Je, Mkristo anapaswa kufanya nini kama yeye ameolewa na asiyeamini?

0
5K
Kuoleka na kafiri inaweza kuwa mojawapo ya changamoto ngumu sana katika maisha ya Mkristo. Ndoa ni agano takatifu ambalo linaunganisha watu wawili pamoja katika mwili mmoja (Mathayo 19:5). Inaweza kuwa vigumu sana kwa muumini na kafiri kuishi kwa amani na umoja (2 Wakorintho 6:14-15). Kama mpenzi mmoja anakuwa Mkristo baada ya ndoa, mapambano asili ya kuishi chini ya mamlaka aina mbili tofauti huwa huwa dhahiri.
 
Mara nyingi Wakristo katika hali hii hutafuta njia ya kujinazua kutoka kwa ndoa, wakiamini kwamba hii ndio njia pekee ya kweli ambayo italeta utukufu kwa Mungu. Neno lake, hata hivyo, linasema kinyume chake. Ni muhimu sana kutoridhika na hali yetu pekee, bali pia kutafuta njia ya kuleta utukufu kwake mbali na changamoto zetu (1 Wakorintho 7:17). Biblia hasa inahusu wale ambao wameolewa na wasioamini katika 1 Wakorintho 7:12-14: "... iwapo ndugu mmoja ana mke asiyeamini, na mke huyo anakubali kukaa naye asiwmeache. Na mwanamke ambaye ana mume asiyeamini, na mume huyo anakubali kukaa naye, asimwache mumewe. Kwa maana Yule mume asiyeamini hutakaswa katika mkewe; na Yule mke asiyeamini hutakswa katika mumewe; kama asiengekuwa hivyo, watot wenu wengekuwa si safi..."
 
Wakristo ambao wameoleka kwa wasioamini wanahitaji kuomba kwa ajili ya nguvu za Roho Mtakatifu ili kuwawezesha kukiri Kristo na kuishi katika mwanga wa uwepo wa Mungu (1 Yohana 1:7). Wanapaswa kutafuta nguvu za Mungu za ubadilisho kubadili nyoyo zao na kuzaa matunda ya Roho Mtakatifu (Wagalatia 5:22-23). Mke Mkristo ana wajibu wa kuwa na moyo mtiifu, hata kwa mume wake ambaye si mkristo (1 Petro 3:01), na atahitaji kubaki karibu na Mungu na kutegemea neema yake kumwezesha kufanya hivyo.
 
Wakristo hawastahili kuishi maisha ya upweke wanahitaji kupata msaada kutoka kwingine kama vile kanisa na makundi ya kujifunza Biblia. Kuolewa na kafiri haina haibadilishi utakatifu wa uhusiano, hivyo ni lazima iwe kipaumbele cha kila Mkristo kuomba kwa ajili ya mke wake na kuweka mfano mzuri, kuruhusu mwanga wa Kristo kuangaza (Wafilipi 2:14). Bu na ukweli ulio katika 1 Petro 3:1-kwamba mwanandoa asiyeamini "amevutwa kwa Kristo"n iwe tumaini na lengo la kila Mkristo ambaye ameoleka kwa mtu asiye Mkristo.
Search
Categories
Read More
OTHERS
How an Atheist Found God
A personal account from an atheist who was convinced no god exists, and what facts led to God....
By MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-23 09:43:58 0 6K
SPIRITUAL EDUCATION
NGUVU KATIKA UDHAIFU – MUNGU ANAVYOWATUMIA WADHAIFU KUWASHINDISHA WENYE NGUVU
SEHEMU YA 1: UTANGULIZI – KINZANI NA MANTIKI YA DUNIA Dunia inafundisha: “Nguvu...
By GOSPEL PREACHER 2026-05-26 13:24:39 0 3K
OTHERS
MWANAMKE WA KIISLAM HANA HAKI MBELE YA MUMEWE
Leo nitawapa hadith kadhaa kuhusu Wanawake wa Kiislam na jinsi wanavyo onewa na Mtume...
By MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-22 04:32:08 0 5K
Other
BOOK OF GENESIS
Book of Genesis Explained Genesis is the book of beginnings. It records the beginning of time,...
By PROSHABO NETWORK 2021-10-02 23:29:25 0 8K
JUDGES
Verse by verse explanation of Judges 3
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 36 questions at the...
By THE HOLY BIBLE 2022-01-25 10:45:16 0 5K