KANUNI YA MUDA KATIKA MAHUSIANO

0
5K

Muda hupima upendo wangu kwako.
Kama kweli nakupenda, nita tumia kiasi kikubwa cha Muda wangu kwa ajili yako! Kama nakunyima Muda wangu kila siku ni kwa sababu tu sikupendi. Inawezekanaje nikawa nakupenda wakati sina Muda na wewe? Muda ndiyo maisha yangu. Ninapotoa Muda wangu ninayatoa maisha yangu. Kwa nini? Maisha ya mtu yamefungwa ktk Muda wake, Muda wa mtu unajenga maisha yake.

Sasa ninapozungumzia Muda ninamaanisha Muda kwa ajili yake na si kwa ajili yako. Kama unatafuta Muda wa kuwa naye kwa ajili ya kutimiza matakwa yako na si kwa ajili yake (mwenzi wako) basi huo si dhabihu itakayojenga mahusiano yenu. Toa Muda wako kwa ajili ya Furaha yake kwanza. Furaha yake ndiyo Furaha yako. Kwanza yeye kisha wewe. Mpe Muda wako, Mpe maisha yako. Unaposhiriki Muda wako na umpendaye unashiriki maisha yako na umpendaye

UPENDO ni gharama, na gharama Inaanza na Muda wako kwa ajili yake. Ukiona huwezi kuutoa Muda wako kwa ajili yake jua umeshindwa kumpenda! Unayempenda utashiri naye Muda wako.

NINASHIRIKI VIPI MUDA WANGU NA MWENZI WANGU?

  1. Tumia Muda wako kumjulia hali na maendeleo yake; ukiwa mbali tumia simu yako, ukiwa karibu kaa naye, taka kujua taarifa zake alipokuwa mbali na wewe. Usiwe na haraka ya kuondoka wala usiwe bize na kitu kingine. Mwangalie usoni unapozungumza naye.
  2. Msikilize, onyesha unajali anachozungumza, onyesha kuwa unamsikia kwa kutikisa kichwa au kuitikia na Umwangalie anapokuwa anazungumza, kwa wanandoa unaweza kuwa umemshika au kumkumbatia wakati anapokuwa anazungumza au waweza kumlalia kifuani, begani au mapajani.
  3. Kula naye matunda ya kazi yako; Mpe sehemu ya unachopata kazini! Mletee zawadi itokanayo na matunda ya kazi yako.
  4. Kula naye chakula, ndani na nje ya nyumbani. Kama unauwezo wa kutoka 'out' na mwenzi wako si kwa sababu kuna kitu unakihitaji toka kwakwe bali kwa sababu unampenda na unataka afurahi basi mtoe
  5. Msifie, mfariji na umtie moyo. Kama kuna jambo la kumshukuru, basi, mshukuru kwa namna maalumu na kama kuna jambo ulimkosea basi maombi msamaha kwa uaminifu na unyenyekevu wote.


Fanya yote kana kwamba hautapata fursa nyingine tena, ni dhabihu ya maisha yako kwa mwenzi wako wa pekee asiye na mbadala

Cerca
Categorie
Leggi tutto
JUDGES
Verse by verse explanation of Judges 21
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 26 questions at the...
By THE HOLY BIBLE 2022-01-25 11:18:55 0 6K
Injili Ya Yesu Kristo
MAZINGIRA HATARAISHI YA KUEPUKA KATIKA KUFANYA KAZI NA ROHO MTAKATIFU
Roho Mtakatifu, kwa nafsi na nafasi yake ameletwa ili AKAE nasi...
By GOSPEL PREACHER 2021-11-23 12:53:48 0 5K
NUMBERS
Book of Numbers Explained
Introduction: Something went terribly wrong on the way to the Promised land. Why would it...
By THE HOLY BIBLE 2022-01-24 14:00:03 0 5K
REVELATION
UFUNUO 20
Bwana wetu YESU KRISTO apewe sifa, karibu katika mwendelezo wa kitabu cha ufunuo, leo tukiwa...
By GOSPEL PREACHER 2021-10-30 12:40:40 0 6K
CERTIFICATE
CERTIFICATE
List of all subjects for the students who are taking certificate courses.
By PROSHABO ONLINE SCHOOLS 2021-10-09 10:45:31 0 5K