NI NINI MAANA YA “ROHO”?

0
7K
Hebu tuzungumzie jinsi Biblia inavyotumia neno “roho.” Watu fulani hufikiri kwamba “roho” ni neno lingine linalomaanisha “nafsi.” Lakini, si kweli. Biblia inaonyesha wazi kwamba “roho” na “nafsi” ni vitu viwili tofauti. Vinatofautianaje?
 
Waandishi wa Biblia walitumia neno la Kiebrania ru′ach au neno la Kigiriki, pneu′ma waliporejelea “roho.” Maandiko yenyewe yanaonyesha maana ya maneno hayo. Kwa mfano, andiko la Zaburi 104:29 linasema: “[Yehova] ukiiondoa roho [ru′ach] yao, wanakata pumzi, na kurudi katika mavumbi yao.” Andiko la Yakobo 2:26 linasema kwamba “mwili bila roho [pneu′ma] umekufa.” Katika andiko hilo “roho” inamaanisha kile ambacho huupa mwili uhai. Bila roho, mwili umekufa. Kwa hiyo, katika Biblia neno ru′ach halitafsiriwi tu “roho” bali pia “nguvu” au kani ya uhai. Kwa mfano, Mungu alisema hivi kuhusu Mafuriko ya siku ya Noa: “Ninaleta gharika ya maji duniani ili kuharibu kutoka chini ya mbingu wote wenye mwili walio na nguvu [ru′ach] za uhai ndani yao.” (Mwanzo 6:17; 7:15, 22) Hivyo, “roho” inarejelea nguvu isiyoonekana, inayotendesha viumbe vyote vilivyo hai.
 
Redio
Nafsi na roho hutofautiana. Mwili unahitaji roho kama vile redio inavyohitaji umeme ili kufanya kazi. Kwa mfano, unapotia betri katika redio na kuiwasha, nguvu zilizo katika betri huiwezesha redio kufanya kazi. Hata hivyo, redio haiwezi kufanya kazi bila betri. Hali kadhalika, redio ambayo imeondolewa kwenye umeme haiwezi kufanya kazi. Vivyo hivyo, roho ni nguvu ambayo hutendesha mwili wetu. Kama umeme, roho haiwezi kuhisi wala kufikiri. Ni nguvu isiyo na utu. Lakini bila roho au kani ya uhai, “tunakata pumzi na kurudi kwenye udongo,” kama mtunga-zaburi alivyosema.
 
Andiko la Mhubiri 12:7 linasema hivi linapozungumzia kifo cha mwanadamu: “Mavumbi [mwili wake] huirudia nchi kama yalivyokuwa, nayo roho yenyewe humrudia Mungu wa kweli aliyeitoa.” Roho au kani ya uhai inapoondoka mwilini, mwili hufa na kurudi ulipotoka, yaani, kwenye udongo. Vivyo hivyo, nguvu ya uhai hurudi ilipotoka, yaani, kwa Mungu. (Ayubu 34:14, 15; Zaburi 36:9) Hiyo haimaanishi kwamba nguvu ya uhai huenda mbinguni kihalisi. Badala yake, inamaanisha kwamba mtu akifa, tumaini lolote la kuishi tena linamtegemea Yehova Mungu. Ni kana kwamba uhai wake uko mikononi mwa Mungu. Ni kupitia nguvu za Mungu tu ndipo roho au nguvu ya uhai inaweza kurudishwa ili mtu aweze kuishi tena.
 
Inafariji kama nini kujua kwamba hivyo ndivyo Mungu atakavyofanya kwa wote wanaopumzika ndani ya “makaburi ya ukumbusho!” (Yohana 5:28, 29) Wakati wa ufufuo, Yehova atamfanyizia mwili mpya yule anayelala katika kifo na kuuhuisha kwa kutia roho, au nguvu ya uhai ndani yake. Itakuwa siku ya shangwe sana.
Tafuta
Vitengo
Soma Zaidi
MAHUSIANO KIBIBLIA
KWA NINI WATU WENGI WANAUMIA BAADA YA KUINGIA KWENYE MAHUSIANO?
Kumekuwa na takwimu nyingi za wachumba na wanandoa kuumia mara tu au muda mfupi baadaye baada ya...
Kwa GOSPEL PREACHER 2021-11-06 14:52:10 0 5K
OTHERS
Jesus and Islam
Here are six questions that followers of Islam, and others, often ask about Jesus... This will...
Kwa MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-23 09:45:24 0 6K
Injili Ya Yesu Kristo
EPUKA UONGO UKIENDELEA KUTENDA DHAMBI BAADA YA KUOKOKA, HUENDI MBINGUNI KAMWE / IF YOU CONTINUE TO SIN AFTER BEING SAVED, YOU WILL NOT GO TO HEAVEN
SWAHILI: Bwana Yesu (ambaye ni Mungu mkuu na mwokozi wetu, Tito 2:13)  asifiweeee! Lengo la...
Kwa PROSPER HABONA 2022-01-16 14:16:25 0 6K
PRE-UNIT
PRE-UNIT 2
List of all of subjects for pre-unit 2 students
Kwa PROSHABO ONLINE SCHOOLS 2021-10-09 10:09:26 0 5K
GENESIS
Verse by verse explanation of Genesis 9
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 25 questions at the...
Kwa THE HOLY BIBLE 2022-01-21 03:12:04 0 5K