UNYENYEKEVU.

0
5KB

Bwana Yesu asifiwe...

Kwa ufupi.

” Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu; “ Mathayo 11:29

“unyenyekevu”hali ya kushuka,kukubali kuonekana mdogo/mtumishi wa wote,kukubali lawama na kuvumilia. Si jambo jepesi kukubali kuwa chini hali wewe una vitu vingi. Si rahisi hata kidogo kukubali lawama. Wengi wanapenda wawe wanyenyekevu lakini hawapo tayari kushuka,kupokea lawama,kuvumilia n.k. Unyenyekevu ni ghalama mpendwa!

  • Unyenyekevu ni tabia ya Yesu. Yesu alikuwa ni mnyenyekevu wa moyo

Yesu alikuwa mnyenyekevu wa moyo,sio wa kuigiza. Alikuli mateso yote ingawa alikuwa na uwezo wa kuyakataa,lakini kwa kusudi la kutufundisha ilimbidi akubali na kwa lile kusudi la ukombozi,alikubali yote. Fikiri pale alipopelekwa mbele wa waashi na wakuu wa makuhani kisha wakamsomea mashtaka ya uongo,lakini alikaa kimya asitie neno lolote hali akijua yote yanayoendelea. Hakika mtu huyu alikuwa ni mnyenyekevu wa moyo. Najiuliza,sijui ungelikuwa mwenzangu na mimi,wewe hapo- ungelisemaje au ngelifanyeje pale unaposhtakiwa kwa maneno ya uongo? naona wewe ungerusha ngumi,au ungetukana sana kiasi kwamba mpaka wangelikuachia! lakini haikuwa hivyo kwa Yesu.

Yeye ambaye ndiye mnyenyekevu wa moyo,anakutaka na wewe usiyemnyenyekevu ukajifunze kwake huo unyenyekevu. Anakualika ujitie  “nira” yake kwa maana nira yake ni laini na mzigo wake ni mwepesi nawe utapata raha nafsini mwako. Neno “nira” ni kongwa,wanalovalishwa ngombe ili waweze kulima pamoja. ( ni kama mbao iwekwayo kwenye shingo zao,kufunga ngombe na ngombe na hatimaye mkulima mmoja uishika mbele na kuwapeleka popote atakapo,nao huenda.)Yesu ametumia piacha hiyo kutufundisha kama tukijifunga nira yake,tutaweza kumfuata popote aendapo,na tujifunze kwake unyenyekevu wake.

  • Kinyume cha unyenyekevu ni kiburi

Ikiwa mtu amekosa unyenyekevu huwa na kiburi,na kiburi ni tabia ya shetani mwenye kupenda kusifiwe. Wataalamu maandiko husema kwamba kila mwanadamu amezaliwa na tabia ya kiburi. Na ndio maana kila mtu hupenda kujisikia,kusifiwe,kuonekana n.k Lakini unyenyekevu hutoka kwa Bwana,mtu hazaliwi nao. Ukimwona mtu mnyenyekevu toka tumboni mwa mamaye hujue huyo kapewa “neema ” tu kwa maana si jambo la kawaida. Kwa hiyo utagundua kwamba unayo kazi ya kujifunza kila siku habari ya unyenyekevu wa Yesu ili kusudi uwe mnyenyekevu na utoke katika kiburi.

Suche
Kategorien
Mehr lesen
Injili Ya Yesu Kristo
AINA SABA (7) ZA UNAFIKI, AMBAZO UNAPASWA UJIEPUSHE NAZO.
Maana inayojulikana ya Unafiki ni ile hali ya kutoa maneno, au kuonyesha hisia au vitendo kwa nje...
Von GOSPEL PREACHER 2022-02-26 19:43:17 0 11KB
BIBLICAL FINANCIAL EDUCATION
How to legally change an invoice with a credit note
No matter how careful you are when invoicing, mistakes can happen. A customer’s...
Von PROSHABO ACCOUNTING 2022-02-02 03:36:35 0 8KB
JOB
Verse by verse explanation of Job 38
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 31 questions at the...
Von THE HOLY BIBLE 2022-04-03 04:20:58 0 6KB
NDOA KIBIBLIA
NAJUTA KWA NINI NILIKUBALI KUOLEWA?
Baada ya mwaka mmoja wa ndoa, Merian asema anajuta kwa nini alikubali kuolewa. Merian na Joseph...
Von GOSPEL PREACHER 2021-11-23 07:11:44 0 6KB
PHD
PHD
List of all subjects for the students who are taking PHD studies
Von PROSHABO ONLINE SCHOOLS 2021-10-09 10:56:16 0 6KB