NI NINI MAANA YA “ROHO”?

0
6K
Hebu tuzungumzie jinsi Biblia inavyotumia neno “roho.” Watu fulani hufikiri kwamba “roho” ni neno lingine linalomaanisha “nafsi.” Lakini, si kweli. Biblia inaonyesha wazi kwamba “roho” na “nafsi” ni vitu viwili tofauti. Vinatofautianaje?
 
Waandishi wa Biblia walitumia neno la Kiebrania ru′ach au neno la Kigiriki, pneu′ma waliporejelea “roho.” Maandiko yenyewe yanaonyesha maana ya maneno hayo. Kwa mfano, andiko la Zaburi 104:29 linasema: “[Yehova] ukiiondoa roho [ru′ach] yao, wanakata pumzi, na kurudi katika mavumbi yao.” Andiko la Yakobo 2:26 linasema kwamba “mwili bila roho [pneu′ma] umekufa.” Katika andiko hilo “roho” inamaanisha kile ambacho huupa mwili uhai. Bila roho, mwili umekufa. Kwa hiyo, katika Biblia neno ru′ach halitafsiriwi tu “roho” bali pia “nguvu” au kani ya uhai. Kwa mfano, Mungu alisema hivi kuhusu Mafuriko ya siku ya Noa: “Ninaleta gharika ya maji duniani ili kuharibu kutoka chini ya mbingu wote wenye mwili walio na nguvu [ru′ach] za uhai ndani yao.” (Mwanzo 6:17; 7:15, 22) Hivyo, “roho” inarejelea nguvu isiyoonekana, inayotendesha viumbe vyote vilivyo hai.
 
Redio
Nafsi na roho hutofautiana. Mwili unahitaji roho kama vile redio inavyohitaji umeme ili kufanya kazi. Kwa mfano, unapotia betri katika redio na kuiwasha, nguvu zilizo katika betri huiwezesha redio kufanya kazi. Hata hivyo, redio haiwezi kufanya kazi bila betri. Hali kadhalika, redio ambayo imeondolewa kwenye umeme haiwezi kufanya kazi. Vivyo hivyo, roho ni nguvu ambayo hutendesha mwili wetu. Kama umeme, roho haiwezi kuhisi wala kufikiri. Ni nguvu isiyo na utu. Lakini bila roho au kani ya uhai, “tunakata pumzi na kurudi kwenye udongo,” kama mtunga-zaburi alivyosema.
 
Andiko la Mhubiri 12:7 linasema hivi linapozungumzia kifo cha mwanadamu: “Mavumbi [mwili wake] huirudia nchi kama yalivyokuwa, nayo roho yenyewe humrudia Mungu wa kweli aliyeitoa.” Roho au kani ya uhai inapoondoka mwilini, mwili hufa na kurudi ulipotoka, yaani, kwenye udongo. Vivyo hivyo, nguvu ya uhai hurudi ilipotoka, yaani, kwa Mungu. (Ayubu 34:14, 15; Zaburi 36:9) Hiyo haimaanishi kwamba nguvu ya uhai huenda mbinguni kihalisi. Badala yake, inamaanisha kwamba mtu akifa, tumaini lolote la kuishi tena linamtegemea Yehova Mungu. Ni kana kwamba uhai wake uko mikononi mwa Mungu. Ni kupitia nguvu za Mungu tu ndipo roho au nguvu ya uhai inaweza kurudishwa ili mtu aweze kuishi tena.
 
Inafariji kama nini kujua kwamba hivyo ndivyo Mungu atakavyofanya kwa wote wanaopumzika ndani ya “makaburi ya ukumbusho!” (Yohana 5:28, 29) Wakati wa ufufuo, Yehova atamfanyizia mwili mpya yule anayelala katika kifo na kuuhuisha kwa kutia roho, au nguvu ya uhai ndani yake. Itakuwa siku ya shangwe sana.
Căutare
Categorii
Citeste mai mult
Injili Ya Yesu Kristo
YESU NDIE NJIA NA KWELI NA UZIMA. Kumbe Dini sio Njia
Katika Biblia tunasoma kuwa Yesu anasema yeye ndie "KWELI" na anaendelea kusema kuwa KWELI ndiyo...
By MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-23 08:34:15 0 5K
SPIRITUAL EDUCATION
Malaika Waliofanya Dhambi
Biblia inafundisha kwamba Mungu ni Roho na kwamba viumbe wake wa kwanza walikuwa roho. (Yohana...
By MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-22 02:35:16 0 5K
NDOA KIBIBLIA
MTOFAUTISHE NA WENGINE
KWELI KUU: Mwenzi wako wa ndoa hafanani na yeyote yule, anafanana na wewe, na wala halingani...
By GOSPEL PREACHER 2021-11-08 00:22:40 0 6K
STANDARD 3
STANDARD 3
List of all subjects for the standard 3 class
By PROSHABO ONLINE SCHOOLS 2021-10-09 10:19:35 0 5K
DEUTERONOMY
Book of Deuteronomy Explained
Deuteronomy is one of the most significant books in the Old Testament. Judging from the number of...
By THE HOLY BIBLE 2022-01-24 16:11:35 0 7K