Biblia inasema je ju ya chale/ kujitoboa mwili?

0
6KB
Agano la kale liliwaamuru waIsraeli, “Msiikate miili yenu kwa ajili ya wafu wala kuchanja chale juu ya ngozi za miili yenu.Mimi ni Bwana” (mambo ya walawi 19:28). Hata hivyo ijapokuwa waumini kwa sasa hawako chini ya sheria ya agano la kale (warumi 10:4; wagalatia 3:23 – 25; waefeso 2:15), hoja ya kuwa kulikuwa na sheria juu ya chale lazima lituletee maswaliagano jipya haisemi lolote juu ya muumini achanjwe chale au asichanjwe.
 
Kulengana na swala la chale na kujikata alama mwilini, mtazamo wetu ni uwe; je, twaweza kumuomba Mungu atumie alama hizo kwa utukufu wake? “kwa hivyo mnapokula, mnapokunywa, chochote mfanyacho, kifanyeni kwa utukufu wa Mungu” (wakorintho wa kwanza 10:31). Biblia haituamuru kinyume cha chale na alama za mwili lakini pia haituonyeshi ya kuwa ana haja na alama hizo miilini mwetu.
 
Jambo lengine ni nidhamu. Biblia inatushauri kuvaa mavazi yetu kwa nidhamu (Timotheo wa kwanza 2:9). Kuvaa ki nidhamu ni kuziba sehemu zote zilizotarajiwa kuzibwa na mavazi. Lengo la nidhamu hii ya ki mavazi si juu ya wewe mwenyewe bali kwa ajili ya wengine wasije wakanaswa na hali yakuvutiwa nawe kiasi cha kukutamani. Chale pia zinaushawishi Fulani kwa hivyo zinakeuka mipaka ya nidhamu hii.
 
Kanuni muhimu ya kibiblia ni kutazama jambo kwa mfumo wa imani. Kama hulionei shaka moyoni juu yakuwa linampendeza Mungu basi lifanye. “kwa kuwa lolote ambalo, si la imani ni dhambi” (warumi 14:23). Tunapaswa kufahamu kuwa miili yetu na nafsi zetu pia zimekombolewa na ni mali ya Mungu. Ijapokuwa haelekei moja kwa moja juu ya chale na alama za miili, wakorintho wa kwanza 6:19 -20 inatupatia kanuni moja, “Nini? Hamjui ya kuwa miili yenu ni hekalu la Roho Mtakatifu, akaaye ndani yenu, ambaye mnaye kutoka kwa Mungu na ninyi si mali yenu wenyewe. Mmenunuliwa kwa thamani kwa hivyo mtukuzeni Mungu katika miili yenu na katika roho zenu ambvyo ni vya Mungu.” Miili yetu sharti iandamane na ukweli kokote tuendako. Kama miili yetu ni mali ya Mungu basi lazima tuwe na ruhusa yake kabla hatujajichanja chale hizo au alama hizo za mwili.
Suche
Kategorien
Mehr lesen
GENESIS
Verse by verse explanation of Genesis 1
o GENESIS 1   GENESIS 2   GENESIS 3   GENESIS 4   GENESIS 5   GENESIS 6...
Von GOSPEL PREACHER 2021-08-25 14:33:52 0 5KB
OTHERS
If Jesus was God, why did He say 'No one is good but God alone'?
It is often claimed by those who reject the deity of Christ that inMark 10:17-22Jesus denies His...
Von MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-23 09:46:29 0 5KB
OTHERS
Kutoka Kwenye Uislamu Hadi Kwenye Ukristo
Jina langu ni Tahir na hii ni safari yangu kutoka kwenye Uislamu hadi kwenye Ukristo. Mara baada...
Von MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-22 04:07:45 0 5KB
2 SAMUEL
Verse by verse explanation of 2 Samuel 12
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 33 questions at the...
Von THE HOLY BIBLE 2022-02-05 09:42:45 0 5KB
JUDGES
Book of Judges Explained
Title: The book bears the fitting name “Judges,” which refers to unique leaders...
Von THE HOLY BIBLE 2022-01-25 08:58:35 0 6KB