Biblia inasema nini juu ya kunywa pombe? Je, ni dhambi kwa mkristo kunywa pombe?

0
6KB
Maandiko yana ilani nyingi juu ya kunywa kileo (mambo ya walawi 10:9; hesabu6:3; kumbukumbu la torati 29:6; waamuzi 13:4,7,14; samueli wa kwanza 1:15; methali 20:1; 31:4,6; isaya 5:11;22; 24:9; 28:7; 29:9; 56:12; mika 2:11; luka 1:15). Maandiko hayakatazi mkristo kunywa pombe, divai wala kinywaji chochote chenye kileo ndani. Maana maandiko mengine huzungumzia kileo kwa kuhalalisha matumizi yake. Mhubiri 9:7 inaamuru, “ kunywa kileo na moyo mkunjufu.” Zaburi 104:14-15 inaeleza Mungu hutoa divai “ inayofurahisha mioyo ya wanadamu.” Amosi 9:14 inazungumzia juu ya kunywa divai kutoka kwa shamba lako kama alama ya baraka za Mungu. Isaya 55;11 inapongeza “ naam, njoo ununue divai na maziwa…”
 
Kile Mungu anachowaamuru wakristo juu ya kileo ni wajizuie na ulevi (waefeso 5:18). Biblia inakataza ulevi na athari zake (methali 23:29-35). Wakristo wanakatazwa kuachilia miili yao itawalwe na vitu vinginevyo. (wakorintho wa kwanza 6:12; petro wa pili 2:19). Kunywa kileo kingi kunaathiri mtu. Maandiko yanakataza chochote kile ambacho kwa kukifanya unasababisha wengine kujikwaa( wakorintho wa kwanza 8:9-13). Kwa mujibu wa haya ni vigumu mkristo kukiri kuwa anakunywa kileo kwa utukufu wa Mungu ( wakorintho wa kwanza 10;31). 
 
Yesu aligeuza maji kuwa Divai. Huenda ikawa Yesu alikuwa akinywa divai katika karamu Fulani Fulani (Yohana 2:1-11; Mathayo 26: 29). Katika nyakati za agano jipya, maji yalikuwa yakijawa na vidudu na uchafu kama hali ilivyo sasa katika mataifamengine ya ulimwengu wa tatu. Hii ndiyo sababu watu walipendelea kunywa divai kutoka kwa zabibu ili kuepukana na taka taka hizi. Katika timotheo wa kwanza 5:23, Paulo alimkataza timotheo kunywa maji yaliyokuwa yakimtatiza tumbo lake na mahali pake anywe divai. Divai ilikuwa na asili ya kileo ndani lakini haikuwa na kiwango cha kilevi sawa na cha leo. Haikuwa maji ya mzabibu moja kwa moja wala kileo sawa na cha leo. Maandiko hayakatazi mkristo kunywa kileo cha aina yoyote bali yanakataza ulevi na utumwa wa kileo (waefeso 5:18; wakorintho wa kwanza 6:12).
 
Kileo, kinapotumiwa kwa uchache hakina athari kwa mwenye kukitumia. Kutumia kiasi kichache cha kileo ni jambo linaloruhusiwa mkristo. Ulevi na utumwa wa kunywa kileo ni dhambi. Kwa sababu ya kushindwa kujizuia katika viwango vya matumizi ya kileo, kukwaza wengine na hata kupatikana na hatia mbali mbali, ni vizuri mkristo aepukane kabisa na matumizi ya kileo cha aina yoyote.
Suche
Kategorien
Mehr lesen
OTHERS
If Jesus is God, then why did He say the Father was greater than He?
  "You heard that I said to you, ‘I go away, and I will come to you.’...
Von MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-23 09:47:05 0 5KB
OTHERS
ALIYE TABIRIWA KWENYE KUMBUKUMBU YA TORATI NI YESU AU MUHAMMAD?
Katika Kumbukumbu 18:17-18; 33:1-2, na 34:10-11, ni Muhammad aliyetabiriwa hapa, kama baadhi ya...
Von MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-24 22:40:09 0 7KB
OTHERS
USHUHUDA: MWANASHERIA MKUU WA SHERIA ZA KIISLAM WA IRAKI AMPOKEA YESU
KUTOKA: KWENYE GIZA LA UDANGANYIFU WA KIISLAMU HADI: KWENYE NURU YA UTUKUFU WA YESU Ushuhuda wa...
Von MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-22 04:10:49 0 5KB
2 CHRONICLES
Verse by verse explanation of 2 Chronicles 3
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 30 questions at the...
Von THE HOLY BIBLE 2022-04-01 21:58:36 0 5KB
Injili Ya Yesu Kristo
KUJA KWA YESU KRISTO MARA YA PILI DUNIANI NA VITA YA HAR-MAGEDONI
Neno la Uzima kutoka kwa  Askofu Zachary Kakobe        ...
Von GOSPEL PREACHER 2022-01-12 00:33:56 0 5KB