MKE WA KAINI KATOKEA WAPI?

0
5KB

Bwana Yesu asifiwe…

Kwa ufupi;

Ukisoma kitabu cha Mwanzo sura 1-4,utaona Mungu akiwa na Adamu na Hawa kama watu wa kwanza kuumbwa na waliokuwepo. Lakini ukiendelea kusoma sura ya 4 baada ya Kaini alipomwua ndugu yake Habili ,utaona Kaini akifukuzwa naye akaenda kuishi kwenye nchi ya Nodi,huko akakutana na mwanamke kisha akamuoa (Mwanzo 4:16-18). Sasa swali linakuja hivi;Huyo mwanamke katokea wapi? Je kulikuwa na watu wengine kabla ya Adamu na Hawa? Umeelewa swali lakini?

Hili ni moja ya maswali yanayoulizwa sana,lakini ebu tujaribu kutafakari hili,na kujaribu kuweka majibu. Sasa,ikumbukwe ya kwamba Biblia tunayoitumia imetokana na taratibu/ustaharabu wa Kiyahudi ambao mwanamke hakuhesabika hasa kwenye jamii,ndio maana unaweza ukaliona hili kwa Dina mtoto wa Yakobo ambaye hatajwi kama kabila la Israeli,bali ndugu zake wale kumi na mbili ndio wanaotajwa (Mwanzo 35:22-26),Au unaweza kuona jambo hili pale Yesu alipowalisha watu elfu tano,wanawake wala watoto hawakuhesabiwa (Mathayo 14:20-21). Hivyo ilikuwa ni desturi ya kutokumwesabu mwanamke na watoto pia.

Kwa desturi hiyo hiyo,watoto wa Adamu wa kike hawakupewa nafasi ya kuhesabika kwa maana Adamu alikuwa na watoto wengine baada ya Kaini na Habili. Hivyo Kaini alimwoa dada yake,maana Adamu aliendelea kuwa na watoto wa kike na wakiume (Mwanzo 5:4). Biblia haikutupa kujua muda ambao Kaini aliishi katika nchi ya Nodi,tunachoelezwa ni kwamba Kaini akakaa katika nchi ya Nodi na akaoa huko. Hivyo inawezekana kuna muda fulani alioutumia Kaini kabla ya kuoa alipokuwa huko Nodi. Kaini alimwoa mmoja wa dada yake kama desturi ya zamani. Kwa maana hata Ibrahimu alimwoa Sara aliyekuwa ni dada yake wa mama mwingine ila baba yao alikuwa mmoja mzee Tera (Mwanzo 20:12)

Rechercher
Catégories
Lire la suite
BIBLICAL FINANCIAL EDUCATION
What is a Tithe?
What does the Bible say about tithing Tithing is the practice of setting aside 10% of your...
Par BIBLICAL FINANCES 2021-12-29 14:51:07 0 7KB
Injili Ya Yesu Kristo
Prayer for Peace and Justice in Tanzania
Our Omnipotent God, in whom the whole Adamic family of earth is one, breathe your Spirit of...
Par MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-23 09:57:52 0 5KB
OTHERS
EVOLUTION IS SATANISM!! Abortion Holocaust
If I were you I would BLOW UP MYSELF!Your existence is totally POINTLESS.This was my way of...
Par MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-24 22:32:07 0 5KB
SPIRITUAL EDUCATION
Was Jesus Rich
JESUS WAS GIVEN GIFTS AS A CHILD AGED APPROXIMATELY 2 YEARS OLDJesus was given gifts of gold,...
Par MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-22 02:52:44 0 5KB
Injili Ya Yesu Kristo
NAMNA YA KUMTUMIA ROHO MTAKATIFU KAMA MSAIDIZI KUPITIA KAZI ZAKE
Yohana 14:16-18 … Nami nitamwomba Baba, naye atawapa Msaidizi mwingine, ili akae...
Par GOSPEL PREACHER 2021-11-23 12:56:52 0 5KB