KWANINI MUNGU HUBARIKI MATAIFA YANAYOIBARIKI ISRAELI?

0
5KB
Taifa la Israeli pamoja na mji wake mtakatifu wa Yerusalemu, kimsingi ndio unaoshika funguo za maisha ya baadaye na kuratibu kila hitimisho la kidunia kulingana na unabii katika Maandiko matakatifu. Patanisho la wanadamu na Mungu hata kuwaletea wanadamu neema ya kuwa na amani na Mungu lilifanyika Israeli. Kwa upande mwingine, ningeweza kusema kwamba; kutimilika kwa unabii wa maandiko matakatifu, kunahusianishwa moja kwa moja na taifa la Israeli.
 
Ni kwa sababu hiyo basi, chochote kinachotokea katika nchi ya Israeli kinaathiri kwa namna moja au nyingine kile Mungu anachokwenda kufanya kwa mataifa yote ya ulimwengu.
 
Kama kungekuwa na uwezekano wa kulitowesha taifa la Israeli pamoja na nchi yao, basi Biblia ingekuwa haina maana na wala utimilifu wa maandiko usingewezekana. Kumbuka kwamba, uwanja wa matukio yote ya nyakati za mwisho yaliyoandikwa kwenye Biblia ni Israeli. Mfano;
 
§ Vita vya Harmagedon vitapiganwa kwenye bonde la Megido lililoko Israeli UFUNUO 16:14-16, “Hizo ndizo roho za mashetani, zifanyazo ishara, zitokazo na kuwaendea wafalme wa ulimwengu wote; kuwakusanya kwa vita ya siku ile kuu ya Mungu mwenyezi. Tazama naja kama mwivi. Heri akeshaye, na kuyatunza mavazi yake, asiende uchi hata watu wakaione aibu yake. Wakawakusanya hata mahali paitwapo kwa Kiebrania, Har-Magedoni.” ZEKARIA 12:11 Biblia inasema” Siku hiyo kutakuwa na maombolezo makuu huko Yerusalemu kama maombolezo ya Hadadrimoni katika bonde la MEGIDO”
 
§ Bwana Yesu atakaporudi mara ya pili, ni lazima ashukie kwenye mlima wa Mizeituni nchini Israeli, ZEKARIA 14:4 Biblia inasema, “Na siku hiyo miguu yake itasimama juu ya mlima wa Mizeituni unaoelekea Yerusalemu upande wa mashariki, nao mlima wa Mizeituni utapasuka katikati yake upande wa mashariki na upande wa magharibi, litakuwapo huko bonde kubwa sana na nusu ya mlima ule utaondoka kwenda upande wa kaskazini na nusu yake utaondoka kwenda upande wa kusini”
 
§ Wakati wa utawala wa miaka 1000 wa Bwana wetu Yesu Kristo hapa duniani, maskani yake yatakuwa katika mji wa Yerusalemu ulioko Israeli (UFUNUO 20:7-10).
§ Mpinga Kristo na nabii wa uongo watakaojiinua katika kipindi cha dhiki kuu, ni lazima waukanyage mji mtakatifu wa Yerusalemu, UFUNUO 11:2, “Na behewa iliyo nje ya hekalu uiache nje wala usiipime, kwa maana Mataifa wamepewa hiyo, nao wataukanyaga mji mtakatifu miezi arobaini na miwili.”

Kwa hiyo, kwa kadri tunavyolielewa taifa hili la Mungu kwa mapana na marefu, na ndivyo uelewa wetu wa mambo ya sasa na yajayo unavyozidi kuwa mpana sana.
Suche
Kategorien
Mehr lesen
DIPLOMA
DIPLOMA
List of all subjects for the students who are taking diploma courses.
Von PROSHABO ONLINE SCHOOLS 2021-10-09 10:54:15 0 6KB
EXODUS
Verse by verse explanation of Exodus 2
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 70 questions at the...
Von THE HOLY BIBLE 2022-01-21 12:42:02 0 5KB
OTHERS
UONGO WA DINI YA KIISLAM
Tunaamini unapofuata kwa makini mada hii utatii neno la Mungu wa kweli, kuliishi, na kulitenda....
Von MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-22 04:45:10 0 5KB
HOLY BIBLE
Did Jesus fight Satan for the keys to the kingdom?
Keys are a symbol of control. Keys keep people in or out. If they do not have a key to a lock,...
Von MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-24 04:21:41 0 6KB
OTHERS
ALLAH IS A CREATION AND NOT THE CREATOR
Who is Allah?   the Islamic diabolical deity is called “The Greatest Deceiver”...
Von MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-24 20:28:12 0 6KB