UNYENYEKEVU.

0
5K

Bwana Yesu asifiwe...

Kwa ufupi.

” Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu; “ Mathayo 11:29

“unyenyekevu”hali ya kushuka,kukubali kuonekana mdogo/mtumishi wa wote,kukubali lawama na kuvumilia. Si jambo jepesi kukubali kuwa chini hali wewe una vitu vingi. Si rahisi hata kidogo kukubali lawama. Wengi wanapenda wawe wanyenyekevu lakini hawapo tayari kushuka,kupokea lawama,kuvumilia n.k. Unyenyekevu ni ghalama mpendwa!

  • Unyenyekevu ni tabia ya Yesu. Yesu alikuwa ni mnyenyekevu wa moyo

Yesu alikuwa mnyenyekevu wa moyo,sio wa kuigiza. Alikuli mateso yote ingawa alikuwa na uwezo wa kuyakataa,lakini kwa kusudi la kutufundisha ilimbidi akubali na kwa lile kusudi la ukombozi,alikubali yote. Fikiri pale alipopelekwa mbele wa waashi na wakuu wa makuhani kisha wakamsomea mashtaka ya uongo,lakini alikaa kimya asitie neno lolote hali akijua yote yanayoendelea. Hakika mtu huyu alikuwa ni mnyenyekevu wa moyo. Najiuliza,sijui ungelikuwa mwenzangu na mimi,wewe hapo- ungelisemaje au ngelifanyeje pale unaposhtakiwa kwa maneno ya uongo? naona wewe ungerusha ngumi,au ungetukana sana kiasi kwamba mpaka wangelikuachia! lakini haikuwa hivyo kwa Yesu.

Yeye ambaye ndiye mnyenyekevu wa moyo,anakutaka na wewe usiyemnyenyekevu ukajifunze kwake huo unyenyekevu. Anakualika ujitie  “nira” yake kwa maana nira yake ni laini na mzigo wake ni mwepesi nawe utapata raha nafsini mwako. Neno “nira” ni kongwa,wanalovalishwa ngombe ili waweze kulima pamoja. ( ni kama mbao iwekwayo kwenye shingo zao,kufunga ngombe na ngombe na hatimaye mkulima mmoja uishika mbele na kuwapeleka popote atakapo,nao huenda.)Yesu ametumia piacha hiyo kutufundisha kama tukijifunga nira yake,tutaweza kumfuata popote aendapo,na tujifunze kwake unyenyekevu wake.

  • Kinyume cha unyenyekevu ni kiburi

Ikiwa mtu amekosa unyenyekevu huwa na kiburi,na kiburi ni tabia ya shetani mwenye kupenda kusifiwe. Wataalamu maandiko husema kwamba kila mwanadamu amezaliwa na tabia ya kiburi. Na ndio maana kila mtu hupenda kujisikia,kusifiwe,kuonekana n.k Lakini unyenyekevu hutoka kwa Bwana,mtu hazaliwi nao. Ukimwona mtu mnyenyekevu toka tumboni mwa mamaye hujue huyo kapewa “neema ” tu kwa maana si jambo la kawaida. Kwa hiyo utagundua kwamba unayo kazi ya kujifunza kila siku habari ya unyenyekevu wa Yesu ili kusudi uwe mnyenyekevu na utoke katika kiburi.

Zoeken
Categorieën
Read More
OTHERS
IS MUHAMMAD THE SPIRIT OF TRUTH?
Today I will answer Muhammadans with biblical proof that Muhammad was not the Spirit of Truth as...
By MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-22 02:25:52 0 5K
Injili Ya Yesu Kristo
ISHARA ZA ZAMANI HIZI
Neno la Uzima kutoka kwa Askofu Zachary Kakobe Tovuti : http://www.bishopzacharykakobe.org...
By GOSPEL PREACHER 2022-01-12 01:55:23 4 5K
1 SAMUEL
Verse by verse explanation of 1 Samuel 31
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 25 questions at the...
By THE HOLY BIBLE 2022-01-26 05:17:22 0 6K
Injili Ya Yesu Kristo
UMEJIAANDAJE KWA TUKIO LA UNYAKUO? (Sehemu ya 1)
Nakusalimu kwa jina la Yesu! Ili uweze kuelewa somo hili mpenzi msomaji nakushauri tafuta muda...
By GOSPEL PREACHER 2021-11-23 13:07:03 0 5K
OTHERS
ALLAH ANAAPA KWA ALIYE UMBA KIUME NA KIKE
JE, NANI KAUMBA KIUME NA KIKE?QURAN 92 1-3 Naapa kwa usiku ufunikapo, 2 kwa mchana uingiapo, 3....
By MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-23 08:39:34 0 5K