FAHAMU UWEZO WA DAMU YA YESU KRISTO

0
6K

Ukweli ni kwamba katika damu ya Yesu Kristo kunapatikana zaidi ya mambo manne nitakayokushirikisha humu; lakini kwa sasa naona nianze na haya manne:-

  1. Uwezo wa Damu ya Yesu Kristo katika kuondoa dhambi. Imeandikwa katika kitabu cha 1Yohana 1:9 kuwa; “Tukiziungama dhambi zetu, Yeye ni mwaminifu na wa haki hata ATUONDOLEE dhambi zetu, na kutusafisha na udhalimu wote”.

 

  1. Uwezo wa Damu ya Yesu Kristo katika kupatanisha. Imeandikwa katika kitabu cha Waefeso 2:13-16 kuwa; “Lakini sasa, katika Kristo Yesu, ninyi mliokuwa mbali hapo kwanza mmekuwa karibu kwa damu yake Kristo. Kwa maana yeye ndiye amani yetu, aliyetufanya sisi sote tuliokuwa wawili kuwa mmoja; akakibomoa kiambaza cha kati kilichotutenga. Naye akiisha kuuondoa ule uadui kwa mwili wake; ndiyo sheria ya amri zilizo katika maagizo; ili afanye hao wawili kuwa mtu mpya mmoja ndani ya nafsi yake; akafanya amani. AKAWAPATANISHA wote wawili na Mungu katika mwili mmoja, kwa njia ya msalaba, akiisha kuufisha ule uadui kwa huo msalaba”

 

  1. Uzima wa Milele katika Damu ya Yesu Kristo. Imeandikwa katika kitabu cha Yohana 6:53-54 kuwa; “Basi Yesu akawaambia Amini, amini, nawaambieni, msipoula mwili wake mwana wa Adamu nakuinywa damu yake, hamna uzima ndani yenu. Aulaye mwili wangu na kuinywa damu yangu anao UZIMA WA MILELE…..”

 

  1. Uwezo wa Damu ya Yesu Kristo katika kutulinda. Imeandikwa katika kitabu cha ufunuo wa Yohana 12:11a kuwa; “Nao wakamshinda (shetani) kwa damu ya mwana-Kondoo….” Mtihani mkubwa sana kwetu sisi wakristo ni kuyaweka katika matendo yale tunayofahamu katika Biblia. Nakushauri kwa Jina la Yesu Kristo kuwa uwe mtendaji wa neno, na usiwe msomaji tu. Ni maombi yangu kwa Bwana ya kuwa Roho wa ufahamu wa Bwana atakuwa juu yako unaposoma na ketenda neno lake.

 

Zoeken
Categorieën
Read More
Injili Ya Yesu Kristo
EPUKA UONGO UKIENDELEA KUTENDA DHAMBI BAADA YA KUOKOKA, HUENDI MBINGUNI KAMWE / IF YOU CONTINUE TO SIN AFTER BEING SAVED, YOU WILL NOT GO TO HEAVEN
SWAHILI: Bwana Yesu (ambaye ni Mungu mkuu na mwokozi wetu, Tito 2:13)  asifiweeee! Lengo la...
By PROSPER HABONA 2022-01-16 14:16:25 0 6K
PSALMS
Verse by verse explanation of Psalm 16
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 19 questions at the...
By THE HOLY BIBLE 2022-05-20 11:58:21 0 7K
Religion
HOW TO BECOME A CHRISTIAN?
This question is very important, and not all human beings know its answer. But it is very simple...
By GOSPEL PREACHER 2021-08-25 10:01:32 0 5K
GENESIS
Verse by verse explanation of Genesis 48
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 21 questions at the...
By THE HOLY BIBLE 2022-01-21 10:11:32 0 6K
MASWALI & MAJIBU
Ubatizo Wa Moto Ni Upi?
JIBU: Ni kweli Yohana alibatiza kwa maji na alisema Bwana YESU atakapokuja atatubatiza kwa...
By GOSPEL PREACHER 2022-06-13 09:44:22 0 6K