Sabato Halisi Ni Lini, Je! Ni Jumapili Au Jumamosi?, Ni Siku Gani Itupasayo Kuabudu?

0
5K

JIBU: Neno la Mungu linasema Mungu ni Roho nao wamwabuduo imewapasa wamwabudu katika roho na kweli. Wakristo hawahesabiwi haki mbele za Mungu katika siku, miezi au miaka ya kuabudia, aidha uabudu jumapili, jumatatu, jumamosi au jumatano huo ni utaratibu wa mtu tu! haimuongezei mtu chochote katika uhusiano wake na Mungu. Biblia inasema..  

Wagalatia 4:9 “Bali sasa mkiisha kumjua Mungu, au zaidi kujulikana na Mungu, kwa nini kuyarejea tena mafundisho ya kwanza yaliyo manyonge, yenye upungufu, ambayo mnataka kuyatumikia tena? Mnashika SIKU, NA MIEZI, NA NYAKATI NA MIAKA.”

 Na Pia inasema tena katika

Wakolosai 2:16 “Basi, mtu asiwahukumu ninyi katika vyakula au vinywaji, au kwa sababu ya sikukuu au mwandamo wa mwezi, au SABATO; mambo hayo ni kivuli cha mambo yajayo; bali mwili ni wa Kristo.”  

Hivyo Maana ya NENO sabato ni “Pumziko”, na pumziko kwa wakristo lipo rohoni, na mwokozi wetu Yesu yeye alituambia kuwa ndiye BWANA wa sabato (soma Mathayo 12:8), hivyo tukimpata YESU tumeipata SABATO au “pumziko letu la rohoni” na ndio maana anasema..  

Mathayo 11:28 “ Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami NITAWAPUMZISHA. 29 Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu; 30 kwa maana nira yangu ni laini, na mzigo wangu ni mwepesi.”

Kwahiyo wanaoabudu jumamosi, au jumapili au jumatano hawafanyi makosa, ni utaratibu wao tu, mbele za Mungu wote wapo sawa, kwa mfano tunasoma katika biblia wakristo wakwanza waliiteua siku ya kwanza ya juma ( yaani JUMAPILI) kwa ajili ya kukusanyika na kufanya changizo pamoja na kumega mkate,ukisoma Matendo 20:7 na 1Wakoritho 16:1-2 utaona jambo hilo, hivyo kuteua siku fulani na kusema hiyo ndio Mungu anairidhia kuabudia zaidi ya siku nyingine, ni kutokuyaelewa maandiko.   kwasababu ibada halisi ipo rohoni na Mungu anaabudiwa katika roho na kweli, na sio katika siku maalumu au miezi maalumu au miaka maalumu bali ni kila saa na kila wakati mahali popote.  

Ubarikiwe sana.

Cerca
Categorie
Leggi tutto
OTHERS
ETI, YESU ALIPOKUWA AMEKUFA DUNIA ILIKUWA INAENDESHWA NA NANI?
Hili ndilo swali la wafuasi wa Muhammad kwa Wakristo na leo nitalijibu hapa.   Hili ni swali...
By MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-25 11:42:36 0 6K
Injili Ya Yesu Kristo
Ushuhuda wa Victoria Juu ya Kuzimu
Huu ni ufupisho wa ushuhuda wa Victoria Nehale Nilizaliwa na kuishi Namibia maisha yangu yote;...
By MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-22 02:40:22 0 5K
SPIRITUAL EDUCATION
MACHO YA TAI AWINDAE MAWINDO YAKE
Macho ya Tai AWINDAE mawindo yake  Kila mmoja wetu tunapaswa kuwa na macho ya kuona...
By Martin Laizer 2023-09-22 09:29:34 2 20K
REVELATION
UFUNUO 14
Kama tunavyofahamu baada ya wakati wa mataifa kuisha yaani unyakuo kupita itakuwa imebaki miaka 7...
By GOSPEL PREACHER 2021-10-30 11:47:48 0 6K
BIBLICAL FINANCIAL EDUCATION
7 BIBLICAL PRINCIPLES OF MONEY MANAGEMENT
The 7 Biblical Principles of Money Management that you are about to learn were...
By BIBLICAL FINANCES 2021-12-29 15:38:36 0 16K