. Ni maombi yangu kwa Bwana ya kuwa Roho wa ufahamu wa Bwana atakuwa juu yako unaposoma na ketenda neno lake.

 

Pesquisar
Categorias
Leia mais
OTHERS
Yesu Aongea na Binti wa Kiislamu; Binti Aokoka
Sharoni hakuwa Mkristo bali alikuwa ni binti wa Kiislamu. Na wala hakuwa amewahi kujifunza habari...
Por MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-23 09:22:01 0 5KB
2 SAMUEL
Verse by verse explanation of 2 Samuel 4
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 22 questions at the...
Por THE HOLY BIBLE 2022-02-05 09:20:26 0 5KB
OTHERS
IS MUHAMMAD THE SPIRIT OF TRUTH?
Today I will answer Muhammadans with biblical proof that Muhammad was not the Spirit of Truth as...
Por MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-22 02:25:52 0 5KB
REVELATION
UTAWALA WA MIAKA 1000
Shalom mtu wa Mungu, karibu tujifunze maandiko matakatifu, kama Biblia inavyosema...
Por GOSPEL PREACHER 2021-10-30 12:39:10 0 6KB
NUMBERS
Verse by verse explanation of Numbers 9
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 26 questions at the...
Por THE HOLY BIBLE 2022-01-24 14:30:57 0 5KB