MWANAUME UKIKOSA UNYENYEKEVU MKE ATAKUSHINDA

3
6Кб

Unyenyekevu ni tabia ya kujishusha na kuvaa kiatu cha aliye chini yako; unavua heshima na utukufu wako, kisha unavaa hali yake aliye chini yako. Kwa mume aliye chini yake ni mkewe.

Yesu kama kichwa cha kanisa ni mfano wetu sisi waume tulio vichwa vya wake zetu katika swala zima la unyenyekevu. Yeye alijishusha akavaa kiatu chetu, na kuanzia hapo ndipo anaanza kutuleta pale alipo anapopenda na anapotaka tuwe sisi Kama mwili wake yaani kanisa lake.(Waefeso 5:22, 23, 25 - 29)

Kujiposea kanisa ambalo ni mwili wake, Yesu alijinyenyekesha kiasi cha kuyasalimu maisha yake. Aliacha utukufu na heshima yake akawa mtumwa kwa ajili ya mwili wake ambalo ndilo kanisa lake.(Wafilipi 2:5 - 8)

Mume, ukitaka mke wako akunyenyekee, basi jinyenyekeze kwanza wewe. Unyenyekevu si udhaifu ni nguvu na ujasiri wa kukabiliana na changamoto kwa yule unayempenda, lakini ni njia ya kuuteka moyo wake ili kumtiisha chini ya mapenzi yako.

Unyenyekevu wako unamleta mkeo chini ya mamlaka yako. Kama unataka ajitiishe chini ya mamlaka yako, wewe acha ubwanyenye, jishushe mpaka pale alipo, vaa hali na hadhi yake, mchukue mikononi mwako, kisha anza kupanda naye juu.

Yesu alijishusha, akawa mnyenyekevu hata mauti ya msalaba. Kwa kuwa sisi tulikuwa wenye dhambi, Yeye alifanyika dhambi ili atutakase, na kwa kuwa tulikuwa chini ya kifungo cha mauti alikufa mauti yetu kisha tukafufuka pamoja naye, tukapaa pamoja naye juu, na tukaketishwa pamoja naye mbinguni.

Mwanaume, wewe kama umeoa, njia nzuri ya kumfanya mkeo awe vile wewe upendavyo inaanza kwa wewe kumkubali na kumpenda vile alivyo yeye ambavyo wewe hupendi. Na huo ni unyenyekevu. Huwezi kufanya hivyo mpaka umevaa kiatu chake.

Yesu hakuwapenda watakatifu, aliupenda ulimwengu uliokuwa wenye dhambi. Hakupenda dhambi zao, alizichukia. Alimpenda mtu lakini alichukia dhambi, lakini ili amfanye vile apendavyo ilimbidi awe dhambi ya yule mtu, ajishushe kutoka katika hali ya mwenye haki mpaka hali ya mwenye dhambi ambayo alikuwa nayo huyu mlimwengu. Akafanyika dhambi ili kwa njia ya mauti amkomboe na kumfanya vile apendavyo.

Hii ni kanuni ya unyenyekevu ili kumleta mwenzi wako pale ulipo ktk hali uliyonayo. Kama hayupo vile upendavyo, vaa kiatu chake, kisha mbebe na kumchukulia udhaifu wake kwa upole wote.

Kumbuka, unyenyekevu ni tunda la Roho Mtakatifu. Hivyo ni lazima uonyeshwe katika hali ya utakatifu.

Поиск
Категории
Больше
1 SAMUEL
Verse by verse explanation of 1 Samuel 19
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 30 questions at the...
От THE HOLY BIBLE 2022-01-26 03:53:56 0 5Кб
PSALMS
Verse by verse explanation of Psalm 7
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 25 questions at the...
От THE HOLY BIBLE 2022-04-04 23:14:19 0 5Кб
2 KINGS
Verse by verse explanation of 2 Kings 24
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 28 questions at the...
От THE HOLY BIBLE 2022-03-19 21:11:47 0 6Кб
Injili Ya Yesu Kristo
Hekima yao ikapate kuwa ubatili na maarifa yao yawe ujinga!
2Samuel 15:30-31 “Daudi akapanda akishika njia ya kuupandia mlima wa Mizeituni, akilia...
От GOSPEL PREACHER 2022-04-01 09:26:31 4 7Кб
JUDGES
Verse by verse explanation of Judges 11
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 40 questions at the...
От THE HOLY BIBLE 2022-01-25 11:00:05 0 6Кб