Je! Mtu Aliyeokoka Anaruhusiwa Kumiliki Lodge Ambayo Ina Bar Ndani Yake?

0
6KB

Swali linaendelea….na kutoa fungu la kumi kwa kupitia hiyo?,kwa mfano mimi nina rafiki yangu anafanya kazi kampuni ya TBL kazi ya kampuni hii ni kutengeneza na kuuza bia kama yalivyo makampuni mengine kama Serengeti nk. Huyu ndugu ni mkristo aliyeokoka na jumapili bila shaka hutoa fungu la kumi na sadaka zingine pia ana cheo kanisani ..je! ni kuna makosa yoyote kufanya hivyo?


JIBU: Kumiliki bar ni dhambi, vilevile kumiliki lodge lenye bar ni dhambi..biblia inasema wazi katika

Kumbukumbu 23:18 “usilete ujira wa kahaba wala mshahara wa mbwa katika nyumba ya Bwana, ni machukizo”

Kumbuka na sio tu kazi ya bar tu, bali hata na kazi nyingine yoyote isiyokuwa halali mfano biashara ya madawa ya kulevya, ufisadi, ulanguzi,uuzaji pombe,wizi, kamari, uuzaji sigara n.k kamwe usijaribu kufanya hivyo ukadhani kuwa Mungu ataziridhia sadaka zako, hata kama unatoa nyingi kiasi gani au kwa moyo kiasi gani, kwa kufanya hivyo utakuwa unajichukulia laana badala ya baraka, ni machukizo mbele za BWANA, kutii ni bora kuliko dhabihu(1 Samweli 15:22) Mungu ni mtakatifu na sio mtaka-vitu.

Kwahiyo unapokwenda mbele zake ni vema kufahamu kuwa yeye ni Mtakatifu na anaihitaji roho yako sana zaidi ya vitu vyako. Kwahiyo kuhusu hiyo kazi anapaswa aache,kwasababu biblia imeturuhusu kiungo chetu kimoja kikitukosesha tuking’oe. kumiliki bar ni dhambi..Hivyo amwombe tu Mungu awe mwaminifu atampa kazi nyingine tena nzuri zaidi ya hiyo.. Mungu Alisema kuwa anajua tunayahitaji hayo yote

Mathayo 6:31 “Msisumbuke, basi, mkisema, Tule nini? Au Tunywe nini? Au Tuvae nini? 32 Kwa maana hayo yote Mataifa huyatafuta; kwa sababu Baba yenu wa mbinguni anajua ya kuwa mnahitaji hayo yote. 33 Bali utafuteni kwanza ufalme wake, na haki yake; na hayo yote mtazidishiwa. 34 Basi msisumbukie ya kesho; kwa kuwa kesho itajisumbukia yenyewe. Yatosha kwa siku maovu yake.”

Kwahiyo asiwe na wasiwasi hilo suala la baada ya kuiacha hiyo kazi atakula nini? hilo amwachie Mungu.Hivyo mshauri atafute kazi nyingine inayompa Mungu utukufu.  

Ubarikiwe sana.  

Rechercher
Catégories
Lire la suite
SPIRITUAL EDUCATION
KWA MAANA KUJIZOEZA KUPATA NGUVU ZA MWILI KUNAFAA BALI ZA KIROHO ZAIDI SANA
KWA MAANA KUJIZOEZA KUPATA NGUVU ZA MWILI KUNAFAA BALI ZA KIROHO ZAIDI SANA  
Par Martin Laizer 2023-10-10 20:38:59 4 6KB
NDOA KIBIBLIA
KUISHI NA MWANAMKE ALIYEKUZIDI KIPATO, MALI AU CHEO.
Hiki ni kipindi cha hatari sana, wanawake wengi wanapigania haki sawa. Harakati za wanawake...
Par GOSPEL PREACHER 2021-11-06 12:53:27 0 5KB
GENESIS
Verse by verse explanation of Genesis 29
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 27 questions at the...
Par THE HOLY BIBLE 2022-01-21 06:42:29 0 5KB
OTHERS
UNAJUA KWANINI WAISLAM WANAMSWALIA MUHAMMAD KILA SIKU?
KWASABABU MUHAMMAD ALIKUFA NA DHAMBI NYINGI SANA KULIKO KIUMBE CHOCHOTE KILE.   Katika...
Par MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-24 21:37:38 0 5KB
OTHERS
SINAGOGI SIO MSIKITI
TUNAZIDI KUCHAMBUA HOJA ZA MIHADHARA ya Kiislamu   LEO TUANGALIE SINAGOGI!! Sehemu ya...
Par MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-25 11:56:02 0 8KB