JINSI YA KUENENDA KWA ROHO.

0
6K

Wagalatia 5:16 “Basi, nasema enendeni kwa Roho, wala hamtatimiza kamwe tamaa za mwili”Hapa tunaona Paulo anawaagiza wagalatia kwamba waenende kwa Roho na lengo kubwa ni ili wasizitimize tama za mwili.

Lengo la waraka huu mfupi ni kukueleza namna unavyoweza kuenenda kwa Roho, na hii ni kwa sababu Yesu  mwenyewe alisema ni heri mimi niondokeili aje mwingine msaidizi huyo Roho wa kweli. Na
kama tunaye Roho mtakatifu ni lazima tujue ni kwa namna gani tutaenenda kwa roho?Neno la Mungu/ Mungu anaposema, enendeni kwa Roho ana maana hii:- 

(a)            Kila unalolizungumza, lizungumze chini ya uongozi wa Roho mtakatifu. Yohana 12:49-50. Yesu mwenyewe hakunena neno lolote kwa shauri lake, bali kila ambalo baba alimwambia kupitia Roho mtakatifu. Hivyo hata wewe
kama unafundisha, unahubiri, unaonya hakikisha unachokisema Roho mtakatifu ndiye amekuruhusu ukiseme. Usiseme kitu cha kwako halafu ukasema Roho mtakatifu amekuongoza.

(b)            Tii uongozi wake .Yohana 16:13 “ lakini atakapokuja huyo Roho wa kweli; atawaongoza awatie kwenye kweli yote…….” Moja ya kazi za Roho mtakatifu ni kutuongoza na kututia kwenye kweli yote. Hivyo kuenenda kwa Roho maana yake ni kutii katika yale anayotuambia maana hata yeye haneni kwa ridhaa yake isipokuwa yale anayoyasikia kutoka kwa Mungu. 

(c)             Jifunze kuyafikiri mambo ya Roho wa Mungu. Warumi 8:5b “
Bali wale waifuatao roho huyafikiri mambo ya roho”Kuenenda kwa roho kunajumuisha kukaa chini na kuanza kutafakari mambo/kazi za Roho mtakatifu. Vile jinsi utendaji wake ulivyo, karama zake, vipawa, tunda la Roho na vile jinsi anavyofanyika msaidizi katika maisha yako.

(d) Kuliishi tunda la Roho.Wagalatia 5:22 “lakini tunda la Roho ni upendo, Furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu, upole na kiasi………”Sikiliza ukijifunza au kadri unavyoishi maisha yaliyojaa upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu, upole na kiasi ndivyo unavyokuwa umejiweka kwenye mkao wa kuongozwa na Roho au ndiko kunaitwa kuenenda kwa Roho. 

 (e) Kwa kuyakataa na kuyafisha/vunja matendo ya mwili katika maisha yako. Wagalatia 4:28-31 ule mstari wa 30 unasema” Lakini lasemaje andiko? Mfukuze mjakazi na mwanawe kwa maana mwana wa mjakazi hatarithi kabisa pamoja na mwana wa muungwana”Biblia inapozungumzia kumfukuza mjakazi pamoja na mwanawe ina maana ya kuyafukuza, kuyapinga, kuyaondoa, kuyafisha, kuyaharibu matendo ya mwili katika maisha yako ambayo yametajwa katika. Wagalatia 5:19-21 ikiwa ni pamoja na uasherati, ulevi, husuda, uadui, ugomvi, uchafu, ufisadi nk.Naamini baada ya ujumbe huu utaanza kuenenda kwa Roho na kuomba msaada wa Mungu katika maisha yako kwenye eneo hili..

Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo na iwe pamoja nawe.

Cerca
Categorie
Leggi tutto
1 CHRONICLES
Verse by verse explanation of 1 Chronicles 16
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 33 questions at the...
By THE HOLY BIBLE 2022-03-20 05:00:28 0 6K
OTHERS
THERE IS A GOD How the World’s Most Notorious Atheist Changed His Mind
In the parable of the lost sheep, in the Gospel of Luke, Jesus says there shall be more joy in...
By MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-23 10:00:09 0 6K
SPIRITUAL EDUCATION
What are fallen angels?
Angels are created beings used by God as messengers, warriors, and servants. The word "angel"...
By MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-24 05:55:44 0 5K
NDOA KIBIBLIA
JE, UNAJUA HIYO NDOA UNAYOTAKA KUINGIA INAKUPELEKA WAPI?
Mtumishi, ninachohitaji sasa ni mume tu, umri unazidi kwenda na nimeomba ila sioni nikijibiwa,...
By GOSPEL PREACHER 2021-11-19 08:00:54 0 6K
OTHERS
God of the Bible is "FATHER", In Contrast, Allah of Koran is Not "FATHER"
SCRIPTURES THAT SHOW THAT GOD IS A FATHER Let’s take a look at the groundwork that Judaism...
By MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-23 08:34:59 0 5K