ETI ALLAH AMEKUBALI KUTOA USHAIDI KWA VIUMBE VYAKE?

0
5K

Je, nani atakuwa Hakimu wakati Allah anatoa Ushaidi?

NDUGU WASOMAJI, Hivi Allah anaweza kuwa shaidi wakati yeye ndie anadai kuwa alitoa Utume kwa Muhammad? Hivi Mungu anaweza kwenda kutoa Ushaidi kwa viumbe vyake? Nani atakuwa Hakimu wa hiyo Kesi?

Katika hii aya hapa chini, mhukumiwa ni Allah aliyedai katoa Utume kwa Muhammad, kivipi na tokea lini Mhukumiwa akawa shaidi katika Kesi yake ya jinai?

Quran 4:72 Surat Annisa inasema "wema uliokufikia unatoka kwa Mwenyenzi Mungu na baya lililokufikia linatoka nafsini mwako nasi tumekupeleka kwa watu kuwa Mtume na Mwenyenzi Mungu ni shahid wa kutosha wala hapaitajiwa shaid mwingine ila yeye"

Allah anadai kuwa yeye ndie aliye mpa Utume Muhammad na hapo hapo ALLAH anajihami kuwa mkibisha na au kuwa na shaka na utume wa Muhammad basi yeye ni Shaidi yake. Hivi, MFANO: Rais akimpa Mtu uwaziri, umesha wai sikia Rais anajihami kwa kusema kama wakikukataa mimi nitakuwa Shaidi yako? Kwani Allah ana mshindani mpaka atoe maneno ya kujihami? Je, Allah ni Mungu? Mbona anakubali kuchukia nafasi ya chini ya kuwa Shaidi kwa viumbe vyake? Au kuna Mungu mwingine ambaye ni zaidi ya Allah ndio maana Allah anajihami kwa kusema yeye atakuwa shaidi wa Muhammad?

Ndugu zanguni, tukisoma Biblia, hakuna hata sehemue moja na au aya yeyote ile inayo sema kuwa Yehovah alijihami kwa Mitume wake kuwa, kama wakikataliwa basi Yehovah atakuwa shaidi yao. Allah anadai kuwa yeye ni shaidi lakini ameshindwa kutuambia wapi hiyo kesi itakuwa na nani ni Hakimu!

Binadamu/Sisi labda ndio tunaweza kuwa Mashaidi wa Neno la Mungu lakini si Mungu mwenye Mamlaka yote awe shaid katika viumbe vyake na neno lake. Mungu huwa halizimishi mambo kama Allah wa Uislam. Yesu anasema kuwa yeye Ndie Mwanzo na Mwisho, Alfa na Omega. Hakuna zaidi yake, lakini Allah amekiri kuwa yeye anaweza kuwa shaidi pale mambo yanapokuwa magumu. Hakika Allah hana Mamlaka yeyote yake, ndio maana yeye ni shaidi na sio Mungu mwenye Mamlaka. Sijui nani atakuwa Hakimu wakati Allah amesimama kutoa Ushaidi?

Cerca
Categorie
Leggi tutto
JOSHUA
Verse by verse explanation of Joshua 3
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 22 questions at the...
By THE HOLY BIBLE 2022-01-25 07:16:08 0 5K
Injili Ya Yesu Kristo
NAFASI YA MAWAZO KATIKA KUVIPIGA VITA VYA KIROHO
Vita vya kiroho, ni vita ambayo inapigwa katika ulimwengu wa roho, kwa jinsi ya rohoni baina ya...
By GOSPEL PREACHER 2021-11-23 12:28:21 2 5K
2 CHRONICLES
Verse by verse explanation of 2 Chronicles 9
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 30 questions at the...
By THE HOLY BIBLE 2022-04-01 22:11:52 0 5K
Networking
Three reasons why marketplaces fail (and how not to)
This article discusses the three most common pitfalls for peer-to-peer marketplaces and outlines...
By Business Academy 2022-09-17 02:24:59 0 6K
Injili Ya Yesu Kristo
NAFASI YAKO NI MUHIMU SANA KATIKA KUUJENGA MWILI WA KRISTO
Biblia katika 1 Wakorinto 12:11-14,18 imeandikwa ‘Lakini kazi hizi zote huzitenda Roho huyo...
By GOSPEL PREACHER 2021-11-23 12:30:00 0 5K