JE! SISI NI WAFALME NA MAKUHANI KWA NAMNA GANI?

5
3χλμ.

*Je! sisi ni wafalme na makuhani kwa namna gani?*

 

Na: Martin Laizer

 

SWALI: Yohana hapa anasema Bwana ametufanya kuwa Ufalme na Makuhani Ufunuo1:6 …(Sasa hapa anamaanisha sasa hivi sisi ni wafalme na makuhani au ni katika ule umilele ujao?) na je! ni sahihi kumuita mwanamke kuhani??

 

JIBU: Ndio sasahivi sisi ni ufalme na makuhani wa Bwana katika roho,..kama vile Bwana Yesu alivyokuwa duniani tangu siku za kuzaliwa kwake mpaka siku za kuondoka kwake,,…tayari yeye alishakuwa mfalme,..Kama unakumbuka wale Mamajusi walimuuliza Herode yuko wapi mfalme wa wayahudi tunataka kumsujudia (Mathayo 2:3)? unaona hapo tangu alipokuwa mdogo tayari ni mfalme, pia Pilato tunaona baadaye siku chache kabla ya kuondoka kwake duniani alikuja kumuuliza Bwana …

 

Yohana 18: 33 “Basi Pilato akaingia tena ndani ya Praitorio, akamwita Yesu, akamwambia, Je! Wewe ni Mfalme wa Wayahudi?

 

34 Yesu akamjibu, Wewe wasema hivi kwa nafsi yako, au watu wengine walikuambia habari zangu?

 

35 Pilato akajibu, Ama! Ni Myahudi mimi! Taifa lako na wakuu wa makuhani ndio waliokuleta kwangu. Umefanya nini?

 

36 Yesu akajibu, Ufalme wangu sio wa ulimwengu huu. Kama ufalme wangu ungekuwa wa ulimwengu huu, watumishi wangu wangenipigania, nisije nikatiwa mikononi mwa Wayahudi. Lakini ufalme wangu sio wa hapa.

 

37 Basi Pilato akamwambia, Wewe u mfalme basi? Yesu akajibu, Wewe wasema, kwa kuwa mimi ni mfalme. Mimi nimezaliwa kwa ajili ya haya, na kwa ajili ya haya mimi nalikuja ulimwenguni, ili niishuhudie kweli. Kila aliye wa hiyo kweli hunisikia sauti yangu”.

 

Kwahiyo hata sisi tuliookolewa, na kuoshwa kwa damu ya Bwana wetu Yesu Kristo, ni makuhani na ufalme. Lakini mambo hayo yatakuja kudhihirika katika ulimwengu unaokuja kama Bwana alivyosema ufalme wake ni wa ulimwengu unaokuja!…Na ukuhani wenyewe hautakuwa wa kuvukiza uvumba tena, ule ulikuwa ni taswira ya mambo yatakayokuja yanayofunua kumkaribia Mungu.. 

 

Vivyo hivyo na katika huo ulimwengu unaokuja hatutakuwa tu wafalme bali tutakuwa na uwezo kumkaribia Mungu kwa namna ya kipekee mfano wa makuhani, ambao sio watu wote watapewa uwezo huo bali ni wale watakaoshinda tu!.. Na thawabu hiyo itakuwa ni kwa wote…wanawake na wanaume.

 

Hivyo ukuhani wako mbele za Mungu unautengeneza ukiwa hapa hapa duniani, kwahiyo tunapaswa tukaze mwendo ili tusikose thawabu hizo.

 

Ubarikiwe sana.

Αναζήτηση
Κατηγορίες
Διαβάζω περισσότερα
Injili Ya Yesu Kristo
MFANO WA MPANZI NA MBEGU
  LUKA 5;8-5 "Mpanzi alitoka kwenda kupanda mbegu zake; naye alipokuwa akizipanda, nyingine...
από GOSPEL PREACHER 2022-01-15 22:24:38 0 6χλμ.
Injili Ya Yesu Kristo
YESU NDIE NJIA NA KWELI NA UZIMA. Kumbe Dini sio Njia
Katika Biblia tunasoma kuwa Yesu anasema yeye ndie "KWELI" na anaendelea kusema kuwa KWELI ndiyo...
από MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-23 08:34:15 0 6χλμ.
Injili Ya Yesu Kristo
Je, Yesu anawezaje kuwa Mungu na mwanadamu kwa wakati mmoja?
Ni nini maana ya muungano wa kimwili na Uungu?Hili ni swali linalo ulizwa mara nyingi sana, ni...
από MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-22 21:14:28 0 5χλμ.
OTHERS
ABOUT BISHOP ZACHARY KAKOBE ( HISTORY)
Bishop Zachary Kakobe is the International Revivalist, and Founder of Bishop Zachary Kakobe...
από GOSPEL PREACHER 2022-01-12 00:53:13 0 11χλμ.
Injili Ya Yesu Kristo
YESU KRISTO NI MUNGU: THIBITISHO SABA
UFUNUO WA YOHANA 1:1-7 Kitabu hiki kinaelezea jinsi itakavyokua baadaye kwa watendao maovu...
από MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-22 05:25:58 0 5χλμ.