UKRISTO NI NINI?

0
5K
Neno Ukristo ni tegemezi ya kutoka kwa Jina "KRISTO". Hivyobasi, Mkristo ni mfuasi wa Kristo. Ni kama unavyoweza sema Mtanzania anatoka Tanzania na/au neno Mtanzania ni tegemezi kutoka Tanzania au Utanzania litakoka kwenye muungano wa U na Tanzania.
 
Lengo la mkristo ni kutafuta ushirika wa karibu na Mungu Baba. Ushirika huo unawezeshwa na kazi aliyoifanya Yesu pamoja na huduma ndani ya maisha ya mkristo ya Roho Mtakatifu.

Mungu Mtakatifu hana ushirika na dhambi. Kati yake na mwanadamu kuna ufa mkubwa wa dhambi. Mwanadamu hujaribu kumfikia Mungu kwa nija nyingi: DINI, matendo mema, sala, n.k., lakini hizi zote hazitoshi. Mwanadamu bado ni mwenye dhambi.
 
MAANA YA UKRISTO:
Ukristo ni imani maalum kulinganisha na nyinginezo, Kwa sababu inasimamia zaidi ushirika na Mungu kuliko matendo ya kidini. Kinyume na kushikilia orodha ya masharti ya fanya haya na usifanye yale, Lengo la mkristo ni kutafuta ushirika wa karibu na Mungu Baba. Ushirika huo unawezeshwa na kazi aliyoifanya Yesu pamoja na huduma ndani ya maisha ya mkristo ya Roho Mtakatifu.
Wakristo huamini ya kuwa biblia ni Neno la Mungu na mafundisho yake ndiyo mamlaka ya mwisho (Timotheo wa pili 3:16, Petro wa pili 1: 20-21). Wakristo huamini juu ya Mungu mmoja akaaye katika utatu, Baba na Mwana (Yesu kristo), na Roho Mtakatifu.
Wakristo huamini ya kuwa biblia ni Neno la Mungu na mafundisho yake ndiyo mamlaka ya mwisho (Timotheo wa pili 3:16, Petro wa pili 1: 20-21). Wakristo huamini juu ya Mungu mmoja akaaye katika utatu, Baba na Mwana (Yesu kristo), na Roho Mtakatifu.
 
MAANA YA DINI:
Dini ni jaribio la mwanadamu kuwa na uhusiano na Mungu. Imani ya kikristo ni uhusiano na Mungu kwa sababu yale ametufanyia kupitia kwa kusulubiwa kwa Yesu Kristo.
WALE WOTE WENYE MASWALI KUHUSU UKRISTO. Tafadhali uliza hapa na utajibiwa kiurefu sana.
UKRISTO SIO DINI BALI NI IMANI MAALUM INAYO SIMAMIA ZAIDI NA KUSHIRIKIANA NA MUNGU KULIKO MATENDO YA KIDINI.
 
Kuna njia moja tu ya kushirikiana na Mungu .
YESU KRISTO NI NJIA YA PEKEE YA KUONDOA DHAMBI.
Alikufa kwa ajili yetu ili tujue upendo na mpango wa Mungu kwa maisha yetu.
 
IMANI YA KWELI NI IPI?
Imani/Dini ya kweli sio ile ya kuangazia sheria bali ya kanuni. Imani ya kweli ni uhusiano na Mungu. Mambo mawili ambayo dini zote zashikilia ni kwamba mwanadamu kwa njia moja au nyingine ametengwa kutoka kwa Mungu na anahitaji kupatanishwa Naye. Dini za uongo zatafuta kuzuluhisha shida hii kwa kutunza sheria au kanuni. Imani ya kweli yazuluhisha tatizo kwa kutambua kwamba ni Mungu pekee anaweza kurekebisha utengano, na amekwisha fanya. Imani ya kweli yatambua yafuatayo:
• Wote tumetenda dhambi na kwa hivyo tumetenganishwa na Mungu (Warumi 3:23).
• Kama hautarekebishwa, adhabu ya haki ya dhambi ni mauti na utengano na Mungu wa milele baada ya kufa (Warumi 6:23).
• Mungu alikuja kwetu kupitia Kristo Yesu na akafa kwa ajili yetu, akachukua adhabu ambayo tulistahili, na akafufuka kutoka kwa wafu ili adhihirishe kuwa kifo chake kulikuwa dhabihu iliyotosha (Warumi 5:8; 1Wakorintho 15:3-4; 2Wakorintho 5:21)
• Kama tutampokea Yesu kama mwokozi wetu, kuamini kifo chake kama fidia kamili ya dhambi zetu, tumesamehewa, tumeokolewa, kombolewa, patanishwa na kufanywa wenye haki na Mungu (Yohana 3:16; Warumi 10:9-10; Waefeso 2:8-9).
 
MAANA YA UKRISTO KWA KIFUPI
Ukristo ni imani maalum kulinganisha na nyinginezo, Kwa sababu inasimamia zaidi ushirika na Mungu kuliko matendo ya kidini. Kinyume na kushikilia orodha ya masharti ya fanya haya na usifanye yale, Lengo la mkristo ni kutafuta ushirika wa karibu na Mungu Baba kupitia Mwana ambaye ni Yesu. Ushirika huo unawezeshwa na kazi aliyoifanya Yesu pamoja na huduma ndani ya maisha ya mkristo ya Roho Mtakatifu.
Wakristo huamini ya kuwa Biblia ni Neno la Mungu na mafundisho yake ndiyo mamlaka ya mwisho (Timotheo wa pili 3:16, Petro wa pili 1: 20-21). Wakristo huamini juu ya Mungu mmoja akaaye katika utatu, Baba na Mwana (Yesu kristo), na Roho Mtakatifu.

Kwa hivyo, huku dini nyingine zikitaka waumini wao watende mambo Fulani Fulani au wasitende mambo Fulani ukristo ni juu ya kuwa na ushirika na Mungu.

Hivyo Basi, Ukristo ni Ufuasi wa Kristo ambaye ni Mungu. Yesu Kristo ni Mungu.
Max Shimba Ministries
Search
Categories
Read More
EXODUS
Verse by verse explanation of Exodus 12
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 136 questions at the...
By THE HOLY BIBLE 2022-01-22 11:33:32 0 5K
MAHUSIANO KIBIBLIA
HIZI NI TABIA HATARISHI KWA MWANAMKE KATIKA MAHUSIANO: UCHUMBA HADI NDOA
KWELI KUU: Tabia ni msingi na kielelezo cha mahusiano bora ya aina yoyote na hasa yale ya uchumba...
By GOSPEL PREACHER 2021-11-07 23:18:56 0 10K
REVELATION
UFUNUO 22
Bwana wetu YESU KRISTO apewe sifa, Karibu katika mfululizo wa mwendelezo wa kitabu cha ufunuo leo...
By GOSPEL PREACHER 2021-10-30 18:55:33 0 6K
MASWALI & MAJIBU
Je! Wayahudi Wote Wataokolewa Kulingana Na Warumi 11:26?
SWALI: Je! Wayahudi wote wataokolewa? maana biblia inasema katika; Warumi 11:25...
By GOSPEL PREACHER 2022-06-13 00:22:40 0 5K
2 CHRONICLES
Verse by verse explanation of 2 Chronicles 36
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 30 questions at the...
By THE HOLY BIBLE 2022-04-02 02:39:04 0 6K