Unajimu na Kutafsiri Nyota

0
5كيلو بايت

Je? Mungu anasema nini kuhusu wao wanao tafsiri nyota kuweza kujua jinsi maisha yao yatakavyokuwa? Imo katika Biblia, Isaya 47:13-15 "Umechoka kwa wingi wa mashauri yako basi nawasimame hao wajuao falaki, wazitazamao nyota watabirio kila mwezi mambo ya mwezi huo, wakakuokoe na mambo yatakayokupata. Tazama watakuwa kama mabua makavu; moto utawateketeza hawatajiokoa na nguvu za mwali wa moto; hautakuwa kaa la kukota moto, wala moto wa kukaa karibu nao ndivyo itakavyokuwa mambo hayo uliyojitaabisha nayo; wale walio fanya biashara nawe tangu ujana wako watatanga-tanga mbali nawe, kila mtu akienda zake; hapatakuwa na mtu wakukuokoa." 

Unajimu ni imani ambayo yafundisha kuwa uwambatano wa mwezi, nyota na jua waweza kuleta tukio katika maisha ya mtu. Katika lugha ya kiebrania neno unajimu ni kutabiri mbingu, kuweza kutoa siri, kutabiri jambo litakalotokea. Imo katika Biblia, Walawi 19:26 "...... Msifanye kuloga, wala kutumia utambuzi." 

Kabla ya wana waisiraeli kuingia katika nchi ya ahadi, walionywa kutofanya unajimu, imo katika Biblia, Torati 18:9, 12, 14 "Utakapokwisha ingia katika nchi akupayo Bwana, Mungu wako usijifunze kutenda kwa mfano wa machukizo ya mataifa yale 12- kwamaana yule atendaye hayo ni chukizo kwa Bwana; kisha ni kwa sababu ya hayo Bwana Mungu wako anawafukuza mbele yako 14 maana mataifa haya utakaowamiliki huwasikiliza wanao shika nyakati mbaya na kutazama bao; bali wewe Bwana, Mungu wako, hukupa ruhusa kutenda hayo." 

1Samueli 15:23 "Kwani kuasi ni kama dhambi ya uchawi, na ukaidi ni kama ukafiri na vinyongo; kwa kuwa umelikataa neno la Bwana yeye naye amekukataa usiwe mfalme 

Wakati mfalme Nebukadreza alipo ota ndoto aliwaita wagana, wachawi, wasihiri na wakaldayo waweze kutafsiri ile ndoto. Imeandikwa Danieli 2:10 "Wakaldayo wakajibu mbele ya mfalme, wakasema hapana mtu duniani awezaye kulionyesha neno hili la mfalme kwa maana hapana mfalme, wala bwana wala liwali aliyetaka neno hili kwa mganga wala kwa mchawi wala kwa mkaldayo." 

Imo katika Biblia, Danieli 2:27-28. "Danieli akajibu mbele ya mfalme akasema ili siri aliyoiuliza mfalme; wenye hekima hawawezi kumfunulia mfalme; wala wachawi, wala waganga, wala wanajimu. Lakini yuko Mungu Mbinguni afunuaye siri naye amemjulisha mfalme Nebukadreza mambo yatakayo kuwa siku za mwisho."

البحث
الأقسام
إقرأ المزيد
JUDGES
Book of Judges Explained
Title: The book bears the fitting name “Judges,” which refers to unique leaders...
بواسطة THE HOLY BIBLE 2022-01-25 08:58:35 0 6كيلو بايت
ESTHER
ESTA SURA YA 4
BWANA wetu YESU KRISTO atukuzwe. Karibu katika uchambuzi wa kitabu cha Esta. Leo tukiwa...
بواسطة GOSPEL PREACHER 2022-01-20 02:49:30 0 6كيلو بايت
NDOA KIBIBLIA
HATUA TATU MUHIMU KABLA YA KUFUNGA PINGU ZA MAISHA
Mojawapo ya swali gumu kuhusiana na mahusiano ni pale vijana wanapouliza wakae kwenye uchumba kwa...
بواسطة GOSPEL PREACHER 2021-11-06 14:30:07 0 6كيلو بايت
REVELATION
UFUNUO 19
Karibu tujifunze biblia na huu ni mwendelezo wa kitabu cha Ufunuo leo tukiwa katika ule mlango wa...
بواسطة GOSPEL PREACHER 2021-10-30 12:21:07 6 6كيلو بايت
JOB
Verse by verse explanation of Job 24
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 25 questions at the...
بواسطة THE HOLY BIBLE 2022-04-03 03:55:26 0 5كيلو بايت