UNYENYEKEVU.

0
5χλμ.

Bwana Yesu asifiwe...

Kwa ufupi.

” Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu; “ Mathayo 11:29

“unyenyekevu”hali ya kushuka,kukubali kuonekana mdogo/mtumishi wa wote,kukubali lawama na kuvumilia. Si jambo jepesi kukubali kuwa chini hali wewe una vitu vingi. Si rahisi hata kidogo kukubali lawama. Wengi wanapenda wawe wanyenyekevu lakini hawapo tayari kushuka,kupokea lawama,kuvumilia n.k. Unyenyekevu ni ghalama mpendwa!

  • Unyenyekevu ni tabia ya Yesu. Yesu alikuwa ni mnyenyekevu wa moyo

Yesu alikuwa mnyenyekevu wa moyo,sio wa kuigiza. Alikuli mateso yote ingawa alikuwa na uwezo wa kuyakataa,lakini kwa kusudi la kutufundisha ilimbidi akubali na kwa lile kusudi la ukombozi,alikubali yote. Fikiri pale alipopelekwa mbele wa waashi na wakuu wa makuhani kisha wakamsomea mashtaka ya uongo,lakini alikaa kimya asitie neno lolote hali akijua yote yanayoendelea. Hakika mtu huyu alikuwa ni mnyenyekevu wa moyo. Najiuliza,sijui ungelikuwa mwenzangu na mimi,wewe hapo- ungelisemaje au ngelifanyeje pale unaposhtakiwa kwa maneno ya uongo? naona wewe ungerusha ngumi,au ungetukana sana kiasi kwamba mpaka wangelikuachia! lakini haikuwa hivyo kwa Yesu.

Yeye ambaye ndiye mnyenyekevu wa moyo,anakutaka na wewe usiyemnyenyekevu ukajifunze kwake huo unyenyekevu. Anakualika ujitie  “nira” yake kwa maana nira yake ni laini na mzigo wake ni mwepesi nawe utapata raha nafsini mwako. Neno “nira” ni kongwa,wanalovalishwa ngombe ili waweze kulima pamoja. ( ni kama mbao iwekwayo kwenye shingo zao,kufunga ngombe na ngombe na hatimaye mkulima mmoja uishika mbele na kuwapeleka popote atakapo,nao huenda.)Yesu ametumia piacha hiyo kutufundisha kama tukijifunga nira yake,tutaweza kumfuata popote aendapo,na tujifunze kwake unyenyekevu wake.

  • Kinyume cha unyenyekevu ni kiburi

Ikiwa mtu amekosa unyenyekevu huwa na kiburi,na kiburi ni tabia ya shetani mwenye kupenda kusifiwe. Wataalamu maandiko husema kwamba kila mwanadamu amezaliwa na tabia ya kiburi. Na ndio maana kila mtu hupenda kujisikia,kusifiwe,kuonekana n.k Lakini unyenyekevu hutoka kwa Bwana,mtu hazaliwi nao. Ukimwona mtu mnyenyekevu toka tumboni mwa mamaye hujue huyo kapewa “neema ” tu kwa maana si jambo la kawaida. Kwa hiyo utagundua kwamba unayo kazi ya kujifunza kila siku habari ya unyenyekevu wa Yesu ili kusudi uwe mnyenyekevu na utoke katika kiburi.

Αναζήτηση
Κατηγορίες
Διαβάζω περισσότερα
OTHERS
MUHAMMAD ALIKUWA NA WAKE ZAIDI YA 20
Huu ni MSIBA mkubwa sana. Ifuatayo ni orodha ya wake wa Muhammad iliyoandaliwa na mwanazuoni wa...
από MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-24 22:48:32 0 5χλμ.
Injili Ya Yesu Kristo
Kujengwa kwa Hekalu bila kelele!
1Wafalme 6:7. “Na nyumba ilipokuwa ikijengwa, ikajengwa kwa mawe yaliokwisha kuchongwa...
από GOSPEL PREACHER 2022-04-01 08:26:15 0 6χλμ.
Injili Ya Yesu Kristo
NINI MAANA YA KUUMBWA KWA MFANO WA MUNGU?
Mungu ni Roho. Je wewe ni nani?Katika somo hili la uumbaji wa binadamu, nitajibu hoja na maswali...
από MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-23 08:12:32 0 6χλμ.
OTHERS
KUWA MUISLAM NI KUJIFUNZA UCHAWI. SHEHE OMARI MNYISHANI
SOMO:AINA ZA UCHAWI KATIKA UISILAMU i. Habize/Hepatoscopy (huu ni uchawi wa kutumia maini)...
από MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-24 22:22:38 0 6χλμ.
SPIRITUAL EDUCATION
DEMONS - WHAT ARE THEY?
Demons are NOT human. They are invisible evil spirits with various sizes and shapes.God did in...
από MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-22 19:04:18 0 5χλμ.