MKE WA KAINI KATOKEA WAPI?

0
5كيلو بايت

Bwana Yesu asifiwe…

Kwa ufupi;

Ukisoma kitabu cha Mwanzo sura 1-4,utaona Mungu akiwa na Adamu na Hawa kama watu wa kwanza kuumbwa na waliokuwepo. Lakini ukiendelea kusoma sura ya 4 baada ya Kaini alipomwua ndugu yake Habili ,utaona Kaini akifukuzwa naye akaenda kuishi kwenye nchi ya Nodi,huko akakutana na mwanamke kisha akamuoa (Mwanzo 4:16-18). Sasa swali linakuja hivi;Huyo mwanamke katokea wapi? Je kulikuwa na watu wengine kabla ya Adamu na Hawa? Umeelewa swali lakini?

Hili ni moja ya maswali yanayoulizwa sana,lakini ebu tujaribu kutafakari hili,na kujaribu kuweka majibu. Sasa,ikumbukwe ya kwamba Biblia tunayoitumia imetokana na taratibu/ustaharabu wa Kiyahudi ambao mwanamke hakuhesabika hasa kwenye jamii,ndio maana unaweza ukaliona hili kwa Dina mtoto wa Yakobo ambaye hatajwi kama kabila la Israeli,bali ndugu zake wale kumi na mbili ndio wanaotajwa (Mwanzo 35:22-26),Au unaweza kuona jambo hili pale Yesu alipowalisha watu elfu tano,wanawake wala watoto hawakuhesabiwa (Mathayo 14:20-21). Hivyo ilikuwa ni desturi ya kutokumwesabu mwanamke na watoto pia.

Kwa desturi hiyo hiyo,watoto wa Adamu wa kike hawakupewa nafasi ya kuhesabika kwa maana Adamu alikuwa na watoto wengine baada ya Kaini na Habili. Hivyo Kaini alimwoa dada yake,maana Adamu aliendelea kuwa na watoto wa kike na wakiume (Mwanzo 5:4). Biblia haikutupa kujua muda ambao Kaini aliishi katika nchi ya Nodi,tunachoelezwa ni kwamba Kaini akakaa katika nchi ya Nodi na akaoa huko. Hivyo inawezekana kuna muda fulani alioutumia Kaini kabla ya kuoa alipokuwa huko Nodi. Kaini alimwoa mmoja wa dada yake kama desturi ya zamani. Kwa maana hata Ibrahimu alimwoa Sara aliyekuwa ni dada yake wa mama mwingine ila baba yao alikuwa mmoja mzee Tera (Mwanzo 20:12)

البحث
الأقسام
إقرأ المزيد
NUMBERS
Verse by verse explanation of Numbers 2
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 31 questions at the...
بواسطة THE HOLY BIBLE 2022-01-24 14:09:28 0 5كيلو بايت
Religion
Jinsi Shetani Anavyopofusha Fikra za Watu: Maandiko ya Biblia Yanayofafanua
Katika Biblia, Shetani anaelezewa kama roho mbaya ambaye anaweza kushawishi, kudanganya, na...
بواسطة GOSPEL PREACHER 2025-09-28 05:02:20 0 2كيلو بايت
Injili Ya Yesu Kristo
Jinsi ya kuzidi kuwa Hodari.
Utangulizi: Tunasoma Katika maandiko ya kwamba watu wengi wanaotajwa kama mashujaa wa Imani...
بواسطة GOSPEL PREACHER 2022-03-31 14:49:05 0 7كيلو بايت
Injili Ya Yesu Kristo
Prayer for Peace and Justice in Tanzania
Our Omnipotent God, in whom the whole Adamic family of earth is one, breathe your Spirit of...
بواسطة MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-23 09:57:52 0 5كيلو بايت
Injili Ya Yesu Kristo
URAIA WA MBINGUNI.
Bwana Yesu asifiwe… Kwa ufupi; Ni vyema tukajifunza kuhusu uraia lakini uraia wa mbinguni...
بواسطة GOSPEL PREACHER 2022-03-30 04:50:47 0 5كيلو بايت