ALLAH ANASEMA KATIKA KORAN KUWA WAISLAM WOTE WATAINGIA JEHANNAM

0
7KB

Jamani huu ni Msiba katika taifa la Islam kwa kushindwa kusoma aya hii ambayo ipo wazi (Quran 40:60).

Katika mada hii, nitawawekea aya kutoka Koran na simulizi za Muhammad ambazo zinatushuhudia kuwa, Waislam wote wataingia Jehanamu.

Hebu tumsome kwanza Allah katika aya aliyo iteremsha kwa Mtume wake Muhammad (Pbuh).

Quran 40: 60. Na Mola wenu Mlezi anasema: Niombeni nitakuitikieni. Kwa hakika wale ambao wanajivuna na kuniabudu Mimi wataingia Jahannamu wadhalilike.

Mungu wa Waislam ajulikanaye kwa Jina la Allah amesema kiuwazi kabisa kuwa “wale wote ambao wanajivunia Uislam na kumuabudu Allah wataingia Motoni”


Ndugu zanguni, huu ni Msiba, tena msiba mkubwa sana katika dini na taifa la Kiislam. Allah amesha toa hukumu kwa wamfuatao na inafahamika fika kuwa, Wale wote waingiao Jehannam, hao walikuwa hawafanyi Mapenzi ya Mungu wa Biblia.  Allah anasema kuwa, ukifanya mapenzi yake, basi wewe utaingia Jehannam. Huu ushaidi ndio tulio usoma katika Quran 40:60.

Sasa tuwasikilize na maswahiba wa Mtume Muhammad.

Simulizi:

Pia imesimuliwa na Ibn Jarir, iliyosimuliwa na Abu Kurayb, imesimuliwa na Ibn Yaman, imesimuliwa na Ibn Malik Maghul, imesimuliwa na Ibn Ishaq ambaye alisema, "Kila mara Abu Maysarah anapo kwenda kulala na akiwa kitandani kwake yeye husema, 'Mimi nasikia Uchungu kuzaliwa na Mama yangu. 'na kisha anaanza kulia kwa Machozi. Alipoulizwa kwa nini alikuwa akilia, alijibu ayafuatayo,' Tuliambiwa kwamba SISI WAISLAMU tutaingia Jehannamu, LAKINI HATUKUAMBIWA kwamba TUTATOLEWA HUKO JEHANNAMU NA HATUKUAMBIWA NI KIVIPI TUTATOKA HUKO'"

Mfuasi huyu wa Muhammad anaoneka kupatwa na mshtuko mkubwa, pale alipo ambiwa kuwa, Waislam wote wataingia Jehannam. Mshtuko huu umemfanya ailaani siku ambayo alizaliwa. Kitu cha kujiuliza, kwanini Allah ambaye ni mungu wa Waislam anatoa ahadi ya Jehannam na si Akhera kama wafundishavyo Waislam?

Ndugu zanguni, ningependa mfahamu kuwa, utakapo ingia Jehannam, kutakuwa hakuna tena njia nyingine ya kutoka huko. Pale Jehannam ndio mwisho wa maisha ya walio tenda dhanb. Allah anasema kuwa, ukifanya mapenzi yake, basi wewe utaingia Jehannam. Je, kufanya mapenzi ya Allah ni sawa na kutenda dhanb? Je, Uislam ni dini ya haki, kama wanavyo sema wafundishaji wa dini hiyo? Jiulize tena, kwanini Allah anatoa ahadi ya Jehannam kwa wafuatayo mafundisho yake?

 

Lakini Yesu anasema haya:

Yohana 14: 6 Yesu akamwambia, Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi. 

Ndugu zanguni, mwamini Yesu ili uwe na uzima wa milele. Yesu anakupenda. Yesu Ndie Njia Pekee. Yesu Ndie Uzima. Dini haita kupeleka kwa Baba aliye Mbingu, lakini Yesu anasema Yeye NDIE NJIA.

Mungu awabariki sana.

Suche
Kategorien
Mehr lesen
HOLY BIBLE
FAHAMU UWEZO WA DAMU YA YESU KRISTO
Ukweli ni kwamba katika damu ya Yesu Kristo kunapatikana zaidi ya mambo manne...
Von MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-24 06:24:49 0 7KB
PSALMS
Verse by verse explanation of Psalm 7
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 25 questions at the...
Von THE HOLY BIBLE 2022-04-04 23:14:19 0 5KB
REVELATION
MAJIRA YA KANISA LA SARDI
(1) MLENGWA WA KANISAUFUNUO 3:1Na kwa malaika wa kanisa lililoko Sardi andika; Haya ndiyo anenayo...
Von GOSPEL PREACHER 2021-09-24 10:07:38 0 6KB
SPIRITUAL EDUCATION
Utakatifu ni nini kibiblia?
Utakatifu ni nini kibiblia?
Von Martin Laizer 2023-10-31 20:03:00 3 6KB
MAHUSIANO KIBIBLIA
JINSI YA KUISHINDA DHAMBI YA TAMAA ZA MWILI
WAGALATIA 5:16-17:-"Basi nasema, ENENDENI KWA ROHO, WALA HAMTAZITIMIZA KAMWE TAMAA ZA MWILI. Kwa...
Von GOSPEL PREACHER 2021-11-19 07:10:57 0 8KB