MWANAUME UKIKOSA UNYENYEKEVU MKE ATAKUSHINDA

3
6KB

Unyenyekevu ni tabia ya kujishusha na kuvaa kiatu cha aliye chini yako; unavua heshima na utukufu wako, kisha unavaa hali yake aliye chini yako. Kwa mume aliye chini yake ni mkewe.

Yesu kama kichwa cha kanisa ni mfano wetu sisi waume tulio vichwa vya wake zetu katika swala zima la unyenyekevu. Yeye alijishusha akavaa kiatu chetu, na kuanzia hapo ndipo anaanza kutuleta pale alipo anapopenda na anapotaka tuwe sisi Kama mwili wake yaani kanisa lake.(Waefeso 5:22, 23, 25 - 29)

Kujiposea kanisa ambalo ni mwili wake, Yesu alijinyenyekesha kiasi cha kuyasalimu maisha yake. Aliacha utukufu na heshima yake akawa mtumwa kwa ajili ya mwili wake ambalo ndilo kanisa lake.(Wafilipi 2:5 - 8)

Mume, ukitaka mke wako akunyenyekee, basi jinyenyekeze kwanza wewe. Unyenyekevu si udhaifu ni nguvu na ujasiri wa kukabiliana na changamoto kwa yule unayempenda, lakini ni njia ya kuuteka moyo wake ili kumtiisha chini ya mapenzi yako.

Unyenyekevu wako unamleta mkeo chini ya mamlaka yako. Kama unataka ajitiishe chini ya mamlaka yako, wewe acha ubwanyenye, jishushe mpaka pale alipo, vaa hali na hadhi yake, mchukue mikononi mwako, kisha anza kupanda naye juu.

Yesu alijishusha, akawa mnyenyekevu hata mauti ya msalaba. Kwa kuwa sisi tulikuwa wenye dhambi, Yeye alifanyika dhambi ili atutakase, na kwa kuwa tulikuwa chini ya kifungo cha mauti alikufa mauti yetu kisha tukafufuka pamoja naye, tukapaa pamoja naye juu, na tukaketishwa pamoja naye mbinguni.

Mwanaume, wewe kama umeoa, njia nzuri ya kumfanya mkeo awe vile wewe upendavyo inaanza kwa wewe kumkubali na kumpenda vile alivyo yeye ambavyo wewe hupendi. Na huo ni unyenyekevu. Huwezi kufanya hivyo mpaka umevaa kiatu chake.

Yesu hakuwapenda watakatifu, aliupenda ulimwengu uliokuwa wenye dhambi. Hakupenda dhambi zao, alizichukia. Alimpenda mtu lakini alichukia dhambi, lakini ili amfanye vile apendavyo ilimbidi awe dhambi ya yule mtu, ajishushe kutoka katika hali ya mwenye haki mpaka hali ya mwenye dhambi ambayo alikuwa nayo huyu mlimwengu. Akafanyika dhambi ili kwa njia ya mauti amkomboe na kumfanya vile apendavyo.

Hii ni kanuni ya unyenyekevu ili kumleta mwenzi wako pale ulipo ktk hali uliyonayo. Kama hayupo vile upendavyo, vaa kiatu chake, kisha mbebe na kumchukulia udhaifu wake kwa upole wote.

Kumbuka, unyenyekevu ni tunda la Roho Mtakatifu. Hivyo ni lazima uonyeshwe katika hali ya utakatifu.

Rechercher
Catégories
Lire la suite
NUMBERS
Verse by verse explanation of Numbers 26
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 55 questions at the...
Par THE HOLY BIBLE 2022-01-24 15:16:54 0 6KB
Injili Ya Yesu Kristo
Je, Yesu anawezaje kuwa Mungu na mwanadamu kwa wakati mmoja?
Ni nini maana ya muungano wa kimwili na Uungu?Hili ni swali linalo ulizwa mara nyingi sana, ni...
Par MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-22 21:14:28 0 5KB
LEVITICUS
Verse by verse explanation of Leviticus 12
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 30 questions at the...
Par THE HOLY BIBLE 2022-01-24 10:05:53 0 5KB
DEUTERONOMY
Verse by verse explanation of Deuteronomy 10
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 28 questions at the...
Par THE HOLY BIBLE 2022-01-25 06:00:10 0 5KB
DEUTERONOMY
Verse by verse explanation of Deuteronomy 19
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 22 questions at the...
Par THE HOLY BIBLE 2022-01-25 06:16:50 0 5KB