MAANA HALISI YA IBADA YA KWELI

0
687

MAANA HALISI YA IBADA KWA UJUMLA. EBR 10:25

Ibada ni tendo la heshima ya hali ya juu linalotolewa kwa Mungu au kwa kitu kinachoheshimiwa kama mungu. Ni kitendo cha kuonyesha unyenyekevu, utiifu, shukrani, na utukufu kwa moyo wote.

KATIKA MUKTADHA WA IMANI YA KIKRISTO, IBADA INAHUSISHA:

Ibada ni tendo la ndani la Kumuabudu Mungu katika Roho na kweli (Yohana 4:24)na ibada hii ya Roho na kweli hudhihirishwa mwilini kwa njia zifuatazo

- Kusifu na kuimba nyimbo za kiroho.

- Kusujudu, kufunga, kutoa sadaka, na kushiriki sakramenti kama Meza ya Bwana.

- Kujitoa kwa Mungu kwa mwili na roho—maisha yenye utakatifu ni ibada ya kila siku (Warumi 12:1).

-kukusanyika kwa pamoja kama watu wenye nia Moja Ili kumtukuza Mungu na kuyapeleka mahitaji yenu kwa pamoja kama Wana wa baba mmoja na Bwana mmoja katika Kristo Yesu (Ebrania 10:25)

KIBIBLIA, KUNA AINA KUU TATU ZA IBADA:

1. Ibada ya kweli kwa Mungu – inayotokana na Roho Mtakatifu na Neno la Mungu. Yohana 4:23-24, Nehemiah 9:3,Luka 24:50-53.

2. Ibada kwa shetani – kwa njia ya ushirikina au uchawi. Isaya 47:10-14,Warumi 1:25, Yeremia 10:14,2:11,16 :20, Zaburi 115:4-7, Ufunuo 9:20-21.

3. Ibada za wanadamu walizojitungia – ambazo hazina msingi wa maandiko. Mathayo 15:1-9

 Neno "ibada" linatokana na Kiarabu عبادة (ibadah), likiwa na mizizi ya maana ya "utumwa" au "kujitoa kwa unyenyekevu" kwa Mungu.

 Kwasababu hiyo Ibada ni tendo la kiroho linalounganisha Ulimwengu wa mwili na Ulimwengu wa kiroho, Ibada ni unyenyekevu wa moyo juu ya Mungu au kitu chochote unachokipa Heshima ya Hali ya juu Leo hii tunaona wakristo wengi hawafanyi Ibada ya kweli Bali wafanya ibada ya Mwilini Ili waonekane na watu zaidi sana wengi wameheshimu mambo Yao kuliko Mungu na kama tunavyojua ibada ni tendo la Heshima ya Hali ya juu sana juu ya kile unachokiamini hivyo ikiwa kazi yako inaweza kukufanya usimfanyie Mungu ibada basi ni WAZI KUWA wewe unaabudu kazi ya mikono yako na siyo Mungu, Leo hii viambatanishi kama vitambaa,maji,sabuni Keki za upako zimepewa Heshima ya Hali ya juu kuliko Mungu na jina la Yesu.

Hivyo geuka Leo mpe Yessu Maisha yako naye atakujaza Roho Mtakatifu nawe utaabudu katika Roho na kweli naye atakuongoza na kukufundisha Zaburi 32:8

BY. EV. MARTIN LAIZER.

 

Site içinde arama yapın
Kategoriler
Read More
2 SAMUEL
Verse by verse explanation of 2 Samuel 1
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 31 questions at the...
By THE HOLY BIBLE 2022-02-05 09:05:11 0 5K
Injili Ya Yesu Kristo
UMEJIAANDAJE KWA TUKIO LA UNYAKUO? (Sehemu ya 2)
Katika sehemu hii ya pili nataka tuweze kuangalia jinsi baadhi ya maandiko yanavyozungumzia tukio...
By GOSPEL PREACHER 2021-11-23 13:08:10 0 5K
DEUTERONOMY
Verse by verse explanation of Deuteronomy 3
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 33 questions at the...
By THE HOLY BIBLE 2022-01-24 19:18:47 0 5K
NDOA KIBIBLIA
SHAMBA LA MTU MVIVU, ASIYE NA AKLI: MAHUSIANO YA NDOA (NA UCHUMBA)
MAHUSIANO: SHAMBA LA MTU MVIVU, ASIYE NA AKLI(Uvivu na Kukosa Akili Kichocheo Cha...
By GOSPEL PREACHER 2021-11-07 23:23:24 0 5K
Injili Ya Yesu Kristo
MKE WA KAINI KATOKEA WAPI?
Bwana Yesu asifiwe… Kwa ufupi; Ukisoma kitabu cha Mwanzo sura 1-4,utaona Mungu akiwa na...
By GOSPEL PREACHER 2022-03-30 05:14:43 0 5K