Eti Biblia inataja mashehe, kwa hiyo inaunga mkono Uislamu!

0
5KB

Wahubiri wa ‘injili’ wa Kiislamu wanaendelea kuhaha kuhalalisha quran kupitia Biblia. Nasema ‘kuhaha’ kwa sababu hakika kabisa wana juhudi kubwa mno lakini inasikitisha kwa sababu hakuna hata siku moja waliyowahi kusema jambo lenye ukweli kibiblia linalounga mkono quran kama wasemavyo wao – Mungu ni shahidi yangu. Mara waseme Muhammad ametabiriwa kwenye Biblia; mara waseme Yesu aliposema kuwa ataletwa Msaidizi basi alimaanisha Muhammad, n.k. Ni kituko kimoja baada ya kingine. Na wanayemdanganya ni wao wenyewe pamoja na Wakristo wachache wasiojua Biblia.

Kwa msingi huohuo, wanasema eti Biblia imewataja mashehe; na kwa hiyo kwao huo ni ushahidi kuwa uislamu ulikuwapo tangu zamani.

Acha ninukuu hoja ya mmoja wao kama ilivyo, kuhusiana na suala hili, kisha kama kawaida, utaona jinsi hoja hiyo inavyosambaratika mbele za nuru ya Kristo, yaani neno lake.

Mtu huyu anasema:

Swali kwenu nyinyi ambao hamjabahatika kuwa waislam, yaani Wakristo. Kama uislam uliletwa na muhammad s.a.w, vipi masheikh watajwe ndani ya agano la kale?

“Ndivyo walivyosimama mikutano miwili yao walioshukuru nyumbani mwa mungu, na mimi, na nusu ya mashehepamoja nami.” (Nehemia 12:40)

Mkristo jiulize mwenyewe hili swali; mashehe ni viongozi wa dini ipi? waislam...!? au wakristo?

Mwisho wa kunukuu.

Hapa huyu ndugu wa Kiislamu anaongea kwa ujasiri kabisa na kwa kituo. Na unaona kabisa kuwa moyoni mwake anawaza, “Hapa leo nimewapata Wakristo. Lazima waone kuwa Uislamu ndiyo dini ya kweli.”

Na hivi ndivyo ilivyo kwa hoja zao ZOTE kuhusiana na Ukristo. NI UONGO; NI UONGO; NI UONGO!! NI UPOTOVU MTUPU!!

Na mimi nilimpatia jibu fupi tu na rahisi. Kwanza nikamwambia acha nikupatie maana ya neno ‘shehe’ kutoka kwenye kamusi ya Kiswahili.

Kama inavyoonekana hapo juu, kuna maana mbili. Na ni wazi kabisa kuwa, kwa ufahamu wa kawaida kabisa, muktadha wa aya hii ya Nehemia haiongelei maana ya kwanza ya neno hili. Kwanza, wakati Nehemia anaandika, Uislamu haukuwapo. Uislamu ni wa juzijuzi tu; miaka 600 baada ya Yesu kuondoka duniani.

Kisha nikamwambia, soma pia aya hiyo kwa Kiingereza. Imeandikwa hivi: “So stood the two companies of them that gave thanks in the house of God, and I, and the half of THE RULERS with me”

Hilo neno ‘mashehe’ limeandikwa kama ‘rulers’ yaani viongozi. Na hii ndiyo maana inayoendana na ile ya pili kwenye kamusi, yaani wazee wenye busara.

 

Hitimisho

Usidanganywe na tafsiri za Biblia zinazotolewa na Waislamu (siongelei tafsiri za quran; hilo ni suala jingine). Tafsiri za Biblia zinazotolewa na Waislamu ni uongo na upotoshaji mtupu kwa asilimia 100. Kila wanachosema kuhusu Biblia ni kifungo kinachowapeleka watu kuzimu kama wakikiamini.

Ukiwaamini, utakuwa umetupa taji yako; na umeuza uzaliwa wako wa kwanza kwa ujira wa kunde kama Esau.

Bwana Yesu anasema:

“Naja upesi. Shika sana ulicho nacho, asije mtu akaitwaa taji yako.” (Ufunuo 3:11)

Kaa chonjo; adui anahaha kila mahali kukuibia uzima wako wa milele.

Tafakari

Hoji mambo

Chukua hatua

Rechercher
Catégories
Lire la suite
JUDGES
Verse by verse explanation of Judges 13
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 39 questions at the...
Par THE HOLY BIBLE 2022-01-25 11:07:08 0 5KB
OTHERS
Jesus and Islam
Here are six questions that followers of Islam, and others, often ask about Jesus... This will...
Par MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-23 09:45:24 0 5KB
MASWALI & MAJIBU
Naomba Kujua Watakaoenda Mbinguni Je! Ni Wengi Au Wachache?
JIBU: watakaoenda mbinguni je! ni wengi au wachache?..Ni swali ambalo halikuulizwa tu na...
Par GOSPEL PREACHER 2022-06-13 09:01:02 0 7KB
JOSHUA
Verse by verse explanation of Joshua 20
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 23 questions at the...
Par THE HOLY BIBLE 2022-01-25 08:27:26 0 5KB
SPIRITUAL EDUCATION
NGURUMO SABA
Katika kufunguliwa kwa mihuri saba, kwenye kile kitabu cha ufunuo, tunaona kuwa muhuri wa saba...
Par GOSPEL PREACHER 2021-10-30 11:00:50 0 5KB