UTATA: NUHU WA QURAN NI TOFAUTI NA NUHU WA BIBLIA

0
5KB
Ndugu Msomaji:
Siku zote Waislam huwa mnatutambia kuwa, Quran ni kitabu kilichoeleza kila kitu, ni kitabu ambacho kinajitosheleza, kitabu ambacho kimeshuka kutoka kwa Mwenyezi Mungu, na kuikandia BIBLIA, kuwa haitokanani na Mungu, sasa nitatoa aya mbili kutoka Katika BIBLIA, na kisha aya 2 kutoka ndani ya Quran, kisha nitawauliza swali,
 
GHARIKA ILITOKEA LINI KUTOKANA NA BIBLIA:Mwanzo 7:6 Naye Nuhu alikuwa mtu wa miaka mia sita hapo hiyo gharika ya maji ilipokuwa juu ya nchi.
BIBLIA ambayo mnasema haitokani na Mungu, imesema kuwa, Nuhu, alikuwa ni mwenye Umri wa miaka mia sita (600) GHARIKA lilipotokea, pia ikaeleza miaka ya NUHU baada ya Gharika.
Mwanzo 9:28 Na Nuhu akaishi baada ya ile gharika miaka mia tatu na hamsini.
 
NUHU ALIKUFA NA MIAKA MINGAPI?29 Siku zote za Nuhu zilikuwa miaka mia kenda na hamsini, akafa.
Tunaambiwa na BIBLIA kuwa, Nuhu aliishi miaka mia tatu na hamsini (350) baada ya gharika ya maji, akafa akiwa na miaka mia tisa na hamsini (950) HIYO NDIYO MIAKA ya maisha yote ya NUHU hakuishi zaidi ya miaka hiyo, sasa twende Quran kisha niulize swali.
 
GHARIKA ILITOKEA LINI KUTOKANA NA QURAN?Quran 29 وَلَقَدْ أَرْسَلْنَا نُوحًا إِلَى قَوْمِهِ فَلَبِثَ فِيهِمْ أَلْفَ سَنَةٍ إِلَّا خَمْسِينَ عَامًا فَأَخَذَهُمُ الطُّوفَانُ وَهُمْ ظَالِمُون
َ14. Na bila shaka tulimpeleka Nuhu kwa watu wake na akakaa nao miaka elfu kasoro miaka hamsini, basi mafuriko yakawaangamiza hali walikuwa madhalimu.

فَأَنجَيْنَاهُ وَأَصْحَابَ السَّفِينَةِ وَجَعَلْنَاهَا آيَةً لِّلْعَالَمِين
َ15. Na tukamuokoa yeye na watu wa (ndani ya ) safina, na tukaifanya (iwe mazingatio kwa walimwengu).
 
MADA KAMILI:BIBLIA imesema, Gharika limetokea Nuhu akiwa na miaka 600 Quran inasema, Gharika la Nuhu limetokea akiwa na miaka 950, sawa na miaka ya kufa kwa Nuhu, kwa mujibu wa BIBLIA, Biblia imesema, Nuhu akaishi miaka 350 baada ya Gharika, akafa na miaka 950 sawa na miaka ya gharika la Nuhu wa Ndani wa Quran.
 
MASWALI:-
1. Kwa kuwa ndani ya Quran, Nuhu alikuwa na miaka 950 Ndipo gharika likaja, na Biblia imesema ni miaka 600 gharika lilipokuja, na akafa akiwa na miaka 950 Sasa kwa mujibu wa Quran, Nuhu aliishi miaka mingapi kutoka katika Miaka hiyo 950 ya gharika?
2. au alikufa mwaka huo huo wa Gharika, akiwa na miaka hiyo 950 tuliyoambiwa alikuwa nayo wakati wa gharika ndani ya Quran?
 
NB. Majibu yatokane na Quran, tu kitabu ambacho mnatuambia ni cha Mungu, kama hakijitoshelezi, semeni, niwape ruhusa mtumie hata magazeti, na majarida.
 
Imeratibiwa na Abel Suleiman Shiliwa
Rechercher
Catégories
Lire la suite
OTHERS
UTHIBITISHO 12 KUWA ALLAH SIO MUNGU
  Leo nitawapa Sababu 12 kwanini allah sio mungu. 1. ALLAH NI MUNGU ASIYE NA JINA...
Par MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-22 03:12:48 0 5KB
JOB
Verse by verse explanation of Job 15
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 26 questions at the...
Par THE HOLY BIBLE 2022-04-03 03:27:40 0 5KB
TANZANIA
PROSHABO ONLINE SCHOOL
WELCOME TO PROSHABO ONLINE SCHOOL Please select which class are you? CHEKECHEA CHEKECHEA 1...
Par PROSHABO ONLINE SCHOOLS 2021-10-09 10:05:17 0 6KB
SPIRITUAL EDUCATION
USIUZE URIDHI WAKO ULIOKABIDHIWA KWA GHARAMA KUBWA MWANZO 25:27-34
USIUZE URIDHI WAKO ULIOKABIDHIWA KWA GHARAMA KUBWA MWANZO 25:27-34
Par Martin Laizer 2023-11-17 16:07:34 0 13KB
OTHERS
SABABU 10 KWANINI USIZINI.
1. Uzinzi ni dhambi pekee inayotajwa kama "UBAYA MKUBWA". Haimaanishi kwamba dhambi...
Par PROSPER HABONA 2026-01-15 11:29:42 0 866