MKE WA KAINI KATOKEA WAPI?

0
5KB

Bwana Yesu asifiwe…

Kwa ufupi;

Ukisoma kitabu cha Mwanzo sura 1-4,utaona Mungu akiwa na Adamu na Hawa kama watu wa kwanza kuumbwa na waliokuwepo. Lakini ukiendelea kusoma sura ya 4 baada ya Kaini alipomwua ndugu yake Habili ,utaona Kaini akifukuzwa naye akaenda kuishi kwenye nchi ya Nodi,huko akakutana na mwanamke kisha akamuoa (Mwanzo 4:16-18). Sasa swali linakuja hivi;Huyo mwanamke katokea wapi? Je kulikuwa na watu wengine kabla ya Adamu na Hawa? Umeelewa swali lakini?

Hili ni moja ya maswali yanayoulizwa sana,lakini ebu tujaribu kutafakari hili,na kujaribu kuweka majibu. Sasa,ikumbukwe ya kwamba Biblia tunayoitumia imetokana na taratibu/ustaharabu wa Kiyahudi ambao mwanamke hakuhesabika hasa kwenye jamii,ndio maana unaweza ukaliona hili kwa Dina mtoto wa Yakobo ambaye hatajwi kama kabila la Israeli,bali ndugu zake wale kumi na mbili ndio wanaotajwa (Mwanzo 35:22-26),Au unaweza kuona jambo hili pale Yesu alipowalisha watu elfu tano,wanawake wala watoto hawakuhesabiwa (Mathayo 14:20-21). Hivyo ilikuwa ni desturi ya kutokumwesabu mwanamke na watoto pia.

Kwa desturi hiyo hiyo,watoto wa Adamu wa kike hawakupewa nafasi ya kuhesabika kwa maana Adamu alikuwa na watoto wengine baada ya Kaini na Habili. Hivyo Kaini alimwoa dada yake,maana Adamu aliendelea kuwa na watoto wa kike na wakiume (Mwanzo 5:4). Biblia haikutupa kujua muda ambao Kaini aliishi katika nchi ya Nodi,tunachoelezwa ni kwamba Kaini akakaa katika nchi ya Nodi na akaoa huko. Hivyo inawezekana kuna muda fulani alioutumia Kaini kabla ya kuoa alipokuwa huko Nodi. Kaini alimwoa mmoja wa dada yake kama desturi ya zamani. Kwa maana hata Ibrahimu alimwoa Sara aliyekuwa ni dada yake wa mama mwingine ila baba yao alikuwa mmoja mzee Tera (Mwanzo 20:12)

Rechercher
Catégories
Lire la suite
Injili Ya Yesu Kristo
BIBLIA INAWEZA KUAMINIWA NA KUTEGEMEWA
Kimsingi mwanadamu anaweza kumfikiria Mungu kwa njia kuu mbili: Njia ya kwanza ni ile ya...
Par MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-22 04:11:59 0 5KB
MASWALI & MAJIBU
Bwana Aliposema Kuwa Yeye Ni “Mungu Wa Miungu” Alikuwa Na Maana Gani?..Je! Yeye Ni Mungu Wa Sanamu?
JIBU: Tukisoma Kumbukumbu 10:17 inasema… “Kwa maana Bwana, Mungu wenu, yeye ndiye...
Par GOSPEL PREACHER 2022-06-13 08:14:03 0 6KB
UCHUMBA KIBIBLIA
MAMBO YA KUFANYA/KUZINGATIA KATIKA KIPINDI CHA UCHUMBA
Mpenzi msomaji tunakusalimu kwa jina la Yesu! Baada ya kuwa tumepata maombi ya vijana wengi...
Par GOSPEL PREACHER 2021-11-23 07:25:47 0 6KB
Injili Ya Yesu Kristo
Je, Yesu anawezaje kuwa Mungu na mwanadamu kwa wakati mmoja?
Ni nini maana ya muungano wa kimwili na Uungu?Hili ni swali linalo ulizwa mara nyingi sana, ni...
Par MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-22 21:14:28 0 5KB
DEUTERONOMY
Verse by verse explanation of Deuteronomy 17
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 30 questions at the...
Par THE HOLY BIBLE 2022-01-25 06:11:57 0 5KB