Ubatizo wa Rohoho Mtakatifu ni nini?

0
5KB
Ubatizo wa Roho mtakatifu unaweza kufafanuliwa/kuelezwa kuwa ile kazi ambayo Roho Mtakatifu wa Mungu unamweka muumini kuwa na ushirika na Kristo na kwa ushirika na waumini wengine katika mwili wa Kristo wakati wa kuokolewa. Wakorintho wa kwanza 12:12-13 ni ukurasa wa katikati katika Bibilia kuhusu ubatizo wa Roho Mtakatifu, “Kwa maana katika Roho mmoja sisi sote tulibatizwa kuwa mwili mmoja, kwamba tu Wayahudi, au kwamba tu Wayunani; ikiwa tu watumwa au tu huru; nasi sote tulinyweshwa Roho mmoja.” (1Wakorintho 12:13). Bali Warumi 6:1-4 haitaji roho wa Mungu, bali yaelezea sehemu ya wakristo mbele za Mungu kwa lugha sawa na ile ya ujumbe wa kwanza Wakorintho: “Tusema nini basi? Tudumu kaitka dhambi ili neema izidi kuwa nyingi? Hasha! Sisi tulioifia dhambi tutaishije tena katika dhambi? Hamfahamu ya kuwa sisi sote tuliobatizwa katika Kristo Yesu tulibatizwa katika mauti yake? Basi tulizikwa pamoja kwa njia ya ubatizo katika mauti yake, kusudi kama Kristo alivyofufuka katika wafu kwa njia ya utukufu wa Baba, vivyo hivyo na sisi tuenende katika upya wa uzima.”
 
Hoja zifuatazo zatosha kudumisha uelefu wetu juu ya ubatizo wa Roho Mtakatifu. Kwanza, 1Wakorintho 12:13 yataja wazi kwamba wale wote waliobatizwa wananyweshwa Roho mmoja (kuwepo kwa Roho mtakatifu). Pili, hamna mahali katika Bibilia Wakristo wameelezwa wabatizwe, ndani ya, au kwa Roho au kwa vyovyote vile watafute ubatizo wa Roho Mtakatifu. Hii yaonyesha kuwa Wakrisot walikuwa na uzoevu. Tatu, Waefeso 4:5 yaonekana kuashiria ubatizo wa Roho. Kama hii ndio hali, ubatizo wa Roho Mtakatifu ni kitu cha kweli kwa kila Mkristo, kama vile “Imani mija” na “Baba mmoja” viko.
 
Kwa kumalizia, ubatizo wa Roho Mtakatifu wafanya mambo mawili, 1) Watuunganisha na mwili wa Kristo, na 2) Waambatanisha kusulubiwa kwetu na Yesu. Kuwa na mwili wake, yamaanisha, tumefufuliwa naye kwa upya wa uzima (Warumi 6:4). Kwa hivyo lazima tuviweka katika matendo vipawa vyetu vya Roho ili tuuweke mwili wa Kristo kuendelea kufanya kazi kulingana na 1Wakorintho 12:13. Kushuhudia ubatizo wa roho mmoja huwa mzingi wa kuwa na umoja wa Kanisa, kulingana na mkudhatha wa Waefeso 4:5. Kuwa na ushirika wa karibu na Kristo katika mauti yake, kuzikwa kwake na ufufuo wake kupitia kwa ubatizo wa Roho waweka mzingi wa kutenganishwa na nguvu za dhambi na kutembea katika maisha mapya. (Warumi 6:1-10; Wakolosai 2:12).
Rechercher
Catégories
Lire la suite
HOLY BIBLE
What are the keys of the kingdom?
The biblical passage that makes reference to the “keys of the kingdom” isMatthew...
Par MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-24 04:23:00 0 5KB
SPIRITUAL EDUCATION
USIUZE URIDHI WAKO ULIOKABIDHIWA KWA GHARAMA KUBWA MWANZO 25:27-34
USIUZE URIDHI WAKO ULIOKABIDHIWA KWA GHARAMA KUBWA MWANZO 25:27-34
Par Martin Laizer 2023-11-17 16:07:34 0 13KB
Religion
UFAHAMU KUHUSU DHAMBI YA KUMKUFURU ROHO MTAKATIFU
VIPENGELE VYA SOMO(1). NI MAANA YA KUKUFURU?(2). DHAMBI YA KUMKUFURU ROHO MTAKATIFU IKOJEE?(3)....
Par GOSPEL PREACHER 2021-08-24 12:44:21 4 9KB
Injili Ya Yesu Kristo
MAOMBI PEKE YAKE BILA IMANI HAYATOSHI KUTENGENEZA JIBU LA MAHITAJI YAKO.
Marko 9:14-29. Hii ni habari ya yule baba aliyekuwa na mwana mwenye pepo bubu na kiziwi, akamleta...
Par GOSPEL PREACHER 2021-11-23 12:47:11 0 5KB
EZRA
Verse by verse explanation of Ezra 10
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 25 questions at the...
Par THE HOLY BIBLE 2022-04-02 06:26:03 0 6KB