Nini Maana Ya Kusali Kwa Kupayuka Payuka?

0
5KB
Swali linaendelea…..Na Je, nisali kwa namna gani ili maombi yangu yasionekane kuwa ni ya kupayuka payuka mbele za Mungu?
 
JIBU: Mungu akubariki ndugu,Mathayo 6:7 Inasema:
Nanyi mkiwa katika kusali, msipayuke-payuke, kama watu wa mataifa; maana wao hudhani ya kuwa watasikiwa kwa sababu ya maneno yao kuwa mengi.
 Sasa mstari huo ukiangalia kwenye tafsiri nyingine hilo neno “kupayuka-payuka” halimaanishi kama “kupaza sauti kwa nguvu,” kama watu wengi wanavyodhani, hapana bali linamaanisha “KURUDIA-RUDIA” maneno yale yale, Hilo la kupaza sauti kwa nguvu mstari wake ni ule wa juu yake kabla ya huu unaosema:
“Mathayo 6: 5 Tena msalipo, msiwe kama wanafiki; kwa maana wao wapenda kusali hali wamesimama katika masinagogi na katika pembe za njia, ili waonekane na watu. Amin, nawaambia, Wamekwisha kupata thawabu yao. 6 Bali wewe usalipo, ingia katika chumba chako cha ndani, na ukiisha kufunga mlango wako, usali mbele za Baba yako aliye sirini; na Baba yako aonaye sirini atakujazi.
 
Unaona, aina hii ya watu ndio wanaopenda kupaza sauti zao kwa nguvu kwa lengo la kuonekana na watu ndio hao wanaoonekana wamesimama katika masinagogi na katika pembe za njia. Watu wa namna hiyo Bwana anasema Wamekwisha kupata thawabu yao, Lakini pia kumbuka hilo halimaanishi watu wasiombe kwa kupaza sauti zao, hapana, biblia inasisitiza sana tupaze sauti zetu tumliliapo Mungu…Lakini sio kwa lengo la kujionyesha sisi tunajua kusali, au sisi ni wa kiroho sana. Vinginevyo tutakuwa tumeshapata thawabu zetu.
 
Lakini sasa kwa wale wanao payuka payuka mstari wao ndio huo unaofuata…
 7 Nanyi mkiwa katika kusali, msipayuke-payuke, kama watu wa mataifa; maana wao hudhani ya kuwa watasikiwa kwa sababu ya maneno yao kuwa mengi. 8 Basi msifanane na hao; maana Baba yenu anajua mnayohitaji kabla ninyi hamjamwomba. “
Hivyo watu wanao rudia-rudia maneno, kwa mfano watu dini nyingine na watu wanaosali rozari na sala za bikira mariamu wanafahamu,huwa wanarudia rudia maneno yale yale kwa muda mrefu hata masaa na masaa wakidhani kuwa kwa kufanya vile Mungu atasikia dua zao. Hizo ni desturi za kipagani ndio maana tumeonywa tusifanane na hao. kwahiyo tunapoenda mbele za Mungu tuwe na malengo, tutoe hoja zetu zote, kisha zikishaisha, basi, tushukuru tuondoke Tukiamini kuwa Mungu kashatusikia na sio kuanza kurudia rudia tena kile tulichokiomba kana kwamba Mungu hasikii,. kwa ufupi usiweke mfumo fulani unaoonyesha mrudio rudio katika kusali, kuwa huru mbele za Mungu ndivyo Sala zako zitakavyokuwa na thamani mbele za Mungu.
 
Ubarikiwe sana.

 

Rechercher
Catégories
Lire la suite
JOB
Verse by verse explanation of Job 37
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 27 questions at the...
Par THE HOLY BIBLE 2022-04-03 04:19:38 0 5KB
JOSHUA
Verse by verse explanation of Joshua 7
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 31 questions at the...
Par THE HOLY BIBLE 2022-01-25 07:27:14 0 5KB
PSALMS
Verse by verse explanation of Psalm 20
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 26 questions at the...
Par THE HOLY BIBLE 2022-05-20 12:20:31 0 7KB
SPIRITUAL EDUCATION
DEMONS - WHAT ARE THEY?
Demons are NOT human. They are invisible evil spirits with various sizes and shapes.God did in...
Par MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-22 19:04:18 0 4KB
OTHERS
KWANINI MUHAMMAD ALITAKA KUJINYONGA “COMMIT SUICIDE”?
1. MUHAMMAD ALITAKATA KUJINYONGA2. MUHAMMAD ALIPANDA MLIMANI NA KUJARIBU KUJIRUSHA ILI AFE3....
Par MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-24 22:55:32 0 5KB