ETI ALLAH AMEKUBALI KUTOA USHAIDI KWA VIUMBE VYAKE?

0
5كيلو بايت

Je, nani atakuwa Hakimu wakati Allah anatoa Ushaidi?

NDUGU WASOMAJI, Hivi Allah anaweza kuwa shaidi wakati yeye ndie anadai kuwa alitoa Utume kwa Muhammad? Hivi Mungu anaweza kwenda kutoa Ushaidi kwa viumbe vyake? Nani atakuwa Hakimu wa hiyo Kesi?

Katika hii aya hapa chini, mhukumiwa ni Allah aliyedai katoa Utume kwa Muhammad, kivipi na tokea lini Mhukumiwa akawa shaidi katika Kesi yake ya jinai?

Quran 4:72 Surat Annisa inasema "wema uliokufikia unatoka kwa Mwenyenzi Mungu na baya lililokufikia linatoka nafsini mwako nasi tumekupeleka kwa watu kuwa Mtume na Mwenyenzi Mungu ni shahid wa kutosha wala hapaitajiwa shaid mwingine ila yeye"

Allah anadai kuwa yeye ndie aliye mpa Utume Muhammad na hapo hapo ALLAH anajihami kuwa mkibisha na au kuwa na shaka na utume wa Muhammad basi yeye ni Shaidi yake. Hivi, MFANO: Rais akimpa Mtu uwaziri, umesha wai sikia Rais anajihami kwa kusema kama wakikukataa mimi nitakuwa Shaidi yako? Kwani Allah ana mshindani mpaka atoe maneno ya kujihami? Je, Allah ni Mungu? Mbona anakubali kuchukia nafasi ya chini ya kuwa Shaidi kwa viumbe vyake? Au kuna Mungu mwingine ambaye ni zaidi ya Allah ndio maana Allah anajihami kwa kusema yeye atakuwa shaidi wa Muhammad?

Ndugu zanguni, tukisoma Biblia, hakuna hata sehemue moja na au aya yeyote ile inayo sema kuwa Yehovah alijihami kwa Mitume wake kuwa, kama wakikataliwa basi Yehovah atakuwa shaidi yao. Allah anadai kuwa yeye ni shaidi lakini ameshindwa kutuambia wapi hiyo kesi itakuwa na nani ni Hakimu!

Binadamu/Sisi labda ndio tunaweza kuwa Mashaidi wa Neno la Mungu lakini si Mungu mwenye Mamlaka yote awe shaid katika viumbe vyake na neno lake. Mungu huwa halizimishi mambo kama Allah wa Uislam. Yesu anasema kuwa yeye Ndie Mwanzo na Mwisho, Alfa na Omega. Hakuna zaidi yake, lakini Allah amekiri kuwa yeye anaweza kuwa shaidi pale mambo yanapokuwa magumu. Hakika Allah hana Mamlaka yeyote yake, ndio maana yeye ni shaidi na sio Mungu mwenye Mamlaka. Sijui nani atakuwa Hakimu wakati Allah amesimama kutoa Ushaidi?

البحث
الأقسام
إقرأ المزيد
OTHERS
UTATA KATIKA UUMBAJI WA MAJINI
ALLAH: UTATA KATIKA UUMBAJI WA MAJINIJe, Majini yaliumbwaje?Leo hii tutajifunza UTATA wa Allah...
بواسطة MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-23 08:20:08 0 5كيلو بايت
Injili Ya Yesu Kristo
Why did Jesus have to die?
When we ask a question such as this, we must be careful that we are not calling God into...
بواسطة MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-23 10:39:49 0 6كيلو بايت
Injili Ya Yesu Kristo
MJUE MWIGIZAJI WA FILAMU YA YESU AMBAYE BAADHI YA WATU HUDHANI KWAMBA NI YESU.
BRIAN DEACON ndio jina lake mwigizaji huyo ambaye ni mwingereza aliyezaliwa mnamo tarehe...
بواسطة GOSPEL PREACHER 2021-11-19 05:33:52 0 5كيلو بايت
OTHERS
JE, WAGANGA WA KIENYEJI WANAWEZA KUKUPA ULINZI NA MAFANIKIO KATIKA MAISHA YAKO?
Naamini umeshasikia mara kadhaa watu wakitaja kile kinachoitwa “sayansi ya kiafrika”....
بواسطة MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-24 22:19:31 0 6كيلو بايت
NUMBERS
Verse by verse explanation of Numbers 36
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 15 questions at the...
بواسطة THE HOLY BIBLE 2022-01-24 15:40:17 0 6كيلو بايت