MKE WA KAINI KATOKEA WAPI?

0
5KB

Bwana Yesu asifiwe…

Kwa ufupi;

Ukisoma kitabu cha Mwanzo sura 1-4,utaona Mungu akiwa na Adamu na Hawa kama watu wa kwanza kuumbwa na waliokuwepo. Lakini ukiendelea kusoma sura ya 4 baada ya Kaini alipomwua ndugu yake Habili ,utaona Kaini akifukuzwa naye akaenda kuishi kwenye nchi ya Nodi,huko akakutana na mwanamke kisha akamuoa (Mwanzo 4:16-18). Sasa swali linakuja hivi;Huyo mwanamke katokea wapi? Je kulikuwa na watu wengine kabla ya Adamu na Hawa? Umeelewa swali lakini?

Hili ni moja ya maswali yanayoulizwa sana,lakini ebu tujaribu kutafakari hili,na kujaribu kuweka majibu. Sasa,ikumbukwe ya kwamba Biblia tunayoitumia imetokana na taratibu/ustaharabu wa Kiyahudi ambao mwanamke hakuhesabika hasa kwenye jamii,ndio maana unaweza ukaliona hili kwa Dina mtoto wa Yakobo ambaye hatajwi kama kabila la Israeli,bali ndugu zake wale kumi na mbili ndio wanaotajwa (Mwanzo 35:22-26),Au unaweza kuona jambo hili pale Yesu alipowalisha watu elfu tano,wanawake wala watoto hawakuhesabiwa (Mathayo 14:20-21). Hivyo ilikuwa ni desturi ya kutokumwesabu mwanamke na watoto pia.

Kwa desturi hiyo hiyo,watoto wa Adamu wa kike hawakupewa nafasi ya kuhesabika kwa maana Adamu alikuwa na watoto wengine baada ya Kaini na Habili. Hivyo Kaini alimwoa dada yake,maana Adamu aliendelea kuwa na watoto wa kike na wakiume (Mwanzo 5:4). Biblia haikutupa kujua muda ambao Kaini aliishi katika nchi ya Nodi,tunachoelezwa ni kwamba Kaini akakaa katika nchi ya Nodi na akaoa huko. Hivyo inawezekana kuna muda fulani alioutumia Kaini kabla ya kuoa alipokuwa huko Nodi. Kaini alimwoa mmoja wa dada yake kama desturi ya zamani. Kwa maana hata Ibrahimu alimwoa Sara aliyekuwa ni dada yake wa mama mwingine ila baba yao alikuwa mmoja mzee Tera (Mwanzo 20:12)

Rechercher
Catégories
Lire la suite
SPIRITUAL EDUCATION
If Jesus is God, then who did He pray to?
This is a very common question and the answer is found in understanding...
Par MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-24 06:03:16 0 6KB
OTHERS
KAMA YESU NI MUNGU, KWANINI ALIKUFA?
JE, MUNGU ANAKUFA? Hayo ni maswali ya Waislam kila siku, na kwenye hii mada nitayajibu. SOMA: 1...
Par MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-25 11:50:46 0 6KB
Networking
11 marketplace metrics you should be tracking to measure your success
Which marketplace metrics should you really track to know your marketplace is successful? One...
Par Business Academy 2022-09-17 04:01:13 0 12KB
NUMBERS
Verse by verse explanation of Numbers 1
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 62 questions at the...
Par THE HOLY BIBLE 2022-01-24 14:02:27 0 5KB
2 KINGS
Verse by verse explanation of 2 Kings 17
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 24 questions at the...
Par THE HOLY BIBLE 2022-03-19 20:39:06 0 6KB