Unajimu na Kutafsiri Nyota

0
5KB

Je? Mungu anasema nini kuhusu wao wanao tafsiri nyota kuweza kujua jinsi maisha yao yatakavyokuwa? Imo katika Biblia, Isaya 47:13-15 "Umechoka kwa wingi wa mashauri yako basi nawasimame hao wajuao falaki, wazitazamao nyota watabirio kila mwezi mambo ya mwezi huo, wakakuokoe na mambo yatakayokupata. Tazama watakuwa kama mabua makavu; moto utawateketeza hawatajiokoa na nguvu za mwali wa moto; hautakuwa kaa la kukota moto, wala moto wa kukaa karibu nao ndivyo itakavyokuwa mambo hayo uliyojitaabisha nayo; wale walio fanya biashara nawe tangu ujana wako watatanga-tanga mbali nawe, kila mtu akienda zake; hapatakuwa na mtu wakukuokoa." 

Unajimu ni imani ambayo yafundisha kuwa uwambatano wa mwezi, nyota na jua waweza kuleta tukio katika maisha ya mtu. Katika lugha ya kiebrania neno unajimu ni kutabiri mbingu, kuweza kutoa siri, kutabiri jambo litakalotokea. Imo katika Biblia, Walawi 19:26 "...... Msifanye kuloga, wala kutumia utambuzi." 

Kabla ya wana waisiraeli kuingia katika nchi ya ahadi, walionywa kutofanya unajimu, imo katika Biblia, Torati 18:9, 12, 14 "Utakapokwisha ingia katika nchi akupayo Bwana, Mungu wako usijifunze kutenda kwa mfano wa machukizo ya mataifa yale 12- kwamaana yule atendaye hayo ni chukizo kwa Bwana; kisha ni kwa sababu ya hayo Bwana Mungu wako anawafukuza mbele yako 14 maana mataifa haya utakaowamiliki huwasikiliza wanao shika nyakati mbaya na kutazama bao; bali wewe Bwana, Mungu wako, hukupa ruhusa kutenda hayo." 

1Samueli 15:23 "Kwani kuasi ni kama dhambi ya uchawi, na ukaidi ni kama ukafiri na vinyongo; kwa kuwa umelikataa neno la Bwana yeye naye amekukataa usiwe mfalme 

Wakati mfalme Nebukadreza alipo ota ndoto aliwaita wagana, wachawi, wasihiri na wakaldayo waweze kutafsiri ile ndoto. Imeandikwa Danieli 2:10 "Wakaldayo wakajibu mbele ya mfalme, wakasema hapana mtu duniani awezaye kulionyesha neno hili la mfalme kwa maana hapana mfalme, wala bwana wala liwali aliyetaka neno hili kwa mganga wala kwa mchawi wala kwa mkaldayo." 

Imo katika Biblia, Danieli 2:27-28. "Danieli akajibu mbele ya mfalme akasema ili siri aliyoiuliza mfalme; wenye hekima hawawezi kumfunulia mfalme; wala wachawi, wala waganga, wala wanajimu. Lakini yuko Mungu Mbinguni afunuaye siri naye amemjulisha mfalme Nebukadreza mambo yatakayo kuwa siku za mwisho."

Pesquisar
Categorias
Leia mais
EXODUS
Verse by verse explanation of Exodus 1
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 40 questions at the...
Por THE HOLY BIBLE 2022-01-21 12:33:38 0 5KB
HOLY BIBLE
CHAPA YA MNYAMA
CHAPA YA MNYAMA Mwinjilisti mmoja alisema kuwa kuipokea chapa ya mnyama/Alama ya Mnyama ni...
Por GOSPEL PREACHER 2021-11-05 23:36:21 0 7KB
OTHERS
Juhudi za Kupinga Ukristo za Mwanaharakati wa Kundi la Ahmadiah Kutoka Pakistani Zamfanya Aachane na Uislamu
Nusrat Aman alikuwa ni mwanaharakati wa kiislamu wa kundi la Ahmadiah kule Pakistani. Siku moja...
Por MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-23 09:31:32 0 5KB
OTHERS
UTATA NDANI YA KORAN: NINI KITAKUWA CHAKULA CHA WATU JEHANNAM
Leo Allah ameamua kutueleza kuwa, watu watakuwa wanakula nini huko Jehannam. Soma aya hapa...
Por MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-23 08:17:39 0 5KB
JONAH
YONA 4
Bwana wetu YESU KRISTO atukuzwe. Tunamshukuru Mungu kwa kutupa neema hii mpya ya kujifunza...
Por GOSPEL PREACHER 2022-01-20 03:14:39 0 5KB