Sabato Halisi Ni Lini, Je! Ni Jumapili Au Jumamosi?, Ni Siku Gani Itupasayo Kuabudu?

0
5K

JIBU: Neno la Mungu linasema Mungu ni Roho nao wamwabuduo imewapasa wamwabudu katika roho na kweli. Wakristo hawahesabiwi haki mbele za Mungu katika siku, miezi au miaka ya kuabudia, aidha uabudu jumapili, jumatatu, jumamosi au jumatano huo ni utaratibu wa mtu tu! haimuongezei mtu chochote katika uhusiano wake na Mungu. Biblia inasema..  

Wagalatia 4:9 “Bali sasa mkiisha kumjua Mungu, au zaidi kujulikana na Mungu, kwa nini kuyarejea tena mafundisho ya kwanza yaliyo manyonge, yenye upungufu, ambayo mnataka kuyatumikia tena? Mnashika SIKU, NA MIEZI, NA NYAKATI NA MIAKA.”

 Na Pia inasema tena katika

Wakolosai 2:16 “Basi, mtu asiwahukumu ninyi katika vyakula au vinywaji, au kwa sababu ya sikukuu au mwandamo wa mwezi, au SABATO; mambo hayo ni kivuli cha mambo yajayo; bali mwili ni wa Kristo.”  

Hivyo Maana ya NENO sabato ni “Pumziko”, na pumziko kwa wakristo lipo rohoni, na mwokozi wetu Yesu yeye alituambia kuwa ndiye BWANA wa sabato (soma Mathayo 12:8), hivyo tukimpata YESU tumeipata SABATO au “pumziko letu la rohoni” na ndio maana anasema..  

Mathayo 11:28 “ Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami NITAWAPUMZISHA. 29 Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu; 30 kwa maana nira yangu ni laini, na mzigo wangu ni mwepesi.”

Kwahiyo wanaoabudu jumamosi, au jumapili au jumatano hawafanyi makosa, ni utaratibu wao tu, mbele za Mungu wote wapo sawa, kwa mfano tunasoma katika biblia wakristo wakwanza waliiteua siku ya kwanza ya juma ( yaani JUMAPILI) kwa ajili ya kukusanyika na kufanya changizo pamoja na kumega mkate,ukisoma Matendo 20:7 na 1Wakoritho 16:1-2 utaona jambo hilo, hivyo kuteua siku fulani na kusema hiyo ndio Mungu anairidhia kuabudia zaidi ya siku nyingine, ni kutokuyaelewa maandiko.   kwasababu ibada halisi ipo rohoni na Mungu anaabudiwa katika roho na kweli, na sio katika siku maalumu au miezi maalumu au miaka maalumu bali ni kila saa na kila wakati mahali popote.  

Ubarikiwe sana.

Buscar
Categorías
Read More
OTHERS
KORAN INAKIRI KUWA UISLAMU NI DINI YA WAARABU PEKEE
Katika hii mada ninawaletea ushaidi kuwa Uislam ni dini ya Waarabu peke yao. Waislamu bila...
By MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-23 08:44:35 0 5K
SPIRITUAL EDUCATION
JINSI LAANA YA ROHO MTAKATIFU INAVYOENDELEA MIONGONI MWA WAHUBIRI WA INJILI PASIPO KUJIJUA.
JINSI LAANA YA ROHO MTAKATIFU INAVYOENDELEA MIONGONI MWA WAHUBIRI WA INJILI PASIPO KUJIJUA.
By Martin Laizer 2024-01-06 17:28:15 0 8K
MAHUSIANO KIBIBLIA
UNA HOFU YA KUTOKUOLEWA, AU KUACHIKA? SOMA HII ITAKUSAIDIA
Kama wewe ni mwanamke na bado hujaolewa, na sasa kitu kama hofu ndani yako ya kutokuolewa...
By GOSPEL PREACHER 2021-11-07 23:29:46 0 6K
OTHERS
KUMBE KORAN HAIKUTEREMSHWA KUTOKA KWA ALLAH
Ni Nani Walikuwa Waandishi Wa Quran Tukufu Wakati Wa Mtume Muhammad? Je, ungependa kuwafahamu...
By MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-22 18:29:28 0 5K
DEUTERONOMY
Verse by verse explanation of Joshua 10
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 49 questions at the...
By THE HOLY BIBLE 2022-01-25 07:40:06 0 6K