Ubatizo wa Rohoho Mtakatifu ni nini?

0
5K
Ubatizo wa Roho mtakatifu unaweza kufafanuliwa/kuelezwa kuwa ile kazi ambayo Roho Mtakatifu wa Mungu unamweka muumini kuwa na ushirika na Kristo na kwa ushirika na waumini wengine katika mwili wa Kristo wakati wa kuokolewa. Wakorintho wa kwanza 12:12-13 ni ukurasa wa katikati katika Bibilia kuhusu ubatizo wa Roho Mtakatifu, “Kwa maana katika Roho mmoja sisi sote tulibatizwa kuwa mwili mmoja, kwamba tu Wayahudi, au kwamba tu Wayunani; ikiwa tu watumwa au tu huru; nasi sote tulinyweshwa Roho mmoja.” (1Wakorintho 12:13). Bali Warumi 6:1-4 haitaji roho wa Mungu, bali yaelezea sehemu ya wakristo mbele za Mungu kwa lugha sawa na ile ya ujumbe wa kwanza Wakorintho: “Tusema nini basi? Tudumu kaitka dhambi ili neema izidi kuwa nyingi? Hasha! Sisi tulioifia dhambi tutaishije tena katika dhambi? Hamfahamu ya kuwa sisi sote tuliobatizwa katika Kristo Yesu tulibatizwa katika mauti yake? Basi tulizikwa pamoja kwa njia ya ubatizo katika mauti yake, kusudi kama Kristo alivyofufuka katika wafu kwa njia ya utukufu wa Baba, vivyo hivyo na sisi tuenende katika upya wa uzima.”
 
Hoja zifuatazo zatosha kudumisha uelefu wetu juu ya ubatizo wa Roho Mtakatifu. Kwanza, 1Wakorintho 12:13 yataja wazi kwamba wale wote waliobatizwa wananyweshwa Roho mmoja (kuwepo kwa Roho mtakatifu). Pili, hamna mahali katika Bibilia Wakristo wameelezwa wabatizwe, ndani ya, au kwa Roho au kwa vyovyote vile watafute ubatizo wa Roho Mtakatifu. Hii yaonyesha kuwa Wakrisot walikuwa na uzoevu. Tatu, Waefeso 4:5 yaonekana kuashiria ubatizo wa Roho. Kama hii ndio hali, ubatizo wa Roho Mtakatifu ni kitu cha kweli kwa kila Mkristo, kama vile “Imani mija” na “Baba mmoja” viko.
 
Kwa kumalizia, ubatizo wa Roho Mtakatifu wafanya mambo mawili, 1) Watuunganisha na mwili wa Kristo, na 2) Waambatanisha kusulubiwa kwetu na Yesu. Kuwa na mwili wake, yamaanisha, tumefufuliwa naye kwa upya wa uzima (Warumi 6:4). Kwa hivyo lazima tuviweka katika matendo vipawa vyetu vya Roho ili tuuweke mwili wa Kristo kuendelea kufanya kazi kulingana na 1Wakorintho 12:13. Kushuhudia ubatizo wa roho mmoja huwa mzingi wa kuwa na umoja wa Kanisa, kulingana na mkudhatha wa Waefeso 4:5. Kuwa na ushirika wa karibu na Kristo katika mauti yake, kuzikwa kwake na ufufuo wake kupitia kwa ubatizo wa Roho waweka mzingi wa kutenganishwa na nguvu za dhambi na kutembea katika maisha mapya. (Warumi 6:1-10; Wakolosai 2:12).
Pesquisar
Categorias
Leia Mais
Religion
MASWALI NA MAJIBU KUHUSU DHAMBI YA KUMKUFURU ROHO MTAKATIFU
Kumekuwepo na mijadala mingi kila mahali na pia kumewepo na maoni mengi ya watu na mawao tofauti...
Por GOSPEL PREACHER 2021-08-24 13:00:08 0 7K
Injili Ya Yesu Kristo
UTHIBITISHO WA UTATU WA MUNGU
Neno la Uzima kutoka kwa  Askofu Zachary Kakobe        ...
Por GOSPEL PREACHER 2022-01-12 00:36:40 0 5K
Injili Ya Yesu Kristo
YESU NI MWANA WA MUNGU
Je, ina maana gani Yesu kuwa Mwana wa Mungu    Ndugu Msomaji, Yesu si Mwana wa Mungu...
Por MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-22 05:24:13 0 5K
OTHERS
NANI KAMPA UTUME NA UNABII MTUME MUHAMMAD?
Twakusalimu kwa mara ingine katika jina tukufu na takatifu la Yesu Kristo Bwana wetu. Twazidi pia...
Por MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-22 04:46:10 0 5K
DANIEL
DANELI 6
Jina KUU la Bwana wetu YESU KRISTO libarikiwe. Ndugu mpenzi karibu tujifunze Neno la Mungu na...
Por GOSPEL PREACHER 2021-11-05 23:52:47 0 7K