Biblia inasema nini juu ya kunywa pombe? Je, ni dhambi kwa mkristo kunywa pombe?

0
7χλμ.
Maandiko yana ilani nyingi juu ya kunywa kileo (mambo ya walawi 10:9; hesabu6:3; kumbukumbu la torati 29:6; waamuzi 13:4,7,14; samueli wa kwanza 1:15; methali 20:1; 31:4,6; isaya 5:11;22; 24:9; 28:7; 29:9; 56:12; mika 2:11; luka 1:15). Maandiko hayakatazi mkristo kunywa pombe, divai wala kinywaji chochote chenye kileo ndani. Maana maandiko mengine huzungumzia kileo kwa kuhalalisha matumizi yake. Mhubiri 9:7 inaamuru, “ kunywa kileo na moyo mkunjufu.” Zaburi 104:14-15 inaeleza Mungu hutoa divai “ inayofurahisha mioyo ya wanadamu.” Amosi 9:14 inazungumzia juu ya kunywa divai kutoka kwa shamba lako kama alama ya baraka za Mungu. Isaya 55;11 inapongeza “ naam, njoo ununue divai na maziwa…”
 
Kile Mungu anachowaamuru wakristo juu ya kileo ni wajizuie na ulevi (waefeso 5:18). Biblia inakataza ulevi na athari zake (methali 23:29-35). Wakristo wanakatazwa kuachilia miili yao itawalwe na vitu vinginevyo. (wakorintho wa kwanza 6:12; petro wa pili 2:19). Kunywa kileo kingi kunaathiri mtu. Maandiko yanakataza chochote kile ambacho kwa kukifanya unasababisha wengine kujikwaa( wakorintho wa kwanza 8:9-13). Kwa mujibu wa haya ni vigumu mkristo kukiri kuwa anakunywa kileo kwa utukufu wa Mungu ( wakorintho wa kwanza 10;31). 
 
Yesu aligeuza maji kuwa Divai. Huenda ikawa Yesu alikuwa akinywa divai katika karamu Fulani Fulani (Yohana 2:1-11; Mathayo 26: 29). Katika nyakati za agano jipya, maji yalikuwa yakijawa na vidudu na uchafu kama hali ilivyo sasa katika mataifamengine ya ulimwengu wa tatu. Hii ndiyo sababu watu walipendelea kunywa divai kutoka kwa zabibu ili kuepukana na taka taka hizi. Katika timotheo wa kwanza 5:23, Paulo alimkataza timotheo kunywa maji yaliyokuwa yakimtatiza tumbo lake na mahali pake anywe divai. Divai ilikuwa na asili ya kileo ndani lakini haikuwa na kiwango cha kilevi sawa na cha leo. Haikuwa maji ya mzabibu moja kwa moja wala kileo sawa na cha leo. Maandiko hayakatazi mkristo kunywa kileo cha aina yoyote bali yanakataza ulevi na utumwa wa kileo (waefeso 5:18; wakorintho wa kwanza 6:12).
 
Kileo, kinapotumiwa kwa uchache hakina athari kwa mwenye kukitumia. Kutumia kiasi kichache cha kileo ni jambo linaloruhusiwa mkristo. Ulevi na utumwa wa kunywa kileo ni dhambi. Kwa sababu ya kushindwa kujizuia katika viwango vya matumizi ya kileo, kukwaza wengine na hata kupatikana na hatia mbali mbali, ni vizuri mkristo aepukane kabisa na matumizi ya kileo cha aina yoyote.
Αναζήτηση
Κατηγορίες
Διαβάζω περισσότερα
GENESIS
Verse by verse explanation of Genesis 2
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 43 questions at the...
από THE HOLY BIBLE 2022-01-01 10:35:25 0 6χλμ.
GENESIS
Verse by verse explanation of Genesis 21
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 28 questions at the...
από THE HOLY BIBLE 2022-01-21 05:11:59 0 6χλμ.
Religion
JE UNA MATUMAINI YA KUPATA TENA KILE ULICHOPOTEZA?
JE UNA MATUMAINI YA KUPATA TENA KILE ULICHOPOTEZA? Jina kuu la Bwana na Mwokozi wetu na wa...
από WINGU LA MASHAHIDI 2021-09-18 21:20:12 0 8χλμ.
Injili Ya Yesu Kristo
KILA ATAKAYELIITIA JINA LA BWANA ATAOKOKA.
Kwa ufupi.. Bwana Yesu asifiwe… `` Kwa kuwa,kila atakayeliitia Jina la Bwana...
από GOSPEL PREACHER 2022-03-30 05:01:07 0 6χλμ.
EXODUS
Verse by verse explanation of Exodus 3
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 80 questions at the...
από THE HOLY BIBLE 2022-01-21 14:08:20 0 6χλμ.