UTATA: NUHU WA QURAN NI TOFAUTI NA NUHU WA BIBLIA

0
5K
Ndugu Msomaji:
Siku zote Waislam huwa mnatutambia kuwa, Quran ni kitabu kilichoeleza kila kitu, ni kitabu ambacho kinajitosheleza, kitabu ambacho kimeshuka kutoka kwa Mwenyezi Mungu, na kuikandia BIBLIA, kuwa haitokanani na Mungu, sasa nitatoa aya mbili kutoka Katika BIBLIA, na kisha aya 2 kutoka ndani ya Quran, kisha nitawauliza swali,
 
GHARIKA ILITOKEA LINI KUTOKANA NA BIBLIA:Mwanzo 7:6 Naye Nuhu alikuwa mtu wa miaka mia sita hapo hiyo gharika ya maji ilipokuwa juu ya nchi.
BIBLIA ambayo mnasema haitokani na Mungu, imesema kuwa, Nuhu, alikuwa ni mwenye Umri wa miaka mia sita (600) GHARIKA lilipotokea, pia ikaeleza miaka ya NUHU baada ya Gharika.
Mwanzo 9:28 Na Nuhu akaishi baada ya ile gharika miaka mia tatu na hamsini.
 
NUHU ALIKUFA NA MIAKA MINGAPI?29 Siku zote za Nuhu zilikuwa miaka mia kenda na hamsini, akafa.
Tunaambiwa na BIBLIA kuwa, Nuhu aliishi miaka mia tatu na hamsini (350) baada ya gharika ya maji, akafa akiwa na miaka mia tisa na hamsini (950) HIYO NDIYO MIAKA ya maisha yote ya NUHU hakuishi zaidi ya miaka hiyo, sasa twende Quran kisha niulize swali.
 
GHARIKA ILITOKEA LINI KUTOKANA NA QURAN?Quran 29 وَلَقَدْ أَرْسَلْنَا نُوحًا إِلَى قَوْمِهِ فَلَبِثَ فِيهِمْ أَلْفَ سَنَةٍ إِلَّا خَمْسِينَ عَامًا فَأَخَذَهُمُ الطُّوفَانُ وَهُمْ ظَالِمُون
َ14. Na bila shaka tulimpeleka Nuhu kwa watu wake na akakaa nao miaka elfu kasoro miaka hamsini, basi mafuriko yakawaangamiza hali walikuwa madhalimu.

فَأَنجَيْنَاهُ وَأَصْحَابَ السَّفِينَةِ وَجَعَلْنَاهَا آيَةً لِّلْعَالَمِين
َ15. Na tukamuokoa yeye na watu wa (ndani ya ) safina, na tukaifanya (iwe mazingatio kwa walimwengu).
 
MADA KAMILI:BIBLIA imesema, Gharika limetokea Nuhu akiwa na miaka 600 Quran inasema, Gharika la Nuhu limetokea akiwa na miaka 950, sawa na miaka ya kufa kwa Nuhu, kwa mujibu wa BIBLIA, Biblia imesema, Nuhu akaishi miaka 350 baada ya Gharika, akafa na miaka 950 sawa na miaka ya gharika la Nuhu wa Ndani wa Quran.
 
MASWALI:-
1. Kwa kuwa ndani ya Quran, Nuhu alikuwa na miaka 950 Ndipo gharika likaja, na Biblia imesema ni miaka 600 gharika lilipokuja, na akafa akiwa na miaka 950 Sasa kwa mujibu wa Quran, Nuhu aliishi miaka mingapi kutoka katika Miaka hiyo 950 ya gharika?
2. au alikufa mwaka huo huo wa Gharika, akiwa na miaka hiyo 950 tuliyoambiwa alikuwa nayo wakati wa gharika ndani ya Quran?
 
NB. Majibu yatokane na Quran, tu kitabu ambacho mnatuambia ni cha Mungu, kama hakijitoshelezi, semeni, niwape ruhusa mtumie hata magazeti, na majarida.
 
Imeratibiwa na Abel Suleiman Shiliwa
Tafuta
Vitengo
Soma Zaidi
UCHUMBA KIBIBLIA
KANUNI 10 ZA UCHUMBA WENYE KUFANIKIWA
KwanzaWewe na mwenzako mnaweza kuwa na sifa nyingi kama wachumba. Huenda mkijitazama na watu...
Kwa GOSPEL PREACHER 2021-11-06 10:32:02 0 6K
SPIRITUAL EDUCATION
BINTI YA KUHANI YE YOTE ATAKAPOJITIA UNAJISI KWA UKAHABA
BINTI YA KUHANI YE YOTE ATAKAPOJITIA UNAJISI KWA UKAHABA
Kwa Martin Laizer 2024-01-07 15:03:27 0 6K
OTHERS
KWANINI MUNGU HUBARIKI MATAIFA YANAYOIBARIKI ISRAELI?
Taifa la Israeli pamoja na mji wake mtakatifu wa Yerusalemu, kimsingi ndio unaoshika funguo za...
Kwa MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-24 22:37:50 0 5K
OTHERS
Isaac (Christian) or Ishmael (Islam)
Bible = Genesis 17:18,19 “And Abraham said unto God, O that Ishmael might live before thee!...
Kwa MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-24 06:23:35 0 5K
LEVITICUS
Verse by verse explanation of Leviticus 17
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 30 questions at the...
Kwa THE HOLY BIBLE 2022-01-24 10:18:20 0 6K