Unajimu na Kutafsiri Nyota

0
5كيلو بايت

Je? Mungu anasema nini kuhusu wao wanao tafsiri nyota kuweza kujua jinsi maisha yao yatakavyokuwa? Imo katika Biblia, Isaya 47:13-15 "Umechoka kwa wingi wa mashauri yako basi nawasimame hao wajuao falaki, wazitazamao nyota watabirio kila mwezi mambo ya mwezi huo, wakakuokoe na mambo yatakayokupata. Tazama watakuwa kama mabua makavu; moto utawateketeza hawatajiokoa na nguvu za mwali wa moto; hautakuwa kaa la kukota moto, wala moto wa kukaa karibu nao ndivyo itakavyokuwa mambo hayo uliyojitaabisha nayo; wale walio fanya biashara nawe tangu ujana wako watatanga-tanga mbali nawe, kila mtu akienda zake; hapatakuwa na mtu wakukuokoa." 

Unajimu ni imani ambayo yafundisha kuwa uwambatano wa mwezi, nyota na jua waweza kuleta tukio katika maisha ya mtu. Katika lugha ya kiebrania neno unajimu ni kutabiri mbingu, kuweza kutoa siri, kutabiri jambo litakalotokea. Imo katika Biblia, Walawi 19:26 "...... Msifanye kuloga, wala kutumia utambuzi." 

Kabla ya wana waisiraeli kuingia katika nchi ya ahadi, walionywa kutofanya unajimu, imo katika Biblia, Torati 18:9, 12, 14 "Utakapokwisha ingia katika nchi akupayo Bwana, Mungu wako usijifunze kutenda kwa mfano wa machukizo ya mataifa yale 12- kwamaana yule atendaye hayo ni chukizo kwa Bwana; kisha ni kwa sababu ya hayo Bwana Mungu wako anawafukuza mbele yako 14 maana mataifa haya utakaowamiliki huwasikiliza wanao shika nyakati mbaya na kutazama bao; bali wewe Bwana, Mungu wako, hukupa ruhusa kutenda hayo." 

1Samueli 15:23 "Kwani kuasi ni kama dhambi ya uchawi, na ukaidi ni kama ukafiri na vinyongo; kwa kuwa umelikataa neno la Bwana yeye naye amekukataa usiwe mfalme 

Wakati mfalme Nebukadreza alipo ota ndoto aliwaita wagana, wachawi, wasihiri na wakaldayo waweze kutafsiri ile ndoto. Imeandikwa Danieli 2:10 "Wakaldayo wakajibu mbele ya mfalme, wakasema hapana mtu duniani awezaye kulionyesha neno hili la mfalme kwa maana hapana mfalme, wala bwana wala liwali aliyetaka neno hili kwa mganga wala kwa mchawi wala kwa mkaldayo." 

Imo katika Biblia, Danieli 2:27-28. "Danieli akajibu mbele ya mfalme akasema ili siri aliyoiuliza mfalme; wenye hekima hawawezi kumfunulia mfalme; wala wachawi, wala waganga, wala wanajimu. Lakini yuko Mungu Mbinguni afunuaye siri naye amemjulisha mfalme Nebukadreza mambo yatakayo kuwa siku za mwisho."

البحث
الأقسام
إقرأ المزيد
2 CHRONICLES
Verse by verse explanation of 2 Chronicles 3
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 30 questions at the...
بواسطة THE HOLY BIBLE 2022-04-01 21:58:36 0 5كيلو بايت
Injili Ya Yesu Kristo
Biblia inasema je ju ya chale/ kujitoboa mwili?
Agano la kale liliwaamuru waIsraeli, “Msiikate miili yenu kwa ajili ya wafu wala kuchanja...
بواسطة MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-24 04:11:41 0 6كيلو بايت
OTHERS
Ni kwa nini uzao wa ubikira ni wa maana?
 Funzo la uzao wa ubikira ni la maana sana (Isaya 7:14 Mathayo 1:23; Luka 1:27,34). Kwanza,...
بواسطة MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-23 09:41:23 0 5كيلو بايت
Networking
How to build your marketplace supply
Compared to traditional e-commerce, most of a marketplace's unique challenges come from the...
بواسطة Business Academy 2022-09-17 04:08:49 0 10كيلو بايت
Injili Ya Yesu Kristo
Jinsi Ya Kumpokea Roho Mtakatifu
“Je Unajua kuwa watumishi wengi sasa wanaogopa kufanya maombezi ya kuombea watu ujazo wa...
بواسطة GOSPEL PREACHER 2022-04-01 15:48:30 0 7كيلو بايت