NI NINI MAANA YA “ROHO”?

0
6Кб
Hebu tuzungumzie jinsi Biblia inavyotumia neno “roho.” Watu fulani hufikiri kwamba “roho” ni neno lingine linalomaanisha “nafsi.” Lakini, si kweli. Biblia inaonyesha wazi kwamba “roho” na “nafsi” ni vitu viwili tofauti. Vinatofautianaje?
 
Waandishi wa Biblia walitumia neno la Kiebrania ru′ach au neno la Kigiriki, pneu′ma waliporejelea “roho.” Maandiko yenyewe yanaonyesha maana ya maneno hayo. Kwa mfano, andiko la Zaburi 104:29 linasema: “[Yehova] ukiiondoa roho [ru′ach] yao, wanakata pumzi, na kurudi katika mavumbi yao.” Andiko la Yakobo 2:26 linasema kwamba “mwili bila roho [pneu′ma] umekufa.” Katika andiko hilo “roho” inamaanisha kile ambacho huupa mwili uhai. Bila roho, mwili umekufa. Kwa hiyo, katika Biblia neno ru′ach halitafsiriwi tu “roho” bali pia “nguvu” au kani ya uhai. Kwa mfano, Mungu alisema hivi kuhusu Mafuriko ya siku ya Noa: “Ninaleta gharika ya maji duniani ili kuharibu kutoka chini ya mbingu wote wenye mwili walio na nguvu [ru′ach] za uhai ndani yao.” (Mwanzo 6:17; 7:15, 22) Hivyo, “roho” inarejelea nguvu isiyoonekana, inayotendesha viumbe vyote vilivyo hai.
 
Redio
Nafsi na roho hutofautiana. Mwili unahitaji roho kama vile redio inavyohitaji umeme ili kufanya kazi. Kwa mfano, unapotia betri katika redio na kuiwasha, nguvu zilizo katika betri huiwezesha redio kufanya kazi. Hata hivyo, redio haiwezi kufanya kazi bila betri. Hali kadhalika, redio ambayo imeondolewa kwenye umeme haiwezi kufanya kazi. Vivyo hivyo, roho ni nguvu ambayo hutendesha mwili wetu. Kama umeme, roho haiwezi kuhisi wala kufikiri. Ni nguvu isiyo na utu. Lakini bila roho au kani ya uhai, “tunakata pumzi na kurudi kwenye udongo,” kama mtunga-zaburi alivyosema.
 
Andiko la Mhubiri 12:7 linasema hivi linapozungumzia kifo cha mwanadamu: “Mavumbi [mwili wake] huirudia nchi kama yalivyokuwa, nayo roho yenyewe humrudia Mungu wa kweli aliyeitoa.” Roho au kani ya uhai inapoondoka mwilini, mwili hufa na kurudi ulipotoka, yaani, kwenye udongo. Vivyo hivyo, nguvu ya uhai hurudi ilipotoka, yaani, kwa Mungu. (Ayubu 34:14, 15; Zaburi 36:9) Hiyo haimaanishi kwamba nguvu ya uhai huenda mbinguni kihalisi. Badala yake, inamaanisha kwamba mtu akifa, tumaini lolote la kuishi tena linamtegemea Yehova Mungu. Ni kana kwamba uhai wake uko mikononi mwa Mungu. Ni kupitia nguvu za Mungu tu ndipo roho au nguvu ya uhai inaweza kurudishwa ili mtu aweze kuishi tena.
 
Inafariji kama nini kujua kwamba hivyo ndivyo Mungu atakavyofanya kwa wote wanaopumzika ndani ya “makaburi ya ukumbusho!” (Yohana 5:28, 29) Wakati wa ufufuo, Yehova atamfanyizia mwili mpya yule anayelala katika kifo na kuuhuisha kwa kutia roho, au nguvu ya uhai ndani yake. Itakuwa siku ya shangwe sana.
Поиск
Категории
Больше
NDOA KIBIBLIA
SHAMBA LA MTU MVIVU, ASIYE NA AKLI: MAHUSIANO YA NDOA (NA UCHUMBA)
MAHUSIANO: SHAMBA LA MTU MVIVU, ASIYE NA AKLI(Uvivu na Kukosa Akili Kichocheo Cha...
От GOSPEL PREACHER 2021-11-07 23:23:24 0 4Кб
PSALMS
Verse by verse explanation of Psalm 1
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 34 questions at the...
От THE HOLY BIBLE 2022-04-04 17:53:38 0 5Кб
JOB
Verse by verse explanation of Job 30
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 25 questions at the...
От THE HOLY BIBLE 2022-04-03 04:07:11 0 5Кб
Injili Ya Yesu Kristo
KWA NINI IMANI YA MWANAMKE MKANANAYO ILIONEKANA KUWA KUBWA?
Nakusalimu kwa jina la Bwana, amani na iwe kwako. Katika Mathayo 15:21-28 maandiko...
От GOSPEL PREACHER 2021-11-23 12:17:48 0 5Кб
MAHUSIANO KIBIBLIA
SEHEMU YA 5: MISINGI YA KIIMANI KATIKA MAHUSIANO YA UCHUMBA HADI NDOA
Bwana asifiwe!! Unaweza kusoma SEHEMU YA 1, SEHEMU YA 2, SEHEMU YA 3, SEHEMU YA 4 ya somo hili,...
От GOSPEL PREACHER 2021-11-06 11:49:18 0 5Кб