Je! Mtu Aliyeokoka Anaruhusiwa Kumiliki Lodge Ambayo Ina Bar Ndani Yake?

0
6KB

Swali linaendelea….na kutoa fungu la kumi kwa kupitia hiyo?,kwa mfano mimi nina rafiki yangu anafanya kazi kampuni ya TBL kazi ya kampuni hii ni kutengeneza na kuuza bia kama yalivyo makampuni mengine kama Serengeti nk. Huyu ndugu ni mkristo aliyeokoka na jumapili bila shaka hutoa fungu la kumi na sadaka zingine pia ana cheo kanisani ..je! ni kuna makosa yoyote kufanya hivyo?


JIBU: Kumiliki bar ni dhambi, vilevile kumiliki lodge lenye bar ni dhambi..biblia inasema wazi katika

Kumbukumbu 23:18 “usilete ujira wa kahaba wala mshahara wa mbwa katika nyumba ya Bwana, ni machukizo”

Kumbuka na sio tu kazi ya bar tu, bali hata na kazi nyingine yoyote isiyokuwa halali mfano biashara ya madawa ya kulevya, ufisadi, ulanguzi,uuzaji pombe,wizi, kamari, uuzaji sigara n.k kamwe usijaribu kufanya hivyo ukadhani kuwa Mungu ataziridhia sadaka zako, hata kama unatoa nyingi kiasi gani au kwa moyo kiasi gani, kwa kufanya hivyo utakuwa unajichukulia laana badala ya baraka, ni machukizo mbele za BWANA, kutii ni bora kuliko dhabihu(1 Samweli 15:22) Mungu ni mtakatifu na sio mtaka-vitu.

Kwahiyo unapokwenda mbele zake ni vema kufahamu kuwa yeye ni Mtakatifu na anaihitaji roho yako sana zaidi ya vitu vyako. Kwahiyo kuhusu hiyo kazi anapaswa aache,kwasababu biblia imeturuhusu kiungo chetu kimoja kikitukosesha tuking’oe. kumiliki bar ni dhambi..Hivyo amwombe tu Mungu awe mwaminifu atampa kazi nyingine tena nzuri zaidi ya hiyo.. Mungu Alisema kuwa anajua tunayahitaji hayo yote

Mathayo 6:31 “Msisumbuke, basi, mkisema, Tule nini? Au Tunywe nini? Au Tuvae nini? 32 Kwa maana hayo yote Mataifa huyatafuta; kwa sababu Baba yenu wa mbinguni anajua ya kuwa mnahitaji hayo yote. 33 Bali utafuteni kwanza ufalme wake, na haki yake; na hayo yote mtazidishiwa. 34 Basi msisumbukie ya kesho; kwa kuwa kesho itajisumbukia yenyewe. Yatosha kwa siku maovu yake.”

Kwahiyo asiwe na wasiwasi hilo suala la baada ya kuiacha hiyo kazi atakula nini? hilo amwachie Mungu.Hivyo mshauri atafute kazi nyingine inayompa Mungu utukufu.  

Ubarikiwe sana.  

Rechercher
Catégories
Lire la suite
SPIRITUAL EDUCATION
IT IS NOT FOR THE ANOINTED
This message was given to me on the evening of  March 29, 2014 in Njombe Region after...
Par GOSPEL PREACHER 2021-11-23 07:40:43 0 5KB
JOB
Verse by verse explanation of Job 25
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 13 questions at the...
Par THE HOLY BIBLE 2022-04-03 03:56:56 0 5KB
Injili Ya Yesu Kristo
MAOMBI PEKE YAKE BILA IMANI HAYATOSHI KUTENGENEZA JIBU LA MAHITAJI YAKO.
Marko 9:14-29. Hii ni habari ya yule baba aliyekuwa na mwana mwenye pepo bubu na kiziwi, akamleta...
Par GOSPEL PREACHER 2021-11-23 12:47:11 0 4KB
REVELATION
MAJIRA YA KANISA LA FILADELFIA
(1) MLENGWA WA KANISAUFUNUO 3:7“Na kwa malaika wa kanisa lililoko Filadelfia...
Par GOSPEL PREACHER 2021-09-24 10:41:39 0 6KB
Injili Ya Yesu Kristo
USHAURI KWA MJANE WAJANE
Mpenzi msomaji katika category hii ya “maswali na majibu” huwa naandaa masomo...
Par GOSPEL PREACHER 2021-11-23 12:21:28 0 9KB