JE! SISI NI WAFALME NA MAKUHANI KWA NAMNA GANI?

5
3χλμ.

*Je! sisi ni wafalme na makuhani kwa namna gani?*

 

Na: Martin Laizer

 

SWALI: Yohana hapa anasema Bwana ametufanya kuwa Ufalme na Makuhani Ufunuo1:6 …(Sasa hapa anamaanisha sasa hivi sisi ni wafalme na makuhani au ni katika ule umilele ujao?) na je! ni sahihi kumuita mwanamke kuhani??

 

JIBU: Ndio sasahivi sisi ni ufalme na makuhani wa Bwana katika roho,..kama vile Bwana Yesu alivyokuwa duniani tangu siku za kuzaliwa kwake mpaka siku za kuondoka kwake,,…tayari yeye alishakuwa mfalme,..Kama unakumbuka wale Mamajusi walimuuliza Herode yuko wapi mfalme wa wayahudi tunataka kumsujudia (Mathayo 2:3)? unaona hapo tangu alipokuwa mdogo tayari ni mfalme, pia Pilato tunaona baadaye siku chache kabla ya kuondoka kwake duniani alikuja kumuuliza Bwana …

 

Yohana 18: 33 “Basi Pilato akaingia tena ndani ya Praitorio, akamwita Yesu, akamwambia, Je! Wewe ni Mfalme wa Wayahudi?

 

34 Yesu akamjibu, Wewe wasema hivi kwa nafsi yako, au watu wengine walikuambia habari zangu?

 

35 Pilato akajibu, Ama! Ni Myahudi mimi! Taifa lako na wakuu wa makuhani ndio waliokuleta kwangu. Umefanya nini?

 

36 Yesu akajibu, Ufalme wangu sio wa ulimwengu huu. Kama ufalme wangu ungekuwa wa ulimwengu huu, watumishi wangu wangenipigania, nisije nikatiwa mikononi mwa Wayahudi. Lakini ufalme wangu sio wa hapa.

 

37 Basi Pilato akamwambia, Wewe u mfalme basi? Yesu akajibu, Wewe wasema, kwa kuwa mimi ni mfalme. Mimi nimezaliwa kwa ajili ya haya, na kwa ajili ya haya mimi nalikuja ulimwenguni, ili niishuhudie kweli. Kila aliye wa hiyo kweli hunisikia sauti yangu”.

 

Kwahiyo hata sisi tuliookolewa, na kuoshwa kwa damu ya Bwana wetu Yesu Kristo, ni makuhani na ufalme. Lakini mambo hayo yatakuja kudhihirika katika ulimwengu unaokuja kama Bwana alivyosema ufalme wake ni wa ulimwengu unaokuja!…Na ukuhani wenyewe hautakuwa wa kuvukiza uvumba tena, ule ulikuwa ni taswira ya mambo yatakayokuja yanayofunua kumkaribia Mungu.. 

 

Vivyo hivyo na katika huo ulimwengu unaokuja hatutakuwa tu wafalme bali tutakuwa na uwezo kumkaribia Mungu kwa namna ya kipekee mfano wa makuhani, ambao sio watu wote watapewa uwezo huo bali ni wale watakaoshinda tu!.. Na thawabu hiyo itakuwa ni kwa wote…wanawake na wanaume.

 

Hivyo ukuhani wako mbele za Mungu unautengeneza ukiwa hapa hapa duniani, kwahiyo tunapaswa tukaze mwendo ili tusikose thawabu hizo.

 

Ubarikiwe sana.

Αναζήτηση
Κατηγορίες
Διαβάζω περισσότερα
SPIRITUAL EDUCATION
HAIRISHA MAZISHI YAO! (Kufufuka kwa Mwana wa Mjane wa Naini – Luka 7:11-17)
  SEHEMU YA KWANZA: UTANGULIZI – MKUTANO KATIKA NJIA Somo la msingi: Luka...
από GOSPEL PREACHER 2026-05-24 05:56:04 0 3χλμ.
DEUTERONOMY
Verse by verse explanation of Deuteronomy 30
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 19 questions at the...
από THE HOLY BIBLE 2022-01-25 07:02:11 0 6χλμ.
Injili Ya Yesu Kristo
UKWELI KUHUSU HAKI IPATIKANAYO KWA IMANI
BWANA YESU ASIFIWE!! Mpendwa Roho Mtakatifu ameweka Nyakati hizi tunazoishi ni nyakati/siku za...
από PROSPER HABONA 2022-01-16 14:17:28 0 5χλμ.
PSALMS
Verse by verse explanation of Psalm 4
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 38 questions at the...
από THE HOLY BIBLE 2022-04-04 22:58:57 0 5χλμ.
Religion
EPUKA KUPELELEZA KILA KITU MUNGU ANACHOKUAHIDIA.
EPUKA KUPELELEZA KILA KITU MUNGU ANACHOKUAHIDIA. Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe,...
από WINGU LA MASHAHIDI 2021-09-18 21:46:03 0 8χλμ.