Je, Mkristo anapaswa kufanya nini kama yeye ameolewa na asiyeamini?

0
5KB
Kuoleka na kafiri inaweza kuwa mojawapo ya changamoto ngumu sana katika maisha ya Mkristo. Ndoa ni agano takatifu ambalo linaunganisha watu wawili pamoja katika mwili mmoja (Mathayo 19:5). Inaweza kuwa vigumu sana kwa muumini na kafiri kuishi kwa amani na umoja (2 Wakorintho 6:14-15). Kama mpenzi mmoja anakuwa Mkristo baada ya ndoa, mapambano asili ya kuishi chini ya mamlaka aina mbili tofauti huwa huwa dhahiri.
 
Mara nyingi Wakristo katika hali hii hutafuta njia ya kujinazua kutoka kwa ndoa, wakiamini kwamba hii ndio njia pekee ya kweli ambayo italeta utukufu kwa Mungu. Neno lake, hata hivyo, linasema kinyume chake. Ni muhimu sana kutoridhika na hali yetu pekee, bali pia kutafuta njia ya kuleta utukufu kwake mbali na changamoto zetu (1 Wakorintho 7:17). Biblia hasa inahusu wale ambao wameolewa na wasioamini katika 1 Wakorintho 7:12-14: "... iwapo ndugu mmoja ana mke asiyeamini, na mke huyo anakubali kukaa naye asiwmeache. Na mwanamke ambaye ana mume asiyeamini, na mume huyo anakubali kukaa naye, asimwache mumewe. Kwa maana Yule mume asiyeamini hutakaswa katika mkewe; na Yule mke asiyeamini hutakswa katika mumewe; kama asiengekuwa hivyo, watot wenu wengekuwa si safi..."
 
Wakristo ambao wameoleka kwa wasioamini wanahitaji kuomba kwa ajili ya nguvu za Roho Mtakatifu ili kuwawezesha kukiri Kristo na kuishi katika mwanga wa uwepo wa Mungu (1 Yohana 1:7). Wanapaswa kutafuta nguvu za Mungu za ubadilisho kubadili nyoyo zao na kuzaa matunda ya Roho Mtakatifu (Wagalatia 5:22-23). Mke Mkristo ana wajibu wa kuwa na moyo mtiifu, hata kwa mume wake ambaye si mkristo (1 Petro 3:01), na atahitaji kubaki karibu na Mungu na kutegemea neema yake kumwezesha kufanya hivyo.
 
Wakristo hawastahili kuishi maisha ya upweke wanahitaji kupata msaada kutoka kwingine kama vile kanisa na makundi ya kujifunza Biblia. Kuolewa na kafiri haina haibadilishi utakatifu wa uhusiano, hivyo ni lazima iwe kipaumbele cha kila Mkristo kuomba kwa ajili ya mke wake na kuweka mfano mzuri, kuruhusu mwanga wa Kristo kuangaza (Wafilipi 2:14). Bu na ukweli ulio katika 1 Petro 3:1-kwamba mwanandoa asiyeamini "amevutwa kwa Kristo"n iwe tumaini na lengo la kila Mkristo ambaye ameoleka kwa mtu asiye Mkristo.
Pesquisar
Categorias
Leia mais
EXODUS
Verse by verse explanation of Exodus 23
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 57 questions at the...
Por THE HOLY BIBLE 2022-01-22 18:06:43 0 5KB
SPIRITUAL EDUCATION
SPIRITUAL GIFTS AND IT'S PURPOSES
SPIRITUAL GIFTS AND IT'S PURPOSES 
Por Martin Laizer 2023-11-23 15:17:29 3 7KB
Injili Ya Yesu Kristo
UMEJIAANDAJE KWA TUKIO LA UNYAKUO? (Sehemu ya 2)
Katika sehemu hii ya pili nataka tuweze kuangalia jinsi baadhi ya maandiko yanavyozungumzia tukio...
Por GOSPEL PREACHER 2021-11-23 13:08:10 0 5KB
OTHERS
Je, Muhammad Ametabiriwa Kwenye Biblia?
SEHEMU YA KWANZA Waislamu wanashikilia kwamba Muhammad alitabiriwa kwenye Biblia. Andiko lao kuu...
Por MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-23 09:29:25 0 6KB
GENESIS
Verse by verse explanation of Genesis 15
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 26 questions at the...
Por THE HOLY BIBLE 2022-01-21 04:49:07 0 5KB