KUZIMU Ni Mahali Pa Namna Gani, Je! Huko Wanaishi Watu Wakifa Na Kwenda Kupata Mateso Au Ni Vinginevyo?

0
7KB

JIBU: Kuzimu ipo, na ni sehemu iliyo halisi kabisa biblia inaelezea katika (Luka 16:19-31)… Mtu anapokufa katika dhambi (yaani haujaoshwa dhambi zake kwa damu ya YESU KRISTO)..mtu anaenda moja kwa moja kuzimu/jehanum, huko kuna mateso mengi sana, mtu huyo atakaa huko akingojea ufufuo wa wafu, ambao utakuja baada ya ule utawala wa YESU KRISTO wa miaka 1000 kuisha ambapo wafu wote watafufuliwa na kuhukumiwa mbele ya kile kiti cheupe cha Hukumu..  

Ufunuo 20:12 “Nikawaona wafu, wakubwa kwa wadogo, wamesimama mbele ya hicho kiti cha enzi; na vitabu vikafunguliwa; na kitabu kingine kikafunguliwa, ambacho ni cha uzima; na hao wafu wakahukumiwa katika mambo hayo yaliyoandikwa katika vile vitabu, sawasawa na matendo yao. 13 Bahari ikawatoa wafu waliokuwamo ndani yake; na Mauti na Kuzimu zikawatoa wafu waliokuwamo ndani yake. Wakahukumiwa kila mtu kwa kadiri ya matendo yake. 14 Mauti na Kuzimu zikatupwa katika lile ziwa la moto. Hii ndiyo mauti ya pili, yaani, hilo ziwa la moto. 15 Na iwapo mtu ye yote hakuonekana ameandikwa katika kitabu cha uzima, alitupwa katika lile ziwa la moto”.  

Ukisoma pia Yohana 5:28 BWANA YESU aliyasema maneno hayo..

“Msistaajabie maneno hayo; kwa maana saa yaja, ambayo watu wote waliomo makaburini wataisikia sauti yake. 29 Nao watatoka; wale waliofanya mema kwa ufufuo wa uzima, na wale waliotenda mabaya kwa ufufuo wa hukumu.”  

Unaona wale wanaotenda mabaya wote watafufuliwa kwa ufufuo wa hukumu, hivyo baada ya kuhukumiwa kulingana na matendo yao ndipo watakapotupwa kwenye lile ZIWA LA MOTO atakapokuwepo shetani na malaika zake, lenye mateso mengi kuliko jehanum. ni kama tu vile mtu anapokamatwa na hatia anawekwa kwanza mahabusu kwa muda fulani akisubiria kupandishwa mahakamani, sasa akishahukumiwa mahakamani kulingana na makosa yake ndipo anapopelekwa magereza kutumikia makosa yake. na ndivyo itakavyokuwa kwa waovu wote walioikataa neema ya msalaba wa Bwana YESU KRISTO watakapokufa sasa hivi wataenda kuzimu kwenye vifungo na mateso, wakingojea hukumu ya mwanakondoo kisha baadaye watatupwa kwenye lile ziwa la moto.

Lakini wanaokufa sasa katika haki, wanapelekwa mahali panapoitwa “Paradiso” . Paradiso ni mahali panapofanana na mbinguni,lakini sio mbinguni, ni mahali pa raha, wanawekwa humo kwa muda fulani wakingojea ufufuo wa wenye haki, atakapokuja Bwana mawinguni, watafufuliwa na kuvaa miili ya utukufu na kuungana na watakatifu walio hai na kwa pamoja kwenda na Bwana mbinguni kwenye karamu ya mwana kondoo.   Paradiso kwa jina lingine ni Peponi.

1 Wathesalonike 4: 15 “Kwa kuwa twawaambieni haya kwa neno la Bwana, kwamba sisi tulio hai, tutakaosalia hata wakati wa kuja kwake Bwana, hakika hatutawatangulia wao waliokwisha kulala mauti. 16 Kwa sababu Bwana mwenyewe atashuka kutoka mbinguni pamoja na mwaliko, na sauti ya malaika mkuu, na parapanda ya Mungu; nao waliokufa katika Kristo watafufuliwa kwanza. 17 Kisha sisi tulio hai, tuliosalia, tutanyakuliwa pamoja nao katika mawingu, ili tumlaki Bwana hewani; na hivyo tutakuwa pamoja na Bwana milele.”  

Hivyo ndugu fahamu kuwa kuzimu ipo. Ni sehemu halisi kabisa.

Ubarikiwe sana.  


Pesquisar
Categorias
Leia mais
MASWALI & MAJIBU
Je! Wayahudi Wote Wataokolewa Kulingana Na Warumi 11:26?
SWALI: Je! Wayahudi wote wataokolewa? maana biblia inasema katika; Warumi 11:25...
Por GOSPEL PREACHER 2022-06-13 00:22:40 0 5KB
Injili Ya Yesu Kristo
NAMNA YA KUJENGA MAHUSIANO MAZURI NA ROHO MTAKATIFU.
Yohana 14:16-17. Biblia inasema “ Nami nitamwomba Baba, naye atawapa Msaidizi mwingine, ili...
Por GOSPEL PREACHER 2021-11-23 12:59:31 0 5KB
OTHERS
MUHAMMAD NI MTUME BANDIA
1. Hakutumwa na Mungu2. Alipewa Utume na Mkewe3. Alichezewa na Mashetani tokea utoto wake Leo...
Por MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-22 05:33:15 0 5KB
REVELATION
UTAWALA WA MIAKA 1000
Shalom mtu wa Mungu, karibu tujifunze maandiko matakatifu, kama Biblia inavyosema...
Por GOSPEL PREACHER 2021-10-30 12:39:10 0 6KB
Injili Ya Yesu Kristo
EPUKA MUHURI WA SHETANI
Kutoka 21:2-6 ” Ukimnunua MTUMWA wa Kiebrania, atakutumikia muda wa miaka sita; mwaka wa...
Por GOSPEL PREACHER 2023-01-08 00:30:30 0 8KB