KUPENDANA HUSITIRI DHAMBI

0
6χλμ.
Ndugu zangu,
Nawasalimu katika jina la Yesu. Mungu mwema kwa neema zake leo tena tumepata neema ya kumtumikia. 
Napenda tumtafakari Mungu kwa maneno haya machache. Mtume Petro anasema "Zaidi ya yote iweni na juhudi nyingi katika kupendana; kwa sababu upendano husitiri wingi wa dhambi" - 1 Petro 4:8
 
Kuna msemo wa kiswahili wanasema 'kupenda ni upofu'! Wanasema unapompenda mtu hata zile kasoro ambazo wengine wanaziona kwa huyo umpendae basi wewe huzioni. Sababu ni moja tu, Upendo husitiri dhambi wana wa Mungu.  Na mtume Petro anatukumbusha tuwe na bidii katika kupendana. Ndugu zangu tukiwa na bidii katika kupendana ndani ya jamii zetu, ndani ya madhehebu yetu, ndani ya ofisi zetu, ndani ya maeneo yetu tunayofanyia kazi, ndani ya mashambani mwetu, nakuambia katika jina la Yesu hutaona tofauti unazoziona kwa jirani yako au ndugu yako kama unavyoziona sasa. Lakini kwa sababu tu hatujatia bidii katika kupendana ndo maana tunaona hivi vitofauti vidogo vidogo hadi vinaibukia kututenganisha na kutufarakanisha.
 
Mwandishi wa Mithali 10:12 anasema "Kuchukiana huondokesha fitina; Bali kupendana husitiri makosa yote"!.  Ndani ya ndoa zetu kumbe tukipendana viji-ugomvi visivyo na kichwa wala miguu hatutaviona wapendwa wana wa Mungu kwa sababu kuchukiana ndiko kunakoleta fitina. Tena "Upendo huvumilia" - 1Kor 13:4 ndio maana unakuwa kipofu kwa udhaifu kwa mwenzio.
 
Ndugu yangu ni ombi langu siku ya leo Roho Mtakatifu akusaidie uwe na bidii katika kupendana. Kwa maana kupendana kunasitiri dhambi mtumishi wa Mungu nakuambia. Inawezekana ndugu yako au jamaa yako au rafiki yako amekukosea au amekuwa akikukosea mara kwa mara ndo maana hutaki tena kumpenda. Lakini laiti Mungu angehesabu makosa yetu nadhani dunia hii tungekuwa tunapukutika kila siku. Basi nakuombea Roho Mtakatifu arudishe upendo wako wa kwanza na sasa uendelee mbele katika kupendana na jirani yako, na ndugu yako na rafiki yako. Mwambie Roho wa Mungu akusidie kupendana. Kwa nguvu zetu hatuwezi. Hebu omba neema ya Mungu katika hili.
 
Mungu akubariki sana.
Like
1
Αναζήτηση
Κατηγορίες
Διαβάζω περισσότερα
EXODUS
Verse by verse explanation of Exodus 13
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 39 questions at the...
από THE HOLY BIBLE 2022-01-22 11:37:34 0 4χλμ.
OTHERS
ETI ALLAH AMEKUBALI KUTOA USHAIDI KWA VIUMBE VYAKE?
Je, nani atakuwa Hakimu wakati Allah anatoa Ushaidi?NDUGU WASOMAJI, Hivi Allah anaweza kuwa...
από MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-22 02:24:46 0 5χλμ.
1 CHRONICLES
Verse by verse explanation of 1 Chronicles 9
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 30 questions at the...
από THE HOLY BIBLE 2022-03-20 04:47:53 0 5χλμ.
OTHERS
When was the Bible written and who wrote it?
The following dates are not always exact, but are very good estimates. Old Testament Book...
από MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-23 08:45:37 0 5χλμ.
REVELATION
UFUNUO 12
MAELEZO JUU YA “UFUNUO 12” Ufunuo 12 1 Na ishara kuu ilionekana mbinguni;...
από GOSPEL PREACHER 2021-10-30 11:35:41 0 5χλμ.