MWANAUME UKIKOSA UNYENYEKEVU MKE ATAKUSHINDA

3
6K

Unyenyekevu ni tabia ya kujishusha na kuvaa kiatu cha aliye chini yako; unavua heshima na utukufu wako, kisha unavaa hali yake aliye chini yako. Kwa mume aliye chini yake ni mkewe.

Yesu kama kichwa cha kanisa ni mfano wetu sisi waume tulio vichwa vya wake zetu katika swala zima la unyenyekevu. Yeye alijishusha akavaa kiatu chetu, na kuanzia hapo ndipo anaanza kutuleta pale alipo anapopenda na anapotaka tuwe sisi Kama mwili wake yaani kanisa lake.(Waefeso 5:22, 23, 25 - 29)

Kujiposea kanisa ambalo ni mwili wake, Yesu alijinyenyekesha kiasi cha kuyasalimu maisha yake. Aliacha utukufu na heshima yake akawa mtumwa kwa ajili ya mwili wake ambalo ndilo kanisa lake.(Wafilipi 2:5 - 8)

Mume, ukitaka mke wako akunyenyekee, basi jinyenyekeze kwanza wewe. Unyenyekevu si udhaifu ni nguvu na ujasiri wa kukabiliana na changamoto kwa yule unayempenda, lakini ni njia ya kuuteka moyo wake ili kumtiisha chini ya mapenzi yako.

Unyenyekevu wako unamleta mkeo chini ya mamlaka yako. Kama unataka ajitiishe chini ya mamlaka yako, wewe acha ubwanyenye, jishushe mpaka pale alipo, vaa hali na hadhi yake, mchukue mikononi mwako, kisha anza kupanda naye juu.

Yesu alijishusha, akawa mnyenyekevu hata mauti ya msalaba. Kwa kuwa sisi tulikuwa wenye dhambi, Yeye alifanyika dhambi ili atutakase, na kwa kuwa tulikuwa chini ya kifungo cha mauti alikufa mauti yetu kisha tukafufuka pamoja naye, tukapaa pamoja naye juu, na tukaketishwa pamoja naye mbinguni.

Mwanaume, wewe kama umeoa, njia nzuri ya kumfanya mkeo awe vile wewe upendavyo inaanza kwa wewe kumkubali na kumpenda vile alivyo yeye ambavyo wewe hupendi. Na huo ni unyenyekevu. Huwezi kufanya hivyo mpaka umevaa kiatu chake.

Yesu hakuwapenda watakatifu, aliupenda ulimwengu uliokuwa wenye dhambi. Hakupenda dhambi zao, alizichukia. Alimpenda mtu lakini alichukia dhambi, lakini ili amfanye vile apendavyo ilimbidi awe dhambi ya yule mtu, ajishushe kutoka katika hali ya mwenye haki mpaka hali ya mwenye dhambi ambayo alikuwa nayo huyu mlimwengu. Akafanyika dhambi ili kwa njia ya mauti amkomboe na kumfanya vile apendavyo.

Hii ni kanuni ya unyenyekevu ili kumleta mwenzi wako pale ulipo ktk hali uliyonayo. Kama hayupo vile upendavyo, vaa kiatu chake, kisha mbebe na kumchukulia udhaifu wake kwa upole wote.

Kumbuka, unyenyekevu ni tunda la Roho Mtakatifu. Hivyo ni lazima uonyeshwe katika hali ya utakatifu.

Zoeken
Categorieën
Read More
OTHERS
UTATA KATIKA UUMBAJI WA MAJINI
ALLAH: UTATA KATIKA UUMBAJI WA MAJINIJe, Majini yaliumbwaje?Leo hii tutajifunza UTATA wa Allah...
By MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-23 08:20:08 0 5K
OTHERS
MIJADALA YA DINI NI MUHIMU.
Watu wengi katika jamii yetu wanasema kuwa tusiendekeze mijadala ya dini. Wanasema kuwa ni tishio...
By MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-24 22:14:33 0 5K
Injili Ya Yesu Kristo
Yesu ni Mungu
Je, Yesu Kristo ni Mungu?Hebu tuanzie kutafiti ukweli wa hili swali, Je Yesu ni Mungu, kabla ya...
By MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-23 10:42:49 0 5K
JOB
Verse by verse explanation of Job 40
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 21 questions at the...
By THE HOLY BIBLE 2022-04-03 04:23:40 0 6K
CHEKECHEA
CHEKECHEA 2
Orodha ya masomo ya chekechea  kwa darasa la wakubwa
By PROSHABO ONLINE SCHOOLS 2021-10-09 10:08:03 0 5K