Biblia inasema je ju ya chale/ kujitoboa mwili?

0
5K
Agano la kale liliwaamuru waIsraeli, “Msiikate miili yenu kwa ajili ya wafu wala kuchanja chale juu ya ngozi za miili yenu.Mimi ni Bwana” (mambo ya walawi 19:28). Hata hivyo ijapokuwa waumini kwa sasa hawako chini ya sheria ya agano la kale (warumi 10:4; wagalatia 3:23 – 25; waefeso 2:15), hoja ya kuwa kulikuwa na sheria juu ya chale lazima lituletee maswaliagano jipya haisemi lolote juu ya muumini achanjwe chale au asichanjwe.
 
Kulengana na swala la chale na kujikata alama mwilini, mtazamo wetu ni uwe; je, twaweza kumuomba Mungu atumie alama hizo kwa utukufu wake? “kwa hivyo mnapokula, mnapokunywa, chochote mfanyacho, kifanyeni kwa utukufu wa Mungu” (wakorintho wa kwanza 10:31). Biblia haituamuru kinyume cha chale na alama za mwili lakini pia haituonyeshi ya kuwa ana haja na alama hizo miilini mwetu.
 
Jambo lengine ni nidhamu. Biblia inatushauri kuvaa mavazi yetu kwa nidhamu (Timotheo wa kwanza 2:9). Kuvaa ki nidhamu ni kuziba sehemu zote zilizotarajiwa kuzibwa na mavazi. Lengo la nidhamu hii ya ki mavazi si juu ya wewe mwenyewe bali kwa ajili ya wengine wasije wakanaswa na hali yakuvutiwa nawe kiasi cha kukutamani. Chale pia zinaushawishi Fulani kwa hivyo zinakeuka mipaka ya nidhamu hii.
 
Kanuni muhimu ya kibiblia ni kutazama jambo kwa mfumo wa imani. Kama hulionei shaka moyoni juu yakuwa linampendeza Mungu basi lifanye. “kwa kuwa lolote ambalo, si la imani ni dhambi” (warumi 14:23). Tunapaswa kufahamu kuwa miili yetu na nafsi zetu pia zimekombolewa na ni mali ya Mungu. Ijapokuwa haelekei moja kwa moja juu ya chale na alama za miili, wakorintho wa kwanza 6:19 -20 inatupatia kanuni moja, “Nini? Hamjui ya kuwa miili yenu ni hekalu la Roho Mtakatifu, akaaye ndani yenu, ambaye mnaye kutoka kwa Mungu na ninyi si mali yenu wenyewe. Mmenunuliwa kwa thamani kwa hivyo mtukuzeni Mungu katika miili yenu na katika roho zenu ambvyo ni vya Mungu.” Miili yetu sharti iandamane na ukweli kokote tuendako. Kama miili yetu ni mali ya Mungu basi lazima tuwe na ruhusa yake kabla hatujajichanja chale hizo au alama hizo za mwili.
Search
Categories
Read More
HOLY BIBLE
Is it okay to have sinners who are non-Christians as friends?
Yes, it's okay to have non-Christians as friends.  However, we don't want our friendships...
By MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-24 05:39:19 0 5K
EXODUS
Verse by verse explanation of Exodus 26
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 35 questions at the...
By THE HOLY BIBLE 2022-01-22 18:15:15 0 5K
Injili Ya Yesu Kristo
KUBOMOA MADHABAHU ZA SHETANI
Madhabahu ni nini? Ni daraja la kuunganisha katika ya ulimwengu wa roho wa Mungu au shetani. Kuna...
By GOSPEL PREACHER 2021-11-19 07:26:43 0 7K
NDOA KIBIBLIA
KIPI KINAHITAJI MAANDALIZI SANA KATI YA NDOA NA HARUSI?
Shalom mpendwa wangu katika Kristo Yesu, Leo katika kona yetu hii ya mahusiano ya uchumba na...
By GOSPEL PREACHER 2021-11-06 15:04:24 0 5K
2 CHRONICLES
Verse by verse explanation of 2 Chronicles 7
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 26 questions at the...
By THE HOLY BIBLE 2022-04-01 22:07:35 0 5K