Biblia inasema je ju ya chale/ kujitoboa mwili?

0
5كيلو بايت
Agano la kale liliwaamuru waIsraeli, “Msiikate miili yenu kwa ajili ya wafu wala kuchanja chale juu ya ngozi za miili yenu.Mimi ni Bwana” (mambo ya walawi 19:28). Hata hivyo ijapokuwa waumini kwa sasa hawako chini ya sheria ya agano la kale (warumi 10:4; wagalatia 3:23 – 25; waefeso 2:15), hoja ya kuwa kulikuwa na sheria juu ya chale lazima lituletee maswaliagano jipya haisemi lolote juu ya muumini achanjwe chale au asichanjwe.
 
Kulengana na swala la chale na kujikata alama mwilini, mtazamo wetu ni uwe; je, twaweza kumuomba Mungu atumie alama hizo kwa utukufu wake? “kwa hivyo mnapokula, mnapokunywa, chochote mfanyacho, kifanyeni kwa utukufu wa Mungu” (wakorintho wa kwanza 10:31). Biblia haituamuru kinyume cha chale na alama za mwili lakini pia haituonyeshi ya kuwa ana haja na alama hizo miilini mwetu.
 
Jambo lengine ni nidhamu. Biblia inatushauri kuvaa mavazi yetu kwa nidhamu (Timotheo wa kwanza 2:9). Kuvaa ki nidhamu ni kuziba sehemu zote zilizotarajiwa kuzibwa na mavazi. Lengo la nidhamu hii ya ki mavazi si juu ya wewe mwenyewe bali kwa ajili ya wengine wasije wakanaswa na hali yakuvutiwa nawe kiasi cha kukutamani. Chale pia zinaushawishi Fulani kwa hivyo zinakeuka mipaka ya nidhamu hii.
 
Kanuni muhimu ya kibiblia ni kutazama jambo kwa mfumo wa imani. Kama hulionei shaka moyoni juu yakuwa linampendeza Mungu basi lifanye. “kwa kuwa lolote ambalo, si la imani ni dhambi” (warumi 14:23). Tunapaswa kufahamu kuwa miili yetu na nafsi zetu pia zimekombolewa na ni mali ya Mungu. Ijapokuwa haelekei moja kwa moja juu ya chale na alama za miili, wakorintho wa kwanza 6:19 -20 inatupatia kanuni moja, “Nini? Hamjui ya kuwa miili yenu ni hekalu la Roho Mtakatifu, akaaye ndani yenu, ambaye mnaye kutoka kwa Mungu na ninyi si mali yenu wenyewe. Mmenunuliwa kwa thamani kwa hivyo mtukuzeni Mungu katika miili yenu na katika roho zenu ambvyo ni vya Mungu.” Miili yetu sharti iandamane na ukweli kokote tuendako. Kama miili yetu ni mali ya Mungu basi lazima tuwe na ruhusa yake kabla hatujajichanja chale hizo au alama hizo za mwili.
البحث
الأقسام
إقرأ المزيد
EZRA
Verse by verse explanation of Ezra 10
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 25 questions at the...
بواسطة THE HOLY BIBLE 2022-04-02 06:26:03 0 5كيلو بايت
Injili Ya Yesu Kristo
UNAJIFUNZA NINI KUPITIA HUDUMA YA ANANIA NA BARNABA KWA PAULO?
Nakusalimu katika jina la Bwana, mpenzi msomaji.   Katika nyanja hii, leo nimeona ni vema...
بواسطة GOSPEL PREACHER 2021-11-23 12:24:28 0 4كيلو بايت
2 CHRONICLES
Verse by verse explanation of 2 Chronicles 4
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 30 questions at the...
بواسطة THE HOLY BIBLE 2022-04-01 22:00:21 0 5كيلو بايت
Injili Ya Yesu Kristo
MAOMBI PEKE YAKE BILA IMANI HAYATOSHI KUTENGENEZA JIBU LA MAHITAJI YAKO.
Marko 9:14-29. Hii ni habari ya yule baba aliyekuwa na mwana mwenye pepo bubu na kiziwi, akamleta...
بواسطة GOSPEL PREACHER 2021-11-23 12:47:11 0 4كيلو بايت
OTHERS
UTATU UNATHIBITISHWA KWA KUTUMIA HESABU/HISABATI
Kumekuwa na madai na hoja nyingi sana kuhusu hili swala la UTATU. Wengine wanasema kuwa...
بواسطة MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-24 22:58:07 0 4كيلو بايت