UTATA: NUHU WA QURAN NI TOFAUTI NA NUHU WA BIBLIA

0
5K
Ndugu Msomaji:
Siku zote Waislam huwa mnatutambia kuwa, Quran ni kitabu kilichoeleza kila kitu, ni kitabu ambacho kinajitosheleza, kitabu ambacho kimeshuka kutoka kwa Mwenyezi Mungu, na kuikandia BIBLIA, kuwa haitokanani na Mungu, sasa nitatoa aya mbili kutoka Katika BIBLIA, na kisha aya 2 kutoka ndani ya Quran, kisha nitawauliza swali,
 
GHARIKA ILITOKEA LINI KUTOKANA NA BIBLIA:Mwanzo 7:6 Naye Nuhu alikuwa mtu wa miaka mia sita hapo hiyo gharika ya maji ilipokuwa juu ya nchi.
BIBLIA ambayo mnasema haitokani na Mungu, imesema kuwa, Nuhu, alikuwa ni mwenye Umri wa miaka mia sita (600) GHARIKA lilipotokea, pia ikaeleza miaka ya NUHU baada ya Gharika.
Mwanzo 9:28 Na Nuhu akaishi baada ya ile gharika miaka mia tatu na hamsini.
 
NUHU ALIKUFA NA MIAKA MINGAPI?29 Siku zote za Nuhu zilikuwa miaka mia kenda na hamsini, akafa.
Tunaambiwa na BIBLIA kuwa, Nuhu aliishi miaka mia tatu na hamsini (350) baada ya gharika ya maji, akafa akiwa na miaka mia tisa na hamsini (950) HIYO NDIYO MIAKA ya maisha yote ya NUHU hakuishi zaidi ya miaka hiyo, sasa twende Quran kisha niulize swali.
 
GHARIKA ILITOKEA LINI KUTOKANA NA QURAN?Quran 29 وَلَقَدْ أَرْسَلْنَا نُوحًا إِلَى قَوْمِهِ فَلَبِثَ فِيهِمْ أَلْفَ سَنَةٍ إِلَّا خَمْسِينَ عَامًا فَأَخَذَهُمُ الطُّوفَانُ وَهُمْ ظَالِمُون
َ14. Na bila shaka tulimpeleka Nuhu kwa watu wake na akakaa nao miaka elfu kasoro miaka hamsini, basi mafuriko yakawaangamiza hali walikuwa madhalimu.

فَأَنجَيْنَاهُ وَأَصْحَابَ السَّفِينَةِ وَجَعَلْنَاهَا آيَةً لِّلْعَالَمِين
َ15. Na tukamuokoa yeye na watu wa (ndani ya ) safina, na tukaifanya (iwe mazingatio kwa walimwengu).
 
MADA KAMILI:BIBLIA imesema, Gharika limetokea Nuhu akiwa na miaka 600 Quran inasema, Gharika la Nuhu limetokea akiwa na miaka 950, sawa na miaka ya kufa kwa Nuhu, kwa mujibu wa BIBLIA, Biblia imesema, Nuhu akaishi miaka 350 baada ya Gharika, akafa na miaka 950 sawa na miaka ya gharika la Nuhu wa Ndani wa Quran.
 
MASWALI:-
1. Kwa kuwa ndani ya Quran, Nuhu alikuwa na miaka 950 Ndipo gharika likaja, na Biblia imesema ni miaka 600 gharika lilipokuja, na akafa akiwa na miaka 950 Sasa kwa mujibu wa Quran, Nuhu aliishi miaka mingapi kutoka katika Miaka hiyo 950 ya gharika?
2. au alikufa mwaka huo huo wa Gharika, akiwa na miaka hiyo 950 tuliyoambiwa alikuwa nayo wakati wa gharika ndani ya Quran?
 
NB. Majibu yatokane na Quran, tu kitabu ambacho mnatuambia ni cha Mungu, kama hakijitoshelezi, semeni, niwape ruhusa mtumie hata magazeti, na majarida.
 
Imeratibiwa na Abel Suleiman Shiliwa
Căutare
Categorii
Citeste mai mult
Injili Ya Yesu Kristo
MAZINGIRA HATARAISHI YA KUEPUKA KATIKA KUFANYA KAZI NA ROHO MTAKATIFU
Roho Mtakatifu, kwa nafsi na nafasi yake ameletwa ili AKAE nasi...
By GOSPEL PREACHER 2021-11-23 12:53:48 0 5K
MASWALI & MAJIBU
Hamjui Ya Kuwa Mtawahukumu Malaika? Ina Maana Gani?
Biblia inaposema hamjui ya kuwa mtawahukumu malaika? ” Swali ni Je! sisi tutawahukumu vipi...
By GOSPEL PREACHER 2022-06-13 08:51:05 0 6K
SPIRITUAL EDUCATION
AGANO LA AMANI ISAYA 54:10,EZEKIEL 34:25
PASIPO AGONO LA AMANI YA KRISTO HAPANA MAFANIKIO
By Martin Laizer 2023-09-25 15:12:47 0 11K
Injili Ya Yesu Kristo
HAYA NDIYO MADHARA YA KUABUDU PICHA ZA WATU WALIOIGIZA SINEMA ZA YESU!
BWANA YESU ASIFIWE watu wote wa mataifa yote, YESU anawapenda na pia MUNGU anawapenda na ROHO...
By GOSPEL PREACHER 2021-11-19 05:44:36 0 6K
Injili Ya Yesu Kristo
YESU NDIE NJIA NA KWELI NA UZIMA. Kumbe Dini sio Njia
Katika Biblia tunasoma kuwa Yesu anasema yeye ndie "KWELI" na anaendelea kusema kuwa KWELI ndiyo...
By MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-23 08:34:15 0 6K