Je, Mkristo anapaswa kufanya nini kama yeye ameolewa na asiyeamini?

0
5K
Kuoleka na kafiri inaweza kuwa mojawapo ya changamoto ngumu sana katika maisha ya Mkristo. Ndoa ni agano takatifu ambalo linaunganisha watu wawili pamoja katika mwili mmoja (Mathayo 19:5). Inaweza kuwa vigumu sana kwa muumini na kafiri kuishi kwa amani na umoja (2 Wakorintho 6:14-15). Kama mpenzi mmoja anakuwa Mkristo baada ya ndoa, mapambano asili ya kuishi chini ya mamlaka aina mbili tofauti huwa huwa dhahiri.
 
Mara nyingi Wakristo katika hali hii hutafuta njia ya kujinazua kutoka kwa ndoa, wakiamini kwamba hii ndio njia pekee ya kweli ambayo italeta utukufu kwa Mungu. Neno lake, hata hivyo, linasema kinyume chake. Ni muhimu sana kutoridhika na hali yetu pekee, bali pia kutafuta njia ya kuleta utukufu kwake mbali na changamoto zetu (1 Wakorintho 7:17). Biblia hasa inahusu wale ambao wameolewa na wasioamini katika 1 Wakorintho 7:12-14: "... iwapo ndugu mmoja ana mke asiyeamini, na mke huyo anakubali kukaa naye asiwmeache. Na mwanamke ambaye ana mume asiyeamini, na mume huyo anakubali kukaa naye, asimwache mumewe. Kwa maana Yule mume asiyeamini hutakaswa katika mkewe; na Yule mke asiyeamini hutakswa katika mumewe; kama asiengekuwa hivyo, watot wenu wengekuwa si safi..."
 
Wakristo ambao wameoleka kwa wasioamini wanahitaji kuomba kwa ajili ya nguvu za Roho Mtakatifu ili kuwawezesha kukiri Kristo na kuishi katika mwanga wa uwepo wa Mungu (1 Yohana 1:7). Wanapaswa kutafuta nguvu za Mungu za ubadilisho kubadili nyoyo zao na kuzaa matunda ya Roho Mtakatifu (Wagalatia 5:22-23). Mke Mkristo ana wajibu wa kuwa na moyo mtiifu, hata kwa mume wake ambaye si mkristo (1 Petro 3:01), na atahitaji kubaki karibu na Mungu na kutegemea neema yake kumwezesha kufanya hivyo.
 
Wakristo hawastahili kuishi maisha ya upweke wanahitaji kupata msaada kutoka kwingine kama vile kanisa na makundi ya kujifunza Biblia. Kuolewa na kafiri haina haibadilishi utakatifu wa uhusiano, hivyo ni lazima iwe kipaumbele cha kila Mkristo kuomba kwa ajili ya mke wake na kuweka mfano mzuri, kuruhusu mwanga wa Kristo kuangaza (Wafilipi 2:14). Bu na ukweli ulio katika 1 Petro 3:1-kwamba mwanandoa asiyeamini "amevutwa kwa Kristo"n iwe tumaini na lengo la kila Mkristo ambaye ameoleka kwa mtu asiye Mkristo.
Site içinde arama yapın
Kategoriler
Read More
MASWALI & MAJIBU
Je! Mtu Anapofunga Kwa Muda Wa SAA 24,Anapaswa Kunywa Maji Au Kitu Chochote?
JIBU: Biblia haijatoa masharti yoyote ya kufuata katika kufunga kwamba ufunge masaa 12 au 26...
By GOSPEL PREACHER 2022-06-14 13:38:28 0 8K
Injili Ya Yesu Kristo
Ubatizo wa Rohoho Mtakatifu ni nini?
Ubatizo wa Roho mtakatifu unaweza kufafanuliwa/kuelezwa kuwa ile kazi ambayo Roho Mtakatifu wa...
By MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-24 04:05:10 0 5K
DIPLOMA
DIPLOMA
List of all subjects for the students who are taking diploma courses.
By PROSHABO ONLINE SCHOOLS 2021-10-09 10:54:15 0 6K
EXODUS
Verse by verse explanation of Exodus 26
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 35 questions at the...
By THE HOLY BIBLE 2022-01-22 18:15:15 0 5K
NUMBERS
Verse by verse explanation of Numbers 20
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 29 questions at the...
By THE HOLY BIBLE 2022-01-24 15:03:01 0 5K