KANUNI YA MUDA KATIKA MAHUSIANO

0
5K

Muda hupima upendo wangu kwako.
Kama kweli nakupenda, nita tumia kiasi kikubwa cha Muda wangu kwa ajili yako! Kama nakunyima Muda wangu kila siku ni kwa sababu tu sikupendi. Inawezekanaje nikawa nakupenda wakati sina Muda na wewe? Muda ndiyo maisha yangu. Ninapotoa Muda wangu ninayatoa maisha yangu. Kwa nini? Maisha ya mtu yamefungwa ktk Muda wake, Muda wa mtu unajenga maisha yake.

Sasa ninapozungumzia Muda ninamaanisha Muda kwa ajili yake na si kwa ajili yako. Kama unatafuta Muda wa kuwa naye kwa ajili ya kutimiza matakwa yako na si kwa ajili yake (mwenzi wako) basi huo si dhabihu itakayojenga mahusiano yenu. Toa Muda wako kwa ajili ya Furaha yake kwanza. Furaha yake ndiyo Furaha yako. Kwanza yeye kisha wewe. Mpe Muda wako, Mpe maisha yako. Unaposhiriki Muda wako na umpendaye unashiriki maisha yako na umpendaye

UPENDO ni gharama, na gharama Inaanza na Muda wako kwa ajili yake. Ukiona huwezi kuutoa Muda wako kwa ajili yake jua umeshindwa kumpenda! Unayempenda utashiri naye Muda wako.

NINASHIRIKI VIPI MUDA WANGU NA MWENZI WANGU?

  1. Tumia Muda wako kumjulia hali na maendeleo yake; ukiwa mbali tumia simu yako, ukiwa karibu kaa naye, taka kujua taarifa zake alipokuwa mbali na wewe. Usiwe na haraka ya kuondoka wala usiwe bize na kitu kingine. Mwangalie usoni unapozungumza naye.
  2. Msikilize, onyesha unajali anachozungumza, onyesha kuwa unamsikia kwa kutikisa kichwa au kuitikia na Umwangalie anapokuwa anazungumza, kwa wanandoa unaweza kuwa umemshika au kumkumbatia wakati anapokuwa anazungumza au waweza kumlalia kifuani, begani au mapajani.
  3. Kula naye matunda ya kazi yako; Mpe sehemu ya unachopata kazini! Mletee zawadi itokanayo na matunda ya kazi yako.
  4. Kula naye chakula, ndani na nje ya nyumbani. Kama unauwezo wa kutoka 'out' na mwenzi wako si kwa sababu kuna kitu unakihitaji toka kwakwe bali kwa sababu unampenda na unataka afurahi basi mtoe
  5. Msifie, mfariji na umtie moyo. Kama kuna jambo la kumshukuru, basi, mshukuru kwa namna maalumu na kama kuna jambo ulimkosea basi maombi msamaha kwa uaminifu na unyenyekevu wote.


Fanya yote kana kwamba hautapata fursa nyingine tena, ni dhabihu ya maisha yako kwa mwenzi wako wa pekee asiye na mbadala

Site içinde arama yapın
Kategoriler
Read More
JOB
Verse by verse explanation of Job 24
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 25 questions at the...
By THE HOLY BIBLE 2022-04-03 03:55:26 0 5K
OTHERS
Kutoka Kwenye Uislamu Hadi Kwenye Ukristo
Jina langu ni Tahir na hii ni safari yangu kutoka kwenye Uislamu hadi kwenye Ukristo. Mara baada...
By MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-22 04:07:45 0 5K
HOLY BIBLE
Is Hell Eternal?
The teaching that there is an eternal hell in which hordes of mankind will suffer eternal...
By MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-24 05:53:52 1 6K
OTHERS
KUMBE KORAN HAIKUTEREMSHWA KUTOKA KWA ALLAH
Ni Nani Walikuwa Waandishi Wa Quran Tukufu Wakati Wa Mtume Muhammad? Je, ungependa kuwafahamu...
By MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-22 18:29:28 0 5K
HOLY BIBLE
Did Jesus go to hell between His death and resurrection?
There is a great deal of confusion in regards to this question. This concept comes primarily...
By MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-24 04:22:21 0 5K