UKWELI KUHUSU HAKI IPATIKANAYO KWA IMANI

0
5Кб

BWANA YESU ASIFIWE!! Mpendwa Roho Mtakatifu ameweka

Nyakati hizi tunazoishi ni nyakati/siku za mwisho, tena ukweli kamili ni kwamba sisi leo tunaishi mwishoni mwa siku za mwisho, hivyo muda wowote ule kuanzia sasa, Kristo Yesu atarudi kuja kulinyakua kanisa lake (mathayo 99898989). Na kwa kuwa zimebaki siku chache sana, ndio maana Ibilisi/Shetani anafanya kazi kwa kasi kubwa sana maana anajua muda wake uliobaki ni mchache(mathayo 8980980980). Usisahau lengo la Shetani ni moja tu nalo ni kuhakikisha mwanadamu anachomwa moto milele pamoja naye.

Pia usisahau kuwa ilishatabiriwa katika siku zetu hizi za mwisho, watatokea manabii wa uongo wengi, watakaofundisha mafundisho ya uongo ili kudanganya watu waiache njia ya kweli ya Kristo Yesu, tena ilitabiriwa kuwa watafanikiwa kuwadanganya wengi. Muda huu unaposoma ujumbe huu, napenda utambue kuwa roho hii chafu kutoka kuzimu, tayari ipo duniani na inafanya kazi kwa nguvu zake zote. Hivyo kufanya maombi ili kuikemea itoke ni kupoteza muda, maana maombi hayo hayatajibiwa, kwa kuwa huu ndio wakati wake haswa wa kufanya kazi, hivyo maombi sahihi ni kuomba nguvu ya Roho Mtakatifu itufunike ili tusiwe miongoni mwa wengi watakaodanganywa na kupotoshwa na mafundisho potofu yanayohubiriwa na mawakala wa roho hii chafu.

 Hivyo lengo la ujumbe huu sio kuizuia roho hii isifanye kazi (maana inafanya kazi katika wakati wake ulioamuriwa na Mungu), bali ujumbe huu umekusudia mambo makuu matatu yafuatayo:-

  • Nimekusudia kukuhubiri injili halisi na ya kweli ili wewe usiwe miongoni mwa hao wengi wanaodanganywa, kumbuka njia iendayo upotevuni ni pana nao waipitao ni wengi, lakini nakuombea wewe usiwe miongoni mwao.
  • Hata kama utaukataa ujumbe huu kwa siku ya leo, lakini ni maombi yangu kwa Mungu kuwa Roho wake Mtakatifu ataendelea kusema na roho yako ili yamkini nawe pia uweze kuikubali, na ujiunge na safari yetu tuliyonayo ya kwenda mbinguni.
  • Na hata kama bado utaikataa sauti hii ya Roho Mtakatifu, bado nitakuwa nimefanikisha lengo moja tu nalo ni: kukueleza ukweli ili damu yako Mungu asiidai mikononi mwangu.

k

Love
1
Поиск
Категории
Больше
OTHERS
ALLAH ANASEMA KATIKA KORAN KUWA WAISLAM WOTE WATAINGIA JEHANNAM
Jamani huu ni Msiba katika taifa la Islam kwa kushindwa kusoma aya hii ambayo ipo wazi (Quran...
От MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-23 08:48:28 0 7Кб
GENESIS
Verse by verse explanation of Genesis 38
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 39 questions at the...
От THE HOLY BIBLE 2022-01-21 09:13:18 0 5Кб
OTHERS
WAISLAM NAOMBENI MAJIBU KATIKA UTATA HUU WA AYA ZA QURAN!!!
Kila nikiulizaga maswali kwa ndugu zetu waislam hawanijibu,wanachokifanya ni kubadilisha mada tu...
От MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-22 19:23:04 0 5Кб
Injili Ya Yesu Kristo
Je umeshapata Zawadi ya Uzima wa milele?
Bibilia inaonyesha njia ya wazi ya uzimani.Mwanzo ni sharti tutambue yakwamba tumetenda dhambi...
От MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-23 09:42:08 0 6Кб
SPIRITUAL EDUCATION
MUNGU HANA DINI
Mungu Mtakatifu hana ushirika na dhambi. Kati yake na mwanadamu kuna ufa mkubwa wa dhambi....
От MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-22 04:31:19 0 6Кб